Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 31.12
Bible en Swahili de l’est


Dernières paroles de Moïse

Transmission des responsabilités à Josué

1 Musa akaenda akawaambia Waisraeli maneno haya yote.
2 Akawaambia, Mimi leo ni mwenye miaka mia na ishirini; siwezi tena kutoka na kuingia, na Bwana ameniambia, Hutavuka mto huu Yordani.
Deutéronome 34.7 Nombres 27.17 1 Rois 3.7 Exode 7.7 Deutéronome 3.26-3.27
3 Bwana Mungu wako, ndiye atakayevuka mbele yako, atawaangamiza mataifa haya mbele yako, nawe utawamiliki; na Yoshua atavuka mbele yako, kama Bwana alivyonena.
Deutéronome 9.3 Deutéronome 3.28 Psaumes 146.3-146.6 Genèse 48.21 Actes 7.45
4 Na Bwana atawatenda hao kama vile alivyowatenda Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, na nchi yao, ambao aliwaharibu.
Deutéronome 2.33 Deutéronome 3.21 Deutéronome 7.2 Deutéronome 7.16 Nombres 21.24-21.35
5 Naye Bwana atawatia mikononi mwenu, nanyi mtawatenda kadiri ya amri ile niliyowaamuru.
Deutéronome 7.2 Exode 34.12-34.16 Nombres 33.52-33.56 Deutéronome 7.23-7.25 Exode 23.32-23.33
6 Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana Bwana, Mungu wako, yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha.
Josué 1.9 1 Chroniques 28.20 Josué 10.25 Luc 12.32 Psaumes 27.14
7 Musa akamwita Yoshua, akamwambia machoni pa Israeli wote, Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana utakwenda pamoja na watu hawa hata nchi Bwana aliyowaapia baba zao, ya kwamba atawapa; nawe utawarithisha.
Deutéronome 3.28 Deutéronome 1.38 Deutéronome 31.6 Ephésiens 6.10 Daniel 10.19
8 Naye Bwana, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.
Deutéronome 31.6 Exode 33.14 Josué 1.9 Josué 1.5 Romains 8.31

Appel à lire régulièrement la loi

9 Musa akaiandika torati hii, akawapa makuhani, wana wa Lawi, waliolichukua sanduku la agano la Bwana, na wazee wote wa Israeli.
Josué 3.3 Nombres 4.15 Deutéronome 17.18 Deutéronome 31.28 Jean 1.17
10 Musa, akawaamuru, akasema, Mwisho wa kila mwaka wa saba, wakati wa maachilio, wakati ulioamriwa wa sikukuu ya vibanda,
Deutéronome 15.1-15.2 Lévitique 23.34-23.43
11 Israeli wote wafikapo ili kuonekana mbele za Bwana, Mungu wako, mahali pale atakapopachagua, uisome torati hii mbele ya Israeli wote masikioni mwao.
2 Rois 23.2 Josué 8.34-8.35 Deutéronome 12.5 Exode 23.16-23.17 Psaumes 84.7
12 Wakusanye watu, wanaume na wanawake na watoto, na mgeni wako aliyemo malangoni mwako wapate kusikia na kujifunza, na kumcha Bwana, Mungu wenu, na kuangalia kutenda maneno yote ya torati hii;
Deutéronome 4.10 Deutéronome 29.29 Deutéronome 6.6-6.7 Psaumes 19.7-19.11 Psaumes 34.11-34.14
13 na watoto wao wasiojua, wapate kusikia na kujifunza kumcha Bwana, Mungu wenu, siku zote mtakazokaa katika nchi mnayoivukia Yordani ili kuimiliki.
Deutéronome 11.2 Proverbes 22.6 Ephésiens 6.4 Deutéronome 6.7 Psaumes 78.4-78.8

