Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 17.16
Bible en Swahili de l’est


1 Usimchinjie Bwana, Mungu wako, ng’ombe wala kondoo aliye na kilema, wala neno ovu lo lote; kwa kuwa hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 15.21 Malachie 1.8 Deutéronome 24.4 Deutéronome 23.18 Deutéronome 25.16
2 Ikiwa ameonekana katikati yako, ndani ya malango yako mojawapo, upewayo na Bwana, Mungu wako, mtu mume au mke afanyaye yaliyo maovu machoni pa Bwana, Mungu wako, kwa kuvunja maagano yake,
Osée 8.1 Deutéronome 13.6-13.18 Josué 23.16 Osée 6.7 Josué 7.15
3 naye amekwenda kutumikia miungu mingine na kuiabudu, au jua, au mwezi, au vilivyo katika jeshi la mbinguni vyo vyote, nisivyoagiza mimi;
Deutéronome 4.19 Jérémie 7.22-7.23 Jérémie 19.5 Job 31.26-31.27 Jérémie 7.31
4 ukiambiwa hayo nawe umeyasikia, ndipo utafute kwa bidii, na tazama, ikiwa ni kweli lina hakika jambo lile, kuwa yafanywa machukizo kama hayo katika Israeli;
Deutéronome 19.18 Deutéronome 13.12-13.14 Jean 7.51 Proverbes 25.2
5 ndipo umchukue nje malangoni kwako, yule mtu mume, au yule mwanamke, aliyefanya jambo lile ovu; ukawapige kwa mawe, wafe.
Lévitique 24.14 Josué 7.25 Lévitique 24.16 Deutéronome 22.21 Deutéronome 21.21
6 Huyo atakayeuawa na auawe kwa midomo ya mashahidi wawili, au mashahidi watatu; asiuawe kwa mdomo wa shahidi mmoja.
Nombres 35.30 1 Timothée 5.19 Deutéronome 19.15 2 Corinthiens 13.1 Hébreux 10.28
7 Mikono ya wale mashahidi na iwe juu yake kwanza kwa kumwua, kisha mikono ya watu wote. Uondoe vivyo uovu katikati yako.
Deutéronome 13.9 Deutéronome 13.5 1 Corinthiens 5.13 Deutéronome 17.12 Deutéronome 19.19

Les juges

8 Ikiwa limezuka neno lililo zito kukupita wewe, katika maamuzi kati ya damu na damu, na kati ya daawa na daawa, na kati ya pigo na pigo, nayo yashindaniwa katika malango yako; ndipo nawe uondoke, ukwee uende mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako;
Deutéronome 12.5 Aggée 2.11 Deutéronome 19.4 Exode 22.2 Nombres 35.16
9 uwaendee makuhani Walawi, na mwamuzi atakayekuwako siku hizo; uwaulize; nao watakuonyesha hukumu ya maamuzi;
Ezéchiel 44.24 Malachie 2.7 Jérémie 18.18 Aggée 2.11 Deutéronome 19.17-19.21
10 nawe fanya sawasawa na hukumu watakayokuonyesha mahali hapo atakapochagua Bwana; nawe tunza kufanya kwa mfano wa yote watakayokufunza;
Matthieu 22.2-22.3
11 kwa mfano wa sheria watakayokufunza, na kwa mfano wa hukumu watakayokuambia, fanya vivyo; usigeuke katika hukumu watakayokuonyesha, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto.
Josué 1.7 1 Pierre 2.13-2.15 Malachie 2.8-2.9 Deutéronome 17.20 Deutéronome 25.1
12 Na mtu afanyaye kwa kujikinai, kwa kutomsikiza kuhani asimamaye hapo kwa kumtumikia Bwana, Mungu wako, au mwamuzi, na afe mtu huyo; nawe utauondoa uovu katika Israeli.
Nombres 15.30 Deutéronome 13.5 Deutéronome 18.7 Matthieu 10.14 1 Thessaloniciens 4.8
13 Na hao watu wote watasikia na kuogopa, wasifanye tena kwa kujikinai.
Deutéronome 13.11 Deutéronome 19.20 Nombres 15.30-15.31

Règles relatives à la royauté

14 Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako ukaimiliki, na kukaa humo; nawe utakaposema, Nitaweka mfalme juu yangu mfano wa mataifa yote yaliyo kando-kando yangu;
1 Samuel 8.19-8.20 Deutéronome 12.9-12.10 1 Samuel 8.5-8.7 Deutéronome 18.9 Deutéronome 11.31
15 usiache kumweka yule atakayechaguliwa na Bwana, Mungu wako, awe mfalme juu yako; umweke mmoja katika ndugu zako awe mfalme juu yako; usimtawaze mgeni juu yako, ambaye si ndugu yako.
Jérémie 30.21 1 Samuel 10.24 1 Chroniques 22.10 Matthieu 22.17 Psaumes 2.6
16 Ila asifanye farasi wake kuwa wengi, wala asiwarudishe watu Misri, ili apate kufanya farasi kuwa wengi; kwa kuwa Bwana amewaambia, Tangu sasa msirudie tena njia ile.
Deutéronome 28.68 1 Rois 4.26 Osée 11.5 Exode 13.17 Ezéchiel 17.15
17 Wala asijizidishie wake, ili moyo wake usikengeuke; wala asifanye fedha zake na dhahabu kuwa nyingi mno.
Néhémie 13.26 1 Rois 11.1-11.4 2 Samuel 3.2-3.5 1 Timothée 6.9 Genèse 2.24
18 Tena na iwe, zamani aketipo juu ya kiti cha ufalme wake, ajiandikie nakala ya torati hii katika chuo, kufuata hicho kilicho mbele ya makuhani Walawi;
Deutéronome 31.9 2 Rois 22.8 2 Rois 11.12 2 Chroniques 34.15 Deutéronome 31.24-31.26
19 na awe nayo, asome humo siku zote atakazoishi; ili apate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wake, ayashike maneno yote ya torati hii na amri hizi, kwa kuyafanya;
Josué 1.8 Psaumes 1.2 Psaumes 119.97-119.100 Jean 5.39 Deutéronome 4.10
20 moyo wake usije ukainuliwa juu ya ndugu zake, wala asikengeuke katika maagizo, kwa mkono wa kuume wala wa kushoto; ili apate kuzifanya siku zake kuwa nyingi katika ufalme wake, yeye na wanawe, katikati ya Israeli.
1 Rois 15.5 Deutéronome 5.32 1 Samuel 15.23 2 Chroniques 25.19 2 Chroniques 33.12

Cette Bible est dans le domaine public.