Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Michée 1.1
Bible en Swahili de l’est


Menaces contre Israël et Juda

1 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia Mika, Mmorashti, katika siku za Yothamu, na Ahazi, na Hezekia, wafalme wa Yuda; maono aliyoyaona katika habari za Samaria, na Yerusalemu.
Esaïe 1.1 Jérémie 26.18 Osée 1.1 Amos 1.1 2 Chroniques 27.1-27.9
2 Sikilizeni, enyi watu wa kabila zote; sikiliza, Ee dunia, na vyote vilivyomo; Bwana MUNGU na ashuhudie juu yenu, yeye Bwana kutoka hekalu lake takatifu.
Esaïe 1.2 Psaumes 11.4 Jonas 2.7 Michée 6.1-6.2 Habakuk 2.20
3 Kwa maana, angalieni, Bwana anakuja akitoka mahali pake, naye atashuka, na kupakanyaga mahali pa dunia palipoinuka.
Amos 4.13 Esaïe 26.21 Psaumes 115.3 Deutéronome 32.13 Esaïe 25.10
4 Na hiyo milima itayeyuka chini yake, nayo mabonde yatapasuliwa, kama vile nta iliyo mbele ya moto, kama maji yaliyomwagika tena kutelemka gengeni.
Nahum 1.5 Psaumes 97.5 Esaïe 64.1-64.3 Juges 5.4 Amos 9.5
5 Kwa sababu ya kosa la Yakobo yametokea haya yote, na kwa sababu ya makosa ya nyumba ya Israeli. Nini kosa la Yakobo? Je, silo Samaria? Na nini mahali pa Yuda palipoinuka? Sipo Yerusalemu?
Amos 8.14 Jérémie 2.19 Jérémie 4.18 Lamentations 5.16 Osée 8.5-8.6
6 Kwa ajili ya hayo nitafanya Samaria kuwa kama chungu katika shamba, na kama miche ya shamba la mizabibu; nami nitayatupa mawe yake bondeni, nami nitaifunua misingi yake.
Ezéchiel 13.14 Michée 3.12 2 Rois 19.25 Lamentations 4.1 Amos 5.11
7 Na sanamu zake zote za kuchonga zitapondwa-pondwa, na ijara zake zote zitateketezwa kwa moto, na sanamu zake zote nitazifanya ukiwa; kwa kuwa amezikusanya kwa ujira wa kahaba, nazo zitaurudia ujira wa kahaba.
Osée 2.12 Deutéronome 23.18 Osée 8.6 Apocalypse 18.12-18.13 2 Chroniques 31.1
8 Kwa ajili ya hayo nitaomboleza na kulia, Nitakwenda nimevua nguo, ni uchi; Nitafanya mlio kama wa mbweha, Na maombolezo kama ya mbuni.
Esaïe 20.2-20.4 Esaïe 22.4 Job 30.29 Jérémie 9.1 Jérémie 9.10
9 Kwa maana jeraha zake haziponyekani; Maana msiba umeijilia hata Yuda, Unalifikia lango la watu wangu, Naam, hata Yerusalemu.
2 Chroniques 32.1-32.23 Esaïe 8.7-8.8 Michée 1.12 Jérémie 15.18 2 Rois 18.9-18.13
10 Msiyahubiri haya katika Gathi, msilie kamwe; Katika Beth-le-Afra ugae-gae mavumbini.
2 Samuel 1.20 Jérémie 6.26 Job 2.8 Josué 18.23 Lamentations 3.29
11 Piteni; uende ukaaye Shafiri, hali ya uchi na aibu; Hivyo akaaye Saanani hajatokea nje; Maombolezo ya Beth-eseli yatawaondolea tegemeo lake;
Esaïe 20.4 Jérémie 13.22 Michée 1.8 Ezéchiel 16.37 Esaïe 16.2
12 Maana akaaye Marothi ana utungu wa mema; Kwa kuwa msiba umeshuka toka kwa Bwana, Umefika mpaka lango la Yerusalemu.
Jérémie 14.19 Amos 3.6 Esaïe 59.9-59.11 Esaïe 45.7 Michée 1.9
13 Mfungie gari la vita farasi Aliye mwepesi, ukaaye Lakishi; Alikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni; Maana makosa ya Israeli yameonekana kwako.
2 Rois 18.17 Josué 10.3 2 Chroniques 32.9 Esaïe 37.8 Ezéchiel 23.11
14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi ya kuagia; Nyumba za Akzibu zitakuwa kijito kidanganyacho wafalme wa Israeli.
Josué 15.44 2 Rois 16.8 2 Chroniques 16.1-16.3 Psaumes 62.9 Psaumes 146.3-146.4
15 Bado, ukaaye Maresha, nitakuletea yeye atakayekumiliki; Utukufu wa Israeli utafika mpaka Adulamu.
1 Samuel 22.1 Josué 15.44 Josué 15.35 Josué 12.15 Esaïe 10.5-10.6
16 Jifanyie upaa, jikate nywele zako, Kwa ajili ya watoto waliokufurahisha; Panua upaa wako kama tai; Kwa maana wamekwenda mbali nawe utumwani.
Esaïe 22.12 Job 1.20 2 Rois 17.6 Jérémie 7.29 Lamentations 4.5-4.8

Cette Bible est dans le domaine public.