Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 18.13
Bible en Swahili de l’est


Les droits des Lévites et des prêtres

1 Makuhani Walawi, kabila yote ya Lawi, wasiwe na fungu wala urithi pamoja na Israeli; watakula sadaka za Bwana zifanywazo kwa moto, na urithi wake.
Deutéronome 10.9 Deutéronome 12.19 Nombres 18.20 Nombres 18.8-18.9 Josué 13.14
2 Wala wasiwe na urithi kati ya ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaambia.
Psaumes 16.5 1 Pierre 2.5 Psaumes 73.24-73.26 Psaumes 84.11 Apocalypse 1.5-1.6
3 Na hii itakuwa haki ya makuhani kwa watu hao wasongezao sadaka, ikiwa ni ng’ombe au kondoo wampe kuhani mkono, na mashavu mawili, na tumbo.
Lévitique 7.30-7.34 Deutéronome 12.27
4 Malimbuko ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na manyoya ya kwanza ya kondoo zako, umpe.
Lévitique 23.10 Lévitique 23.17 Exode 23.19 Exode 22.29 Néhémie 12.44-12.47
5 Kwani Bwana, Mungu wako, amemchagua katika kabila zako zote, asimame atumike kwa jina la Bwana, yeye na wanawe milele.
Deutéronome 10.8 Nombres 3.10 Deutéronome 17.12 Nombres 17.5-17.9 Nombres 16.9-16.10
6 Na akija Mlawi atokaye katika malango yako mojawapo, katika Israeli yote alipokuwa akikaa, akaja kwa mapenzi yote ya nafsi yake mahali atakapochagua Bwana;
Nombres 35.2-35.3 Deutéronome 12.5 Psaumes 27.4 Psaumes 84.5 Deutéronome 16.2
7 na atumike kwa jina la Bwana, Mungu wake, kama wafanyavyo ndugu zake wote, Walawi wasimamao huko mbele za Bwana.
2 Chroniques 31.2-31.4
8 Wawe na fungu sawasawa la kula, pamoja na haya yaliyomfikilia kwa kuuzwa urithi wa baba zake.
Néhémie 12.44 Néhémie 12.47 Luc 10.7 2 Chroniques 31.4 1 Timothée 5.17-5.18

Les prophètes et non la divination

9 Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.
Deutéronome 12.29-12.31 Lévitique 18.26-18.27 Lévitique 18.30
10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,
Lévitique 19.31 Lévitique 19.26 Exode 22.18 Deutéronome 12.31 2 Rois 17.17
11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.
Lévitique 19.31 1 Samuel 28.11-28.14
12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.
Lévitique 18.24 Deutéronome 9.4 Lévitique 18.27
13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako.
Matthieu 5.48 Genèse 6.9 Genèse 17.1 Job 1.8 Job 1.1
14 Maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanaoshika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe, Bwana, Mungu wako, hakukupa ruhusa kutenda hayo.
Genèse 20.6 Actes 14.16 Psaumes 147.19-147.20 Deutéronome 18.10
15 Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye.
Actes 7.37 Jean 1.25 Jean 1.21 Actes 3.22-3.23 Deutéronome 18.18-18.19
16 Kama vile ulivyotaka kwa Bwana, Mungu wako, huko Horebu, siku ya kusanyiko, ukisema, Nisisikie tena sauti ya Bwana, Mungu wangu, wala nisiuone tena moto huu mkubwa, nisije nikafa.
Exode 20.19 Deutéronome 5.23-5.28 Hébreux 12.19 Deutéronome 9.10
17 Bwana akaniambia, Wametenda vema kusema walivyosema.
Deutéronome 5.28
18 Mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.
Jean 8.28 Deutéronome 18.15 Jean 12.49-12.50 Esaïe 51.16 Jean 4.25
19 Hata itakuwa, mtu asiyesikiliza maneno yangu atakayosema yule kwa jina langu, nitalitaka kwake.
Actes 3.22-3.23 Hébreux 3.7 Hébreux 12.25-12.26 Hébreux 2.3 Hébreux 10.26
20 Lakini nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu, ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena katika jina la miungu mingine, nabii yule atakufa.
Deutéronome 13.1-13.5 Zacharie 13.3 Jérémie 23.13-23.15 Apocalypse 19.20 1 Rois 18.40
21 Nawe ukisema moyoni mwako, Tutajuaje neno asilolinena Bwana?
1 Jean 4.1-4.3 1 Thessaloniciens 5.24 Apocalypse 2.2
22 Atakaponena nabii kwa jina la Bwana, lisifuate jambo lile wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena Bwana; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimwogope
Deutéronome 18.20 Jérémie 28.1-28.17 Jonas 4.2 Proverbes 26.2 2 Rois 20.1

Cette Bible est dans le domaine public.