Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 47
Bible en Swahili de l’est


Le torrent jaillissant du sanctuaire

1 Baadaye akanileta tena mpaka lango la nyumba; na tazama, maji yalitoka chini ya kizingiti cha nyumba, kwa njia ya mashariki, maana upande wa mbele wa nyumba ulielekea upande wa mashariki; nayo maji yakashuka toka chini ya upande wa kuume wa nyumba, upande wa kusini wa madhabahu.
Psaumes 46.4 Joël 3.18 Esaïe 55.1 Zacharie 14.8 Jérémie 2.13
2 Ndipo akanileta nje kwa njia ya lango upande wa kaskazini, akanizungusha kwa njia ya nje mpaka lango la nje, kwa njia yake iliyoelekea mashariki; na tazama, maji yalitoka upande wa kuume.
Ezéchiel 44.2 Ezéchiel 44.4
3 Na alipotoka mtu yule, mwenye uzi wa kupimia mkononi mwake, kwenda masharikini, akapima dhiraa elfu, akanivusha maji yale; maji yakafika mpaka viweko vya miguu.
Ezéchiel 40.3 Zacharie 2.1 Actes 2.33 Luc 24.49 Apocalypse 21.15
4 Kisha akapima dhiraa elfu, akanivusha maji yale, maji yakafika mpaka magoti. Kisha akapima dhiraa elfu, akanivusha, maji yakafika mpaka viuno.
Colossiens 1.6 Romains 15.19 Actes 19.10-19.20
5 Kisha akapima dhiraa elfu, yakawa mto nisioweza kuuvuka; maana maji yamezidi, maji ya kuogelea, mto usiovukika.
Esaïe 11.9 Habakuk 2.14 Apocalypse 11.15 Apocalypse 20.2-20.4 Daniel 2.34-2.35
6 Akaniambia, Mwanadamu, je! Umeona haya? Kisha akanichukua akanirudisha mpaka ukingo wa mto.
Ezéchiel 44.5 Ezéchiel 40.4 Ezéchiel 8.17 Jérémie 1.11-1.13 Zacharie 4.2
7 Basi nikiisha kurudi, tazama, kando ya ukingo wa mto ilikuwapo miti mingi sana, upande huu na upande huu.
Ezéchiel 47.12 Apocalypse 22.2 1 Rois 9.26 2 Rois 2.13 Genèse 2.9-2.10
8 Ndipo akaniambia, Maji haya yanatoka kwenda pande za nchi ya mashariki, nayo yanashuka mpaka Araba, na kuingia katika bahari maji yatokezwayo yataingia baharini, na maji yake yataponyeka.
Deutéronome 3.17 Josué 3.16 2 Rois 2.19-2.22 Esaïe 41.17-41.19 Esaïe 44.3-44.5
9 Tena itakuwa, kila kiumbe hai kisongamanacho, kila mahali itakapofika mito hiyo, kitaishi; kutakuwapo wingi mkubwa wa samaki, kwa sababu maji haya yamefika huko maana maji yale yataponyeka, na kila kitu kitaishi po pote utakapofikilia mto huo.
Jean 5.25 Jean 11.25-11.26 Esaïe 60.3-60.10 Zacharie 2.11 Esaïe 55.1
10 Tena itakuwa, wavuvi watasimama karibu nao; toka Engedi mpaka En-eglaimu, patakuwa ni mahali pa kutandazia nyavu; samaki wao watakuwa namna zao mbalimbali, kama samaki wa bahari kubwa, wengi sana.
Psaumes 104.25 Matthieu 4.19 Nombres 34.6 2 Chroniques 20.2 Ezéchiel 48.28
11 Bali mahali penye matope, na maziwa yake, hayataponywa; yataachwa yawe ya chumvi.
Deutéronome 29.23 Apocalypse 22.11 Jérémie 17.6 Hébreux 10.26-10.31 Marc 9.48-9.49
12 Na karibu na mto, juu ya ukingo wake, upande huu na upande huu, utamea kila mti wa chakula, ambao majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayatatindika kamwe; utatoa matunda mapya kila mwezi, kwa sababu maji yake yanatoka mahali patakatifu; na matunda yake yatakuwa ni chakula; na majani yake yatakuwa ni dawa.
Apocalypse 22.2 Ezéchiel 47.7 Psaumes 1.3 Jérémie 17.8 Genèse 2.9

