Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 5.9
Bible en Swahili de l’est


Vision d’un rouleau volant

1 Basi, nikainua macho yangu tena, nikaona, na tazama, gombo la chuo lirukalo.
Ezéchiel 2.9-2.10 Jérémie 36.1-36.6 Apocalypse 10.2 Apocalypse 5.1-5.14 Apocalypse 10.8-10.11
2 Akaniuliza, Unaona nini? Nikajibu, Naona gombo la chuo lirukalo; na urefu wake ni dhiraa ishirini, na upana wake dhiraa kumi.
Zacharie 4.2 2 Pierre 2.3 Genèse 6.11-6.13 Jérémie 1.11-1.14 Amos 7.8
3 Ndipo akaniambia, Hii ndiyo laana itokayo kwenda juu ya uso wa nchi yote; maana kwa hiyo kila aibaye atatolewa kama ilivyo upande mmoja, na kwa hiyo kila aapaye atatolewa kama ilivyo upande wa pili.
Exode 20.15 Esaïe 48.1 Esaïe 24.6 Esaïe 43.28 Malachie 4.6
4 Nitaituma itokee, asema Bwana wa majeshi, nayo itaingia katika nyumba ya mwivi, na katika nyumba yake yeye aapaye kwa uongo kwa jina langu; nayo itakaa katikati ya nyumba yake, na kuiteketeza, pamoja na boriti zake na mawe yake.
Habakuk 2.9-2.11 Job 18.15 Malachie 3.5 Lévitique 14.34-14.45 Proverbes 3.33

Vision d’une femme

5 Ndipo yule malaika aliyesema nami akatokea, akaniambia, Inua macho yako sasa, uone ni kitu gani kitokeacho.
Zacharie 1.9 Zacharie 1.19 Zacharie 2.3 Zacharie 4.5 Zacharie 1.14
6 Nikasema, Ni kitu gani? Akasema, Kitu hiki ni efa itokeayo. Tena akasema, Huu ndio uovu wao katika nchi hii yote;
Amos 8.5 Ezéchiel 44.10-44.11
7 na tazama, talanta ya risasi iliinuliwa; na tazama, mwanamke akaaye katikati ya hiyo efa.
Osée 1.1-1.3 Ezéchiel 23.1-23.49 Esaïe 13.1 Jérémie 3.1-3.2 Esaïe 22.11
8 Akasema, Huyu ni Uovu; akamtupa chini katikati ya ile efa; akalitupa lile jiwe la risasi juu ya mdomo wa ile efa.
Genèse 15.16 1 Thessaloniciens 2.16 Matthieu 23.32 Michée 6.11 Proverbes 5.22
9 Ndipo nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, wanawake wawili walitokea, nao upepo ulikuwa katika mabawa yao; na mabawa yao yalikuwa kama mabawa ya korongo; wakaiinua ile efa kati ya dunia na mbingu.
Lévitique 11.19 Daniel 9.26-9.27 Osée 8.1 Matthieu 24.28 Deutéronome 28.49
10 Ndipo nikamwambia yule malaika aliyesema nami, Hawa wanaipeleka wapi efa hii?
11 Akaniambia, Wanakwenda kumjengea nyumba katika nchi ya Shinari; tena ikiisha kutengenezwa, atawekwa huko mahali pake mwenyewe.
Genèse 11.2 Daniel 1.2 Genèse 10.10 Genèse 14.1 Jérémie 29.28

Cette Bible est dans le domaine public.