Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 12.8
Bible en Swahili de l’est


Miriam frappée de lèpre

1 Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.
Exode 2.21 Genèse 34.14-34.15 Matthieu 12.48 Jean 15.20 Genèse 26.34-26.35
2 Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? Bwana akasikia maneno yao.
Nombres 11.1 2 Rois 19.4 Esaïe 37.4 Ezéchiel 35.12-35.13 Nombres 16.3
3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.
Matthieu 11.29 2 Corinthiens 11.5 2 Corinthiens 12.11 Nombres 20.10-20.12 Psaumes 147.6
4 Bwana akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje.
Nombres 16.16-16.21 Psaumes 76.9
5 Bwana akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili.
Nombres 11.25 Exode 34.5 Exode 40.38 Psaumes 99.7
6 Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto.
1 Rois 3.5 Genèse 46.2 Genèse 31.10-31.11 Luc 1.22 Daniel 7.1
7 Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;
Psaumes 105.26 Hébreux 3.2-3.6 Josué 1.1 Actes 3.22-3.23 Matthieu 11.11
8 Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?
Deutéronome 34.10 Exode 33.11 1 Corinthiens 13.12 Exode 33.23 Psaumes 49.4
9 Hasira za Bwana zikawaka juu yao; naye akaenda zake.
Nombres 11.1 Osée 5.15 Genèse 17.22
10 Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.
Deutéronome 24.9 2 Rois 5.27 Exode 33.7-33.10 2 Chroniques 26.19-26.21 Matthieu 25.41
11 Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi.
2 Samuel 19.19 2 Samuel 24.10 Proverbes 30.32 1 Samuel 15.24-15.25 1 Samuel 2.30
12 Nakusihi, asiwe kama mmoja aliyekufa, ambaye nyama ya mwili wake nusu imelika hapo atokapo tumbo la mama yake.
Ephésiens 2.1-2.5 1 Corinthiens 15.8 1 Timothée 5.6 Colossiens 2.13 Psaumes 58.8
13 Musa akamlilia Bwana, akasema, Mpoze, Ee Mungu, nakusihi sana.
Exode 32.10-32.14 Esaïe 30.26 1 Samuel 12.23 Jacques 5.15 Matthieu 5.44-5.45
14 Bwana akamwambia Musa, Je! Kama baba yake angalimtemea mate usoni tu, hangaliona aibu muda wa siku saba? Na afungwe nje ya kambi muda wa siku saba, kisha baada ya hayo ataletwa ndani tena.
Deutéronome 25.9 Job 30.10 Nombres 5.2-5.3 Esaïe 50.6 Matthieu 26.67
15 Basi Miriamu alifungwa nje ya kambi muda wa siku saba; wala watu hawakusafiri hata Miriamu alipoletwa ndani tena.
Michée 7.8-7.9 Deutéronome 24.8-24.9 Habakuk 3.2 Michée 6.4 Exode 20.12
16 Baada ya hayo watu wakasafiri kutoka Haserothi, wakapanga kambi katika nyika ya Parani.
Nombres 11.35 Nombres 10.12 Nombres 33.18 Genèse 21.21 1 Samuel 25.1

Cette Bible est dans le domaine public.