Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 5.6
Bible en Swahili de l’est


Jugement et dispersion d’Israël

1 Nawe, mwanadamu, ujipatie upanga mkali, kama wembe wa kinyozi ujipatie, ukaupitishe juu ya kichwa chako na ndevu zako; kisha ujipatie mizani ya kupimia, ukazigawanye nywele hizo.
Lévitique 21.5 Esaïe 7.20 Ezéchiel 44.20 Daniel 5.27
2 Theluthi ya hizo utaiteketeza katikati ya mji, siku za mazingiwa zitakapotimia; nawe utatwaa theluthi, na kuipiga kwa upanga pande zote; nawe utatawanya theluthi ichukuliwe na upepo, nami nitafuta upanga nyuma yake.
Ezéchiel 5.12 Lévitique 26.33 Ezéchiel 12.14 Jérémie 9.16 Ezéchiel 4.1-4.8
3 Nawe twaa nywele chache katika hizo, na kuzifunga katika upindo wa mavazi yako.
Jérémie 52.16 Jérémie 40.6 Jérémie 39.10 2 Rois 25.12 1 Pierre 4.18
4 Nawe utatwaa tena baadhi ya hizo, na kuzitupa katikati ya moto, na kuziteketeza katika moto huo; kutoka nywele hizo moto utakuja na kuingia katika nyumba yote ya Israeli.
Jérémie 52.30 Jérémie 4.4 Jérémie 41.1-41.18 Jérémie 48.45 2 Rois 25.25
5 Bwana MUNGU asema hivi; Huu ndio Yerusalemu; nimeuweka kati ya mataifa, na nchi zauzunguka pande zote.
Ezéchiel 4.1 Deutéronome 4.6 Ezéchiel 16.14 Jérémie 6.6 Matthieu 5.14
6 Nao umeasi hukumu zangu, kwa kutenda mabaya kuliko mataifa hayo, nao umeasi sheria kuliko nchi hizo ziuzungukazo; maana wamezikataa hukumu zangu, wala hawakuenda katika sheria zangu.
Jérémie 11.10 Néhémie 9.16-9.17 Ezéchiel 16.47-16.48 Zacharie 7.11 2 Rois 17.8-17.20
7 Basi, kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu ninyi mmefanya ghasia kuliko mataifa wawazungukao ninyi, wala hamkuenda katika sheria zangu, wala hamkuzishika hukumu zangu, wala hamkutenda kama kawaida za mataifa wawazungukao;
Jérémie 2.10-2.11 2 Chroniques 33.9 2 Rois 21.9-21.11 Ezéchiel 16.54 Ezéchiel 16.47-16.48
8 basi, Bwana MUNGU asema hivi; Angalia, mimi, naam, mimi, ni juu yako; nami nitafanya hukumu kati yako machoni pa mataifa.
Ezéchiel 15.7 Jérémie 24.9 Jérémie 21.13 Jérémie 21.5 Ezéchiel 21.3
9 Nami nitakutenda nisiyoyatenda zamani, wala sitafanya tena mambo kama hayo, kwa sababu ya machukizo yako yote.
Daniel 9.12 Matthieu 24.21 Amos 3.2 Lamentations 4.9 Lamentations 4.6
10 Kwa sababu hiyo baba za watu watawala wana wao kati yako, nao wana watawala baba zao; nami nitafanya hukumu ndani yako, na hao wote waliosalia kwako nitawatawanya kwa pepo zote.
Ezéchiel 12.14 Zacharie 2.6 Deutéronome 28.64 Ezéchiel 36.19 Ezéchiel 5.2
11 Kwa sababu hiyo, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hakika kwa kuwa umepatia unajisi patakatifu pangu, kwa matendo yako yote niyachukiayo, na kwa machukizo yako yote, kwa sababu hiyo mimi nami nitakupunguza; wala jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma.
Ezéchiel 7.20 Ezéchiel 7.9 Ezéchiel 8.5-8.6 Ezéchiel 7.4 Ezéchiel 11.18
12 Theluthi yenu mtakufa kwa tauni, na kwa njaa watakomeshwa ndani yako; na theluthi yenu wataanguka kwa upanga pande zako zote; na theluthi yenu nitawatawanya kwa pepo zote, kisha nitafuta upanga nyuma yao.
Ezéchiel 5.2 Jérémie 15.2 Jérémie 21.9 Ezéchiel 12.14 Ezéchiel 6.11-6.12
13 Hivyo ndivyo ghadhabu yangu itakavyotimia, nami nitatosheleza hasira yangu juu yao, nami nitafarijika; nao watajua ya kuwa mimi, Bwana, nimenena kwa wivu wangu, nitakapokuwa nimeitimiza ghadhabu yangu juu yao.
Ezéchiel 36.5-36.6 Esaïe 1.24 Lamentations 4.11 Ezéchiel 20.21 Ezéchiel 21.17
14 Tena nitakufanya kuwa ukiwa, na aibu, kati ya mataifa wakuzungukao, machoni pa watu wote wapitao.
Ezéchiel 22.4 Psaumes 79.1-79.4 Psaumes 74.3-74.10 Néhémie 2.17 Michée 3.12
15 Nayo itakuwa tukano na aibu, na mafundisho na ajabu, kwa mataifa wakuzungukao, hapo nitakapotekeleza hukumu ndani yako, kwa hasira, na kwa ghadhabu, na kwa malaumu ya ghadhabu; mimi, Bwana, nimeyanena hayo;
Ezéchiel 25.17 Jérémie 22.8-22.9 Esaïe 26.9 1 Rois 9.7 Esaïe 66.15-66.16
16 hapo nitakapopeleka mishale mibaya ya njaa juu yao, iletayo uharibifu, nitakayoipeleka ili kuwaharibu ninyi; nami nitaiongeza njaa juu yenu, na tegemeo lenu la mkate nitalivunja.
Deutéronome 32.23-32.24 Ezéchiel 4.16 Psaumes 7.13 Lévitique 26.26 2 Rois 6.25
17 Nami nitapeleka juu yenu njaa na wanyama wabaya, nao watakunyang’anya watu wako; na tauni na damu zitapita ndani yako; nami nitauleta upanga juu yako; mimi Bwana, nimeyanena hayo.
Ezéchiel 38.22 Ezéchiel 33.27 Lévitique 26.22 Deutéronome 32.24 Ezéchiel 14.21

Cette Bible est dans le domaine public.