Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Amos 7.8
Bible en Swahili de l’est


Visions de l’avenir

Visions des sauterelles, du feu et du niveau

1 Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, aliumba nzige mwanzo wa kuchipuka kwake mimea wakati wa vuli; na tazama, ilikuwa mimea ya wakati wa vuli baada ya mavuno ya mfalme.
Joël 1.4 Amos 8.1 Amos 4.9 Joël 2.25 Nahum 3.15-3.17
2 Ikawa, nzige walipokwisha kula majani ya nchi, ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, samehe, nakusihi; Yakobo atasimamaje? Kwa maana ni mdogo.
Esaïe 37.4 Exode 10.15 Ezéchiel 11.13 Jérémie 42.2 Jérémie 14.20-14.21
3 Bwana akaghairi katika jambo hili. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana.
Deutéronome 32.36 Osée 11.8 Jonas 3.10 Joël 2.14 Jacques 5.16
4 Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, Bwana MUNGU aliita ili kushindana kwa moto; nao ukavila vilindi vikuu, ukataka kuiteketeza nchi kavu.
Amos 7.1 Esaïe 66.15-66.16 Exode 9.23-9.24 Jérémie 4.4 Amos 4.11
5 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, acha, nakusihi; Yakobo atasimamaje? Kwa maana ni mdogo.
Psaumes 85.4 Esaïe 10.25 Joël 2.17 Esaïe 1.9 Jérémie 30.19
6 Bwana akaghairi katika jambo hili pia. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.
Jérémie 26.19 Amos 7.3 Jonas 3.10 Psaumes 90.13 Jonas 4.2
7 Haya ndiyo aliyonionyesha; na tazama, Bwana alisimama karibu na ukuta uliojengwa kwa timazi, mwenye timazi mkononi mwake.
2 Rois 21.13 Esaïe 28.17 Apocalypse 11.1 Esaïe 34.11 Apocalypse 21.15
8 Bwana akaniambia, Amosii, unaona nini? Nikasema, Naona timazi. Ndipo Bwana akasema, Tazama, nitaweka timazi kati ya watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe;
Amos 8.2 Ezéchiel 7.2-7.9 Jérémie 15.6 Lamentations 2.8 Esaïe 28.17
9 na mahali palipoinuka pa Isaka patakuwa ukiwa, na mahali patakatifu pa Israeli pataharibika; nami nitaondoka nishindane na nyumba ya Yeroboamu kwa upanga.
2 Rois 15.8-15.10 Genèse 46.1 Lévitique 26.30-26.31 Amos 3.14 Amos 5.5

Amos et le prêtre Amatsia

10 Ndipo Amazia, kuhani wa Betheli, akapeleka habari kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli, akisema, Amosii amefanya fitina juu yako kati ya nyumba ya Israeli; nchi haiwezi kustahimili maneno yake yote.
Jérémie 38.4 Jérémie 26.8-26.11 1 Rois 12.31-12.32 2 Rois 14.23-14.24 1 Rois 13.33
11 Kwa maana Amosii asema hivi, Yeroboamu atakufa kwa upanga, na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali, hali ya kufungwa, atoke katika nchi yake.
2 Rois 17.6 Jérémie 28.10-28.11 Psaumes 56.5 Amos 6.7-6.8 Actes 6.14
12 Tena Amazia akamwambia Amosii, Ewe mwonaji, nenda zako, ikimbilie nchi ya Yuda, ukale mkate huko, ukatabiri huko;
Matthieu 8.34 1 Samuel 9.9 Amos 2.12 Esaïe 30.10 Romains 16.18
13 lakini usitabiri tena huku Betheli; kwa maana ni mahali patakatifu pa mfalme, nayo ni nyumba ya kifalme.
1 Rois 12.32 Amos 2.12 1 Rois 12.29 1 Rois 13.1 Actes 5.40
14 Ndipo Amosii akajibu akamwambia Amazia, Mimi sikuwa nabii, wala sikuwa mwana wa nabii; bali nalikuwa mchungaji, na mtunza mikuyu;
Amos 1.1 2 Rois 2.5 2 Rois 4.38 2 Rois 2.3 Zacharie 13.5
15 naye Bwana akanitwaa, katika kufuatana na kundi; Bwana akaniambia, Enenda uwatabirie watu wangu Israeli.
2 Samuel 7.8 Ezéchiel 2.3-2.4 Jérémie 1.7 Actes 5.29-5.32 Actes 5.20
16 Basi, sasa lisikie neno la Bwana; Wewe unasema, Usitabiri juu ya Israeli, wala usitoe neno lako juu ya nyumba ya Isaka;
Ezéchiel 20.46 Michée 2.6 Ezéchiel 21.2 Amos 7.13 Deutéronome 32.2
17 kwa hiyo, Bwana asema hivi, Mke wako atakuwa kahaba mjini, na wana wako na binti zako wataanguka kwa upanga, na shamba lako litagawanywa kwa kamba; na wewe mwenyewe utakufa katika nchi iliyo najisi; na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali hali ya kufungwa kutoka nchi yake.
Osée 9.3 2 Rois 17.6 Ezéchiel 4.13 Jérémie 28.16 Osée 4.13-4.14

Cette Bible est dans le domaine public.