Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Amos 7.13
Bible en Swahili de l’est


Visions de l’avenir

Visions des sauterelles, du feu et du niveau

1 Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, aliumba nzige mwanzo wa kuchipuka kwake mimea wakati wa vuli; na tazama, ilikuwa mimea ya wakati wa vuli baada ya mavuno ya mfalme.
Joël 1.4 Amos 8.1 Amos 4.9 Esaïe 33.4 Zacharie 1.20
2 Ikawa, nzige walipokwisha kula majani ya nchi, ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, samehe, nakusihi; Yakobo atasimamaje? Kwa maana ni mdogo.
Ezéchiel 11.13 Esaïe 37.4 Exode 10.15 Jérémie 14.20-14.21 Jérémie 14.7
3 Bwana akaghairi katika jambo hili. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana.
Deutéronome 32.36 Jonas 3.10 Osée 11.8 Joël 2.14 Jérémie 26.19
4 Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, Bwana MUNGU aliita ili kushindana kwa moto; nao ukavila vilindi vikuu, ukataka kuiteketeza nchi kavu.
Amos 7.1 Esaïe 66.15-66.16 Hébreux 1.7 Lévitique 10.2 Amos 5.6
5 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, acha, nakusihi; Yakobo atasimamaje? Kwa maana ni mdogo.
Psaumes 85.4 Esaïe 1.9 Jérémie 30.19 Amos 7.2-7.3 Esaïe 10.25
6 Bwana akaghairi katika jambo hili pia. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.
Psaumes 90.13 Jonas 4.2 Juges 2.18 Juges 10.16 Psaumes 135.14
7 Haya ndiyo aliyonionyesha; na tazama, Bwana alisimama karibu na ukuta uliojengwa kwa timazi, mwenye timazi mkononi mwake.
2 Rois 21.13 Apocalypse 21.15 Ezéchiel 40.3 2 Samuel 8.2 Zacharie 2.1-2.2
8 Bwana akaniambia, Amosii, unaona nini? Nikasema, Naona timazi. Ndipo Bwana akasema, Tazama, nitaweka timazi kati ya watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe;
Amos 8.2 Jérémie 15.6 Lamentations 2.8 Ezéchiel 7.2-7.9 Esaïe 28.17
9 na mahali palipoinuka pa Isaka patakuwa ukiwa, na mahali patakatifu pa Israeli pataharibika; nami nitaondoka nishindane na nyumba ya Yeroboamu kwa upanga.
2 Rois 15.8-15.10 Genèse 46.1 Amos 8.14 Esaïe 63.18 Genèse 26.23-26.25

Amos et le prêtre Amatsia

10 Ndipo Amazia, kuhani wa Betheli, akapeleka habari kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli, akisema, Amosii amefanya fitina juu yako kati ya nyumba ya Israeli; nchi haiwezi kustahimili maneno yake yote.
Jérémie 38.4 2 Rois 14.23-14.24 Jérémie 26.8-26.11 1 Rois 12.31-12.32 1 Rois 13.33
11 Kwa maana Amosii asema hivi, Yeroboamu atakufa kwa upanga, na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali, hali ya kufungwa, atoke katika nchi yake.
2 Rois 17.6 Actes 6.14 Jérémie 26.9 Amos 7.9 Jérémie 28.10-28.11
12 Tena Amazia akamwambia Amosii, Ewe mwonaji, nenda zako, ikimbilie nchi ya Yuda, ukale mkate huko, ukatabiri huko;
Matthieu 8.34 1 Samuel 9.9 1 Corinthiens 2.14 2 Chroniques 16.10 Luc 13.31
13 lakini usitabiri tena huku Betheli; kwa maana ni mahali patakatifu pa mfalme, nayo ni nyumba ya kifalme.
1 Rois 12.32 Amos 2.12 1 Rois 12.29 1 Rois 13.1 Actes 4.17-4.18
14 Ndipo Amosii akajibu akamwambia Amazia, Mimi sikuwa nabii, wala sikuwa mwana wa nabii; bali nalikuwa mchungaji, na mtunza mikuyu;
Amos 1.1 2 Rois 4.38 2 Rois 2.5 Zacharie 13.5 1 Rois 20.35
15 naye Bwana akanitwaa, katika kufuatana na kundi; Bwana akaniambia, Enenda uwatabirie watu wangu Israeli.
Ezéchiel 2.3-2.4 2 Samuel 7.8 Jérémie 1.7 Luc 24.46-24.48 Matthieu 4.18-4.19
16 Basi, sasa lisikie neno la Bwana; Wewe unasema, Usitabiri juu ya Israeli, wala usitoe neno lako juu ya nyumba ya Isaka;
Ezéchiel 20.46 Ezéchiel 21.2 Michée 2.6 Amos 7.13 Deutéronome 32.2
17 kwa hiyo, Bwana asema hivi, Mke wako atakuwa kahaba mjini, na wana wako na binti zako wataanguka kwa upanga, na shamba lako litagawanywa kwa kamba; na wewe mwenyewe utakufa katika nchi iliyo najisi; na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali hali ya kufungwa kutoka nchi yake.
2 Rois 17.6 Osée 9.3 Osée 4.13-4.14 Ezéchiel 4.13 Jérémie 28.16

Cette Bible est dans le domaine public.