Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Sophonie 2.8
Bible en Swahili de l’est


1 Jikusanyeni, naam, jikusanyeni, Ee taifa lisilo na haya;
2 Chroniques 20.4 Joël 1.14 Jérémie 6.15 Jérémie 12.7-12.9 Esaïe 26.8-26.9
2 kabla haijazaa hiyo amri, kabla haijapita siku ile kama makapi, kabla haijawajilia hasira kali ya Bwana, kabla haijawajilia siku ya hasira ya Bwana.
Osée 13.3 Nahum 1.6 Lamentations 4.11 Esaïe 17.13 Psaumes 1.4
3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya Bwana.
Amos 5.14-5.15 Psaumes 57.1 Esaïe 26.20-26.21 Psaumes 76.9 Matthieu 5.5

Jugement des nations

4 Kwa kuwa Gaza utaachwa, na Ashkeloni utakuwa ukiwa; wataufukuzia mbali Ashdodi wakati wa adhuhuri, na Ekroni utang’olewa.
Zacharie 9.5-9.7 Amos 1.6-1.8 Ezéchiel 25.15-25.17 Jérémie 6.4 Jérémie 15.8
5 Ole wao wakaao karibu na pwani ya bahari, taifa la Wakerethi! Neno la Bwana li juu yenu, Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti; mimi nitakuangamiza, asibaki mtu akaaye kwako.
Ezéchiel 25.16 Amos 3.1 Josué 13.3 Jérémie 47.7 Amos 5.1
6 Na hiyo nchi ya pwani itakuwa malisho, yenye vibanda vya wachungaji, na mazizi ya makundi ya kondoo.
Esaïe 5.17 Sophonie 2.14-2.15 Ezéchiel 25.5 Esaïe 17.2
7 Na hiyo nchi ya pwani itakuwa nchi ya watu wa nyumba ya Yuda waliosalia; watalisha makundi yao huko; watalala katika nyumba za Ashkeloni wakati wa jioni; kwa maana Bwana, Mungu wao, atawajilia na kuwarudisha wafungwa wao.
Sophonie 3.20 Abdias 1.19 Exode 4.31 Luc 1.68 Romains 11.5
8 Mimi nimeyasikia matukano ya Moabu, na dhihaka za wana wa Amoni, ambazo kwa hizo wamewatukana watu wangu, na kujitukuza juu ya mpaka wao.
Amos 1.13 Jérémie 49.1 Ezéchiel 36.2 Psaumes 83.4-83.7 Jérémie 48.27-48.29
9 Basi kama niishivyo, asema Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, Hakika Moabu atakuwa kama Sodoma, na wana wa Amoni kama Gomora, yaani, milki ya upupu, na mashimo ya chumvi, ukiwa wa daima; watu wangu waliosalia watawateka nyara, na watu wa taifa langu waliobaki watawarithi.
Deutéronome 29.23 Esaïe 15.1-15.9 Esaïe 11.14 Esaïe 49.18 Michée 5.7-5.8
10 Mambo hayo yatawapata kwa sababu ya kiburi chao, kwa kuwa wamewatukana watu wa Bwana wa majeshi, na kujitukuza juu yao.
Esaïe 16.6 Sophonie 2.8 Exode 10.3 1 Pierre 5.5 Ezéchiel 38.14-38.18
11 Bwana atakuwa mwenye kuwatisha sana; kwa maana atawafisha kwa njaa miungu yote ya dunia; na watu watamsujudia yeye, kila mtu toka mahali pake; naam, nchi zote za mataifa.
Genèse 10.5 Psaumes 72.8-72.11 Psaumes 138.4 Sophonie 3.9 Psaumes 117.1-117.2
12 Na ninyi Wakushi pia, mtauawa kwa upanga wangu.
Ezéchiel 30.4-30.9 Esaïe 18.1-18.7 Esaïe 20.4-20.5 Esaïe 13.5 Jérémie 46.9-46.10
13 Naye atanyosha mkono wake juu ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza Ashuru; naye ataufanya Ninawi kuwa ukiwa, kuwa mahali pakavu kama jangwa.
Nahum 3.7 Nahum 1.1 Esaïe 10.12 Esaïe 10.16 Nahum 2.10-2.11
14 Na makundi ya wanyama watalala kati yake, wanyama wote wa mataifa; mwari-nyuni na nungu watakaa juu ya vichwa vya nguzo zake; sauti yao itasikiwa madirishani; vizingitini mwake mtakuwa ukiwa; kwa maana ameifunua kazi ya mierezi.
Jérémie 22.14 Amos 9.1 Esaïe 14.23 Esaïe 34.11-34.17 Apocalypse 18.2
15 Huu ndio mji ule wa furaha, Uliokaa pasipo kufikiri, Uliosema moyoni mwake, Mimi niko, Wala hapana mwingine ila mimi. Jinsi ulivyokuwa ukiwa, Mahali pa kulala pa wanyama wa bara! Kila mtu apitaye atazomea, Na kutikisa mkono wake.
Ezéchiel 28.2 Nahum 3.19 Esaïe 22.2 Esaïe 47.7-47.8 Ezéchiel 28.9

Cette Bible est dans le domaine public.