Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 12.16
Bible en Swahili de l’est


Miriam frappée de lèpre

1 Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.
Exode 2.21 Exode 2.16 Jean 7.5 Matthieu 10.36 Galates 4.16
2 Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? Bwana akasikia maneno yao.
Nombres 11.1 Ezéchiel 35.12-35.13 Nombres 16.3 Michée 6.4 2 Rois 19.4
3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.
Matthieu 11.29 2 Corinthiens 11.5 2 Corinthiens 12.11 Psaumes 149.4 Jacques 3.2-3.3
4 Bwana akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje.
Nombres 16.16-16.21 Psaumes 76.9
5 Bwana akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili.
Nombres 11.25 Exode 34.5 Exode 40.38 Psaumes 99.7
6 Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto.
1 Rois 3.5 Genèse 46.2 Genèse 31.10-31.11 Actes 22.17-22.18 Actes 10.11
7 Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;
Psaumes 105.26 Hébreux 3.2-3.6 Josué 1.1 Deutéronome 18.18 Actes 7.31
8 Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?
Deutéronome 34.10 Exode 33.11 1 Corinthiens 13.12 Exode 33.23 Psaumes 49.4
9 Hasira za Bwana zikawaka juu yao; naye akaenda zake.
Osée 5.15 Genèse 17.22 Nombres 11.1
10 Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.
Deutéronome 24.9 2 Rois 5.27 Osée 9.12 Ezéchiel 10.4-10.5 Exode 4.6
11 Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi.
2 Samuel 24.10 2 Samuel 19.19 Proverbes 30.32 2 Chroniques 16.9 1 Rois 13.6
12 Nakusihi, asiwe kama mmoja aliyekufa, ambaye nyama ya mwili wake nusu imelika hapo atokapo tumbo la mama yake.
Psaumes 88.4-88.5 Job 3.16 Ephésiens 2.1-2.5 1 Corinthiens 15.8 1 Timothée 5.6
13 Musa akamlilia Bwana, akasema, Mpoze, Ee Mungu, nakusihi sana.
Nombres 14.2 Nombres 16.41 Nombres 14.13-14.20 1 Samuel 15.11 Jérémie 17.14
14 Bwana akamwambia Musa, Je! Kama baba yake angalimtemea mate usoni tu, hangaliona aibu muda wa siku saba? Na afungwe nje ya kambi muda wa siku saba, kisha baada ya hayo ataletwa ndani tena.
Job 30.10 Deutéronome 25.9 Nombres 5.2-5.3 Esaïe 50.6 2 Chroniques 26.20-26.21
15 Basi Miriamu alifungwa nje ya kambi muda wa siku saba; wala watu hawakusafiri hata Miriamu alipoletwa ndani tena.
Genèse 9.21-9.23 Lamentations 3.32 Michée 7.8-7.9 Deutéronome 24.8-24.9 Habakuk 3.2
16 Baada ya hayo watu wakasafiri kutoka Haserothi, wakapanga kambi katika nyika ya Parani.
Nombres 11.35 Nombres 10.12 Nombres 33.18 Nombres 13.26 Nombres 13.3

Cette Bible est dans le domaine public.