Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 6.26
Bible en Swahili de l’est


1 Ilimpendeza Dario kuweka juu ya ufalme maliwali mia na ishirini, wawe juu ya ufalme wote;
Daniel 5.31 Esther 1.1 Exode 18.21-18.22 1 Pierre 2.14

Daniel dans la fosse aux lions

2 na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danielii alikuwa mmoja wao; ili maliwali hawa watoe hesabu kwao, mfalme asipate hasara.
Daniel 5.16 Daniel 2.48-2.49 Daniel 5.29 Esdras 4.22 Esther 7.4
3 Basi Danielii huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote.
Daniel 5.12 Daniel 5.14 Esther 10.3 Néhémie 7.2 Genèse 41.38-41.41
4 Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danielii kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake.
1 Pierre 2.12 1 Pierre 3.16 Philippiens 2.15 Ecclésiaste 4.4 Luc 23.14-23.15
5 Ndipo wale watu wakasema, Hatutapata sababu ya kumshitaki Danielii huyo, tusipoipata katika mambo ya sheria ya Mungu wake.
Actes 24.13-24.16 Actes 24.20-24.21 1 Samuel 24.17 Esther 3.8 Jean 19.6-19.7
6 Basi wale mawaziri na maamiri wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia hivi, Mfalme Dario, uishi milele.
Daniel 2.4 Daniel 6.21 Néhémie 2.3 Daniel 5.10 Daniel 3.9
7 Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba.
Daniel 3.2 Psaumes 59.3 Daniel 3.6 Psaumes 10.9 Psaumes 83.1-83.3
8 Sasa, Ee mfalme, piga marufuku, ukatie sahihi maandiko haya, yasibadilike, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi, isiyoweza kubadilika.
Esther 1.19 Daniel 6.15 Daniel 6.12 Esther 8.10 Esaïe 10.1
9 Basi mfalme Dario akayatia sahihi maandiko yale, na ile marufuku.
Psaumes 118.9 Psaumes 146.3 Psaumes 62.9-62.10 Proverbes 6.2 Esaïe 2.22
10 Hata Danielii, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.
Psaumes 55.17 Psaumes 95.6 Actes 5.29 Psaumes 5.7 Philippiens 4.6
11 Basi watu hao wakakusanyika pamoja, wakamwona Danielii akiomba dua, na kusihi mbele za Mungu wake.
Psaumes 37.32-37.33 Daniel 6.6 Psaumes 10.9
12 Ndipo wakakaribia, wakasema mbele ya mfalme katika habari ya ile marufuku ya mfalme; Je! Hukuitia sahihi ile marufuku, ya kwamba kila mtu atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme, atatupwa katika tundu la simba? Mfalme akajibu, akasema, Neno hili ni kweli, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi isiyoweza kubadilika.
Daniel 6.8 Daniel 3.8-3.12 Esther 1.19 Actes 16.19 Actes 16.24
13 Basi wakajibu, wakasema mbele ya mfalme, Yule Danielii, aliye mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda, hakujali wewe, Ee mfalme, wala ile marufuku uliyoitia sahihi, bali aomba dua mara tatu kila siku.
Daniel 3.12 Daniel 2.25 Daniel 5.13 Esther 3.8 Actes 5.29
14 Basi mfalme aliposikia maneno haya alikasirika sana, akakaza moyo wake ili kumponya Danielii; akajitaabisha kumwokoa hata jua likachwa.
Marc 6.26 2 Samuel 3.28-3.29 Jean 19.7-19.12 Luc 23.13-23.21 Daniel 3.13
15 Ndipo watu wale wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia mfalme, Ee mfalme, ujue ya kuwa ni sheria ya Wamedi na Waajemi, lisibadilike neno lo lote lililo marufuku, wala amri yo yote iliyowekwa na mfalme.
