Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 10.16
Bible en Swahili de l’est


Défense de l’apostolat de Paul

Faiblesse et autorité de Paul

1 Basi, mimi Paulo mwenyewe nawasihi kwa upole na utaratibu wa Kristo; mimi niliye mnyenyekevu nikiwapo pamoja nanyi, bali nisipokuwapo ni mwenye ujasiri kwenu;
Matthieu 11.29 2 Corinthiens 10.10 Galates 5.2 Romains 12.1 Zacharie 9.9
2 naam, naomba kwamba nikiwapo, nisiwe na ujasiri kwa uthabiti ambao nahesabu kuwa nao juu ya wale wanaodhania ya kuwa sisi tunaenenda kwa jinsi ya mwili.
2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 13.2 Romains 8.5 Ephésiens 2.2-2.3 2 Corinthiens 11.9-11.13
3 Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;
2 Timothée 2.3-2.4 1 Pierre 4.1-4.2 2 Timothée 4.7 Romains 8.13 2 Corinthiens 10.4
4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
Jérémie 1.10 2 Corinthiens 6.7 2 Corinthiens 13.3-13.4 1 Corinthiens 2.5 1 Timothée 1.18
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
Matthieu 15.19 Romains 7.23 1 Pierre 1.14-1.15 Romains 1.21 Jérémie 4.14
6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia.
2 Corinthiens 2.9 2 Corinthiens 7.15 Nombres 16.26-16.30 1 Corinthiens 5.3-5.5 Actes 13.10-13.11
7 Yaangalieni yaliyo mbele ya macho yenu. Mtu akijitumainia mwenyewe ya kuwa ni mtu wa Kristo, na afikiri hivi pia nafsini mwake, ya kwamba kama yeye alivyo mtu wa Kristo, vivyo hivyo na sisi.
2 Corinthiens 5.12 2 Corinthiens 11.23 1 Corinthiens 14.37 Jean 7.24 1 Corinthiens 3.23
8 Maana, nijapojisifu zaidi kidogo kwa ajili ya mamlaka yetu, (tuliyopewa na Bwana, tupate kuwajenga wala si kuwaangusha), sitatahayarika;
2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 13.2-13.3 2 Corinthiens 13.8 Galates 1.1 2 Corinthiens 1.24
9 nisije nikaonekana kana kwamba nataka kuwaogofya kwa nyaraka zangu.
1 Corinthiens 4.5 2 Corinthiens 10.10 1 Corinthiens 4.19-4.21
10 Maana wasema, Nyaraka zake ni nzito, hodari; bali akiwapo mwenyewe mwilini ni dhaifu, na maneno yake si kitu.
1 Corinthiens 1.17 2 Corinthiens 11.6 Galates 4.13-4.14 1 Corinthiens 2.1-2.4 Exode 4.10
11 Mtu kama huyo na afikiri hivi, ya kwamba jinsi tulivyo kwa maneno katika nyaraka tusipokuwapo, ndivyo tulivyo kwa matendo tukiwapo.
2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 13.2-13.3 1 Corinthiens 4.19-4.20 2 Corinthiens 12.20
12 Kwa kuwa hatuthubutu kujihesabu pamoja na baadhi yao wanaojisifu wenyewe, wala kujilinganisha nao; bali wao wenyewe wakijipima nafsi zao na nafsi zao, na wakijilinganisha nafsi zao na nafsi zao, hawana akili.
2 Corinthiens 3.1 Proverbes 27.2 Proverbes 26.12 Luc 18.11 2 Corinthiens 10.18
13 Lakini sisi hatutajisifu zaidi ya kadiri yetu; bali kwa kadiri ya kipimo tulichopimiwa na Mungu, yaani, kadiri ya kufika hata kwenu.
Romains 15.20 Esaïe 28.17 Proverbes 25.14 2 Corinthiens 10.14-10.15 Romains 10.18
14 Maana hatujitanui nafsi zetu kupita kadiri yetu, kana kwamba hatuwafikii ninyi; kwa sababu tulitangulia kufika mpaka kwenu katika injili ya Kristo;
1 Corinthiens 4.15 1 Timothée 1.11 Romains 16.25 1 Corinthiens 2.10 Actes 20.24
15 wala hatujisifu zaidi ya kadiri yetu, yaani, katika taabu za watu wengine; bali tukiwa na tumaini ya kwamba, imani yenu ikuapo, tutakuzwa kwenu kwa kadiri ya kipimo chetu, na kupata ziada;
Romains 15.20 2 Corinthiens 10.13 2 Thessaloniciens 1.3 Actes 5.13
16 hata kuihubiri Injili katika nchi zilizo mbele kupita nchi zenu; tusijisifu katika kipimo cha mtu mwingine kwa mambo yaliyokwisha kutengenezwa.
Romains 15.24-15.28 Actes 19.21
17 Lakini, Yeye ajisifuye, na ajisifu katika Bwana.
Jérémie 9.23-9.24 1 Corinthiens 1.31 Jérémie 4.2 Psaumes 106.5 Esaïe 65.16
18 Maana mtu mwenye kukubaliwa si yeye ajisifuye, bali yeye asifiwaye na Bwana.
Romains 2.29 2 Corinthiens 10.12 1 Corinthiens 4.5 1 Pierre 1.7 Proverbes 27.2

Cette Bible est dans le domaine public.