Limites du pays

13 Bwana MUNGU asema hivi; Huu ndio mpaka ambao mtaigawanya nchi iwe urithi sawasawa na kabila kumi na mbili za Israeli; kwa Yusufu, mafungu mawili.
Genèse 48.5 Ezéchiel 48.4-48.6 Nombres 34.2-34.12 Jérémie 3.18 1 Chroniques 5.1
14 Nanyi mtaimiliki, mtu huyu sawasawa na huyu; ambayo naliuinua mkono wangu kuwapa baba zenu; na nchi hii itawaangukia kuwa urithi.
Genèse 12.7 Ezéchiel 20.5-20.6 Ezéchiel 48.29 Ezéchiel 20.28 Genèse 26.3
15 Na huu ndio mpaka wa nchi; upande wa kaskazini, toka bahari kubwa, kwa njia ya Hethloni, mpaka maingilio ya Sedada;
Nombres 34.8 Ezéchiel 48.1
16 Hamathi, na Berotha, na Sibraimu, ulio katikati ya mpaka wa Dameski na mpaka wa Hamathi; na Haser-hatikoni, ulio karibu na mpaka wa Haurani.
2 Samuel 8.8 Nombres 13.21 Ezéchiel 48.1 Genèse 14.15 Zacharie 9.2
17 Nao mpaka toka baharini utakuwa Hasar-enoni, penye mpaka wa Dameski, na kaskazini kuelekea upande wa kaskazini ndio mpaka wa Hamathi. Huu ndio upande wa kaskazini.
Ezéchiel 48.1 Nombres 34.9
18 Na upande wa mashariki, kati ya Haurani na Dameski, na Gileadi na nchi ya sraeli, utakuwa mto Yordani; mtapima toka mpaka wa upande wa kaskazini hata bahari ya mashariki. Huu ndio upande wa mashariki.
Genèse 13.10 Genèse 31.23 Juges 10.8 Job 40.23 Genèse 31.47
19 Na upande wa kusini, kuelekea kusini, utakuwa ni kutoka Tamari mpaka maji ya Meriba-Kadeshi, mpaka kijito cha Misri, mpaka bahari kubwa. Huu ndio upande wa kusini, kuelekea kusini.
Deutéronome 32.51 Ezéchiel 48.28 Nombres 34.5 Nombres 20.13 Deutéronome 33.8
20 Na upande wa magharibi, utakuwa ni bahari kubwa, kutoka mpaka wa kusini mpaka mahali penye kuelekea maingilio ya Hamathi. Huu ndio upande wa magharibi.
Nombres 34.6 Ezéchiel 48.1
21 Basi ndivyo mtakavyojigawanyia nafsi zenu nchi hii, sawasawa na kabila za sraeli.
22 Tena itakuwa mtaigawanya kwa kura, kuwa urithi kwenu, na kwa wageni wakaao kwenu hali ya ugeni, watakaozaa watoto kati yenu, nao watakuwa kwenu, kama wazaliwa miongoni mwa wana Israeli; watakuwa na urithi pamoja nanyi kati ya kabila za Israeli.
Ephésiens 3.6 Colossiens 3.11 Romains 10.12 Esaïe 56.6-56.7 Actes 11.18
23 Tena itakuwa, mgeni akaaye katika kabila iwayo yote, atapewa urithi katika kabila asema Bwana MUNGU.

Cette Bible est dans le domaine public.