Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 5.11
Bible en Swahili de l’est


Vision d’un rouleau volant

1 Basi, nikainua macho yangu tena, nikaona, na tazama, gombo la chuo lirukalo.
Esaïe 8.1 Zacharie 5.2 Jérémie 36.20-36.24 Ezéchiel 2.9-2.10 Jérémie 36.1-36.6
2 Akaniuliza, Unaona nini? Nikajibu, Naona gombo la chuo lirukalo; na urefu wake ni dhiraa ishirini, na upana wake dhiraa kumi.
Zacharie 4.2 Amos 7.8 Apocalypse 18.5 Sophonie 1.14 2 Pierre 2.3
3 Ndipo akaniambia, Hii ndiyo laana itokayo kwenda juu ya uso wa nchi yote; maana kwa hiyo kila aibaye atatolewa kama ilivyo upande mmoja, na kwa hiyo kila aapaye atatolewa kama ilivyo upande wa pili.
Exode 20.15 Esaïe 43.28 Esaïe 48.1 Esaïe 24.6 Lévitique 19.12
4 Nitaituma itokee, asema Bwana wa majeshi, nayo itaingia katika nyumba ya mwivi, na katika nyumba yake yeye aapaye kwa uongo kwa jina langu; nayo itakaa katikati ya nyumba yake, na kuiteketeza, pamoja na boriti zake na mawe yake.
Lévitique 14.34-14.45 Proverbes 3.33 Habakuk 2.9-2.11 Job 18.15 Malachie 3.5

Vision d’une femme

5 Ndipo yule malaika aliyesema nami akatokea, akaniambia, Inua macho yako sasa, uone ni kitu gani kitokeacho.
Zacharie 1.9 Zacharie 2.3 Zacharie 4.5 Zacharie 1.14 Zacharie 1.19
6 Nikasema, Ni kitu gani? Akasema, Kitu hiki ni efa itokeayo. Tena akasema, Huu ndio uovu wao katika nchi hii yote;
Amos 8.5 Ezéchiel 44.10-44.11
7 na tazama, talanta ya risasi iliinuliwa; na tazama, mwanamke akaaye katikati ya hiyo efa.
Ezéchiel 16.1-16.63 Esaïe 15.1 Apocalypse 17.1-17.18 Osée 1.1-1.3 Ezéchiel 23.1-23.49
8 Akasema, Huyu ni Uovu; akamtupa chini katikati ya ile efa; akalitupa lile jiwe la risasi juu ya mdomo wa ile efa.
Lamentations 1.14 Psaumes 38.4 Zacharie 5.7 Genèse 15.16 1 Thessaloniciens 2.16
9 Ndipo nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, wanawake wawili walitokea, nao upepo ulikuwa katika mabawa yao; na mabawa yao yalikuwa kama mabawa ya korongo; wakaiinua ile efa kati ya dunia na mbingu.
Osée 8.1 Matthieu 24.28 Deutéronome 28.49 Lévitique 11.19 Daniel 9.26-9.27
10 Ndipo nikamwambia yule malaika aliyesema nami, Hawa wanaipeleka wapi efa hii?
11 Akaniambia, Wanakwenda kumjengea nyumba katika nchi ya Shinari; tena ikiisha kutengenezwa, atawekwa huko mahali pake mwenyewe.
Genèse 11.2 Genèse 10.10 Daniel 1.2 Jérémie 29.28 Esaïe 11.11

Cette Bible est dans le domaine public.