Esther 8.8 Daniel 6.12 Daniel 6.8 Psaumes 94.20-94.21
16 Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danielii, wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akanena, akamwambia Danielii, Mungu wako unayemtumikia daima, yeye atakuponya.
Psaumes 37.39-37.40 Job 5.19 Daniel 3.28 Esaïe 43.2 Daniel 3.17
17 Likaletwa jiwe, likawekwa mdomoni mwa lile tundu; naye mfalme akalitia muhuri kwa muhuri yake mwenyewe, na kwa muhuri ya wakuu wake, lisibadilike neno lo lote katika habari za Danielii.
Lamentations 3.53 Matthieu 27.60-27.66 Actes 12.4 Actes 16.23-16.24
18 Kisha mfalme akaenda nyumbani kwake, akakesha usiku kucha, akafunga; na vinanda havikuletwa mbele yake; na usingizi wake ukampaa.
Esther 6.1 Daniel 2.1 2 Samuel 12.16-12.17 Psaumes 77.4 Apocalypse 18.22
19 Asubuhi mfalme akaondoka mapema, akaenda kwa haraka mpaka penye lile tundu la simba.
2 Corinthiens 2.13 Matthieu 28.1 1 Thessaloniciens 3.5 Marc 16.2
20 Naye alipolikaribia lile tundu, akamlilia Danielii kwa sauti ya huzuni; mfalme akanena; akamwambia Danielii, Ee Danielii, mtumishi wa Mungu aliye hai, je! Mungu wako, unayemtumikia daima, aweza kukuponya na simba hawa?
Daniel 3.17 Hébreux 7.25 Daniel 6.27 1 Chroniques 16.11 Daniel 6.16
21 Ndipo Danielii akamwambia mfalme, Ee mfalme, uishi milele.
Daniel 2.4 Daniel 6.6 Néhémie 2.3
22 Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi nalionekana kuwa sina hatia; tena, mbele yako, Ee mfalme, sikukosa neno.
Hébreux 11.33 2 Timothée 4.17 Daniel 3.28 Psaumes 91.11-91.13 Actes 12.11
23 Basi mfalme akafurahi sana, akaamuru wamtoe Danielii katika lile tundu. Ndipo Danielii akatolewa katika lile tundu, wala dhara lo lote halikuonekana mwilini mwake, kwa sababu alikuwa anamtumaini Mungu wake.
Daniel 3.25 1 Chroniques 5.20 Esaïe 26.3 Daniel 3.27-3.28 2 Chroniques 20.20
24 Mfalme akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomshitaki Danielii, wakawatupa katika tundu la simba, wao, na watoto wao, na wake zao; na wale simba wakawashinda wakaivunja mifupa yao vipande vipande, kabla hawajafika chini ya tundu.
2 Rois 14.6 Esther 7.10 Esaïe 38.13 Deutéronome 24.16 Esther 9.10
25 Ndipo mfalme Dario akawaandikia watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, waliokaa juu ya uso wa dunia; Amani na iongezeke kwenu.
Daniel 4.1 Esdras 1.1-1.2 Esdras 4.17 Esther 8.9 1 Pierre 1.2
26 Mimi naweka amri, ya kwamba katika mamlaka yote ya ufalme wangu watu watetemeke na kuogopa mbele za Mungu wa Danielii; maana yeye ndiye Mungu aliye hai, adumuye milele, na ufalme wake ni ufalme usioharibika, na mamlaka yake itadumu hata mwisho.
Daniel 4.34 Daniel 3.29 Daniel 4.3 Daniel 2.44 Daniel 7.14
27 Yeye huponya na kuokoa, hutenda ishara na maajabu mbinguni na duniani, ndiye aliyemponya Danielii na nguvu za simba.
Daniel 4.2-4.3 Psaumes 18.48 Psaumes 35.17 Jérémie 32.19-32.20 Marc 16.17-16.18
28 Basi Danielii huyo akafanikiwa katika enzi ya Dario, na katika enzi ya Koreshi, Mwajemi.
Daniel 1.21 Esaïe 44.28-45.1 2 Chroniques 36.22-1.2 Daniel 10.1

Cette Bible est dans le domaine public.