Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 27.12
Bible en Swahili de l’est


Loi sur les héritages

1 Wakati huo wakakaribia hao binti za Selofehadi, mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, wa jamaa za Manase mwana wa Yusufu; na majina ya hao binti za Selofehadi ni haya; Mala, na Noa, na Hogla, na Milka, na Tirsa.
Nombres 26.33 Galates 3.28 Nombres 36.1-36.12 1 Chroniques 7.15 Josué 17.3-17.6
2 Nao wakasimama mbele ya Musa, na mbele ya Eleazari kuhani, na mbele ya wakuu, na mkutano wote, mlangoni pa hema ya kukutania, wakasema,
Deutéronome 17.8-17.10 Nombres 15.33-15.34 Exode 18.13-18.14 Exode 18.19-18.26
3 Babaetu alikufa nyikani, naye hakuwamo katika mkutano wa hao waliojikutanisha kinyume cha Bwana katika mkutano wa Kora; lakini akafa katika dhambi zake mwenyewe; naye alikuwa hana wana wa kiume.
Nombres 26.64-26.65 Ezéchiel 18.4 Nombres 14.35 Nombres 16.32-16.35 Nombres 16.49
4 Kwa nini basi jina la babaetu kufutwa katika jamaa zake kwa sababu alikuwa hana mwana wa kiume? Tupe sisi urithi pamoja na ndugu zake babaetu.
Josué 17.4 Exode 32.11 Proverbes 13.9 Psaumes 109.13
5 Basi Musa akaleta neno lao mbele ya Bwana
Job 23.4 Proverbes 3.5-3.6 Lévitique 24.12-24.13 Exode 18.15-18.19 Exode 25.22
6 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
Psaumes 68.5-68.6 Galates 3.28
7 Hao binti za Selofehadi wananena lililo haki; kweli utawapa milki ya urithi pamoja na ndugu za baba yao; nawe utawapa urithi wa baba yao.
Galates 3.28 Jérémie 49.11 Nombres 36.1-36.2 Josué 17.4 Psaumes 68.5
8 Kisha utanena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Mtu akifa, naye hana mwana wa kiume, ndipo utampa binti yake urithi wake.
9 Tena ikiwa hana binti, mtawapa nduguze urithi wake.
10 Na ikiwa hana ndugu, mtawapa ndugu za babaye huo urithi wake.
11 Tena ikiwa babaye hana ndugu, utampa huyo aliye karibu naye katika jamaa zake huo urithi wake, naye atakuwa nao; na neno hili litakuwa ni amri ya hukumu kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Nombres 35.29 Ruth 4.3-4.6 Jérémie 32.8 1 Samuel 30.25 Lévitique 25.25

Josué désigné comme successeur de Moïse

12 Bwana akamwambia Musa, Panda wewe juu ya mlima huu wa Abarimu, uitazame nchi niliyowapa wana wa Israeli.
Nombres 33.47-33.48 Deutéronome 32.48-32.52 Deutéronome 3.23-3.27 Deutéronome 34.1-34.4
13 Na ukiisha kuiona, wewe nawe utakusanyika pamoja na baba zako, kama Haruni ndugu yako alivyokusanyika;
Nombres 31.2 Deutéronome 10.6 Nombres 20.24-20.28 Genèse 25.8 Nombres 33.38
14 kwa sababu mliasi juu ya neno langu katika jangwa la Sini wakati wa mateto ya mkutano, wala hamkunistahi, hapo majini, mbele ya macho yao. (Maji hayo ndiyo maji ya Meriba ya Kadeshi katika jangwa la Sini.)
Exode 17.7 Nombres 20.24 Deutéronome 32.51-32.52 Nombres 20.8-20.13 Deutéronome 1.37
15 Musa akanena na Bwana akisema,
16 Bwana, Mungu wa roho za wenye mwili wote, na aweke mtu juu ya mkutano,
Nombres 16.22 Jérémie 23.4-23.5 Actes 20.28 Matthieu 9.38 Ezéchiel 37.24
17 atakayetoka mbele yao, na kuingia mbele yao; atakayewaongoza watokapo, na kuwaleta ndani; ili mkutano wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.
1 Rois 22.17 Deutéronome 31.2 Marc 6.34 Ezéchiel 34.5 Matthieu 9.36
18 Bwana akamwambia Musa, Mtwae Yoshua, mwana wa Nuni, mtu mwenye roho ndani yake, ukamwekee mkono wako;
Deutéronome 34.9 Nombres 27.23 Genèse 41.38 Juges 3.10 Daniel 5.14
19 kisha ukamweke mbele ya Eleazari kuhani, na mbele ya mkutano wote; ukampe mausia mbele ya macho yao.
Deutéronome 3.28 1 Timothée 5.21 Deutéronome 31.23 Luc 10.2-10.11 2 Timothée 4.1-4.6
20 Nawe utaweka juu yake sehemu ya heshima yako, ili mkutano wote wa wana wa Israeli wapate kutii.
Josué 1.16-1.18 2 Rois 2.15 Nombres 11.17 1 Samuel 10.6 2 Rois 2.9-2.10
21 Naye atasimama mbele ya Eleazari kuhani, naye atamwulizia kwa hukumu ya ile Urimu mbele za Bwana; kwa neno lake watatoka, na kwa neno lake wataingia; yeye na wana wa Israeli wote pamoja naye, mkutano wote pia.
Exode 28.30 Josué 9.14 1 Samuel 28.6 Juges 20.18 Juges 1.1
22 Musa akafanya kama Bwana alivyomwamuru; akamtwaa Yoshua, akamweka mbele ya Eleazari kuhani, na mbele ya mkutano wote;
23 kisha akaweka mikono yake juu yake, akampa mausia, kama Bwana alivyosema kwa mkono wa Musa.
Nombres 27.19 Deutéronome 3.28 Deutéronome 31.7-31.8

Cette Bible est dans le domaine public.