Annonce de l’infidélité d’Israël

14 Bwana akamwambia Musa, Tazama, siku zako za kufa zinakaribia, umwite Yoshua, nanyi mkajihudhurishe katika hema ya kukutania, ili nipate kumwagiza kazi. Musa na Yoshua wakaenda, wakajihudhurisha ndani ya hema ya kukutania.
Nombres 27.13 Deutéronome 34.5 Deutéronome 31.23 Job 1.6 Deutéronome 32.50
15 Bwana akaonekana katika Hema katika nguzo ya wingu; na ile nguzo ya wingu ikasimama juu ya mlango wa Hema.
Psaumes 99.7 Exode 40.38 Exode 33.9-33.10
16 Bwana akamwambia Musa, Angalia, wewe utalala na baba zako; na watu hawa wataondoka, wataifuata kwa ukahaba miungu ya kigeni ya nchi waiendeayo kuwa kati yao, nao wataniacha mimi na kulivunja agano langu, nililofanya nao.
Juges 2.12 Juges 10.6 Juges 10.13 Actes 13.36 Exode 34.15
17 Ndipo hasira yangu itakapowaka juu yao siku hiyo, nami nitawaacha, nitawaficha uso wangu, nao wataliwa, tena watajiliwa na mambo maovu mengi na mashaka; hata waseme siku hiyo, Je! Kujiliwa kwetu na maovu haya si kwa sababu Mungu wetu hayumo kati yetu?
Nombres 14.42 Esaïe 8.17 Psaumes 104.29 2 Chroniques 15.2 Juges 6.13
18 Nami nitawaficha uso wangu kwa kweli siku hiyo, kwa maovu yote waliyoyafanya, kwa kuigeukia hiyo miungu mingine.
Deutéronome 31.16-31.17
19 Basi sasa jiandikieni wimbo huu, uwafundishe wana wa Israeli; kawatie vinywani mwao, ili uwe shahidi kwangu wimbo huu, juu ya wana wa Israeli.
Deutéronome 6.7 Deutéronome 31.26 Deutéronome 31.21-31.22 Esaïe 51.16 Jérémie 1.9
20 Kwa kuwa nitakapokwisha kuwatia katika nchi niliyowaapia baba zao, imiminikayo maziwa na asali; nao watakapokwisha kula na kushiba, na kuwanda; ndipo watakapoigeukia hiyo miungu mingine, na kuitumikia, na kunidharau mimi, na kulivunja agano langu.
Néhémie 9.25-9.26 Deutéronome 6.10-6.12 Osée 13.6 Jérémie 5.28 Exode 3.8
21 Tena itakuwa, wakiisha kujiliwa na mambo maovu mengi na mashaka, utashuhudia wimbo huu mbele yao kama shahidi, kwa maana hautasahauliwa katika vinywa vya uzao wao; kwani nayajua mawazo yao wayawazayo, hata sasa kabla sijawatia katika nchi niliyoapa.
Osée 5.3 Jean 2.24-2.25 Actes 4.28 Amos 5.25-5.26 Psaumes 139.2
22 Basi Musa akauandika wimbo huu siku iyo hiyo, akawafundisha wana wa Israeli.
Deutéronome 31.19 Deutéronome 31.9
23 Akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia, Uwe hodari na moyo mkuu, kwa kuwa utawapeleka wana wa Israeli katika nchi niliyowaapia; nami nitakuwa pamoja nawe.
Deutéronome 31.7-31.8 Deutéronome 31.14 Josué 1.5-1.9 Deutéronome 31.3 Actes 7.45
24 Basi ikawa hapo Musa alipomaliza kuandika maneno ya torati hii katika chuo, hata yakaisha,
Deutéronome 31.9 Deutéronome 17.18
25 ndipo Musa akawaamuru Walawi waliokuwa wakilichukua sanduku la agano la Bwana akawaambia,
Deutéronome 31.9
26 Twaeni chuo hiki cha torati, mkiweke kando ya sanduku la agano la Bwana, Mungu wenu, ili kiwepo kama shahidi juu yako.
Deutéronome 31.19 2 Chroniques 34.14-34.15 1 Rois 8.9 Galates 2.19 2 Rois 22.8-22.11
27 Kwa kuwa uasi wako naujua, na shingo yako ngumu; angalieni, mimi nikali hai pamoja nanyi leo, mmekuwa waasi juu ya Bwana; siuze nitakapokwisha kufa!
Deutéronome 32.20 Deutéronome 9.24 Actes 7.51 Psaumes 78.8 Exode 32.8-32.9
28 Nikutanishieni wazee wote wa kabila zenu, na maakida yenu, ili niseme maneno haya masikioni mwao, na kuwashuhudizia mbingu na nchi juu yao.
Deutéronome 4.26 Deutéronome 32.1 Deutéronome 30.19 Genèse 49.1-49.2 Luc 19.40
29 Kwa sababu najua baada ya kufa kwangu mtajiharibu kabisa, na kukengeuka katika njia niliyowaamuru; nayo mabaya yatawapata siku za mwisho, kwa vile mtakavyofanya maovu machoni pa Bwana kumtia kasirani kwa kazi ya mikono yenu.
Juges 2.19 Osée 9.9 Deutéronome 32.5 Genèse 49.1 2 Chroniques 34.24

Cantique de Moïse

30 Musa akasema maneno ya wimbo huu masikioni mwa kusanyiko la wana wa Israeli hata yakaisha.
Deutéronome 4.5 Actes 20.27 Hébreux 3.2 Hébreux 3.5 Jean 12.49

Cette Bible est dans le domaine public.