Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 24.20
Bible en Swahili de l’est


Signes de la ruine de Jérusalem

1 Tena, katika mwaka wa kenda, mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,
Ezéchiel 20.1 Ezéchiel 8.1 Ezéchiel 33.21 Ezéchiel 26.1 2 Rois 24.12
2 Mwanadamu, liandike jina la siku hii, naam, la siku ii hii; mfalme wa Babeli ameukaribia Yerusalemu siku iyo hiyo.
Jérémie 39.1 Jérémie 52.4 2 Rois 25.1 Esaïe 30.8-30.9 Habakuk 2.2-2.3
3 Ukawatungie mithali nyumba ya kuasi, ukawaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Teleka sufuria, liteleke; ukatie maji ndani yake;
Ezéchiel 20.49 Ezéchiel 17.2 Ezéchiel 11.3 Esaïe 1.2 Ezéchiel 2.3
4 vikusanye vipande vyake ndani yake, naam, kila kipande chema, paja na bega; lijaze mifupa iliyochaguliwa.
Michée 3.2-3.3 Matthieu 7.2 Ezéchiel 22.18-22.22
5 Uwatwae wateule wa kundi la kondoo, ukafanye chungu ya mifupa chini yake; ukalitokose sana; naam, mifupa yake itokoswe ndani yake.
Jérémie 52.10 Jérémie 52.24-52.27 Jérémie 39.6 Ezéchiel 20.47 Apocalypse 19.20
6 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Ole wake mji wa damu! Hilo sufuria ambalo kutu yake i ndani yake, ambalo kutu yake haikulitoka; litoe kipande kipande; hapana kura iliyoanguka juu yake.
Ezéchiel 22.2 Nahum 3.1 2 Rois 24.4 Nahum 3.10 Ezéchiel 22.27
7 Maana damu yake imo ndani yake; aliiweka juu ya jabali lililo wazi; hakuimwaga juu ya nchi, apate kuifunika kwa mavumbi;
Lévitique 17.13 Deutéronome 12.16 Deutéronome 12.24 Jérémie 2.34 1 Rois 21.19
8 ili ipandishe ghadhabu ya kulipa kisasi, nimeiweka damu yake juu ya jabali lililo wazi, isipate kufunikwa.
Deutéronome 32.21-32.22 Apocalypse 17.1-17.6 Ezéchiel 8.17-8.18 Matthieu 7.2 Apocalypse 18.16
9 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Ole wake mji wa damu! Mimi nami nitaiongeza chungu.
Ezéchiel 24.6 Habakuk 2.12 Esaïe 30.33 2 Pierre 3.7-3.12 Luc 13.34-13.35
10 Tia kuni nyingi, uchochee moto, itokose nyama sana, fanyiza mchuzi mzito, mifupa ikateketee.
Lamentations 1.10 Lamentations 2.16 Jérémie 20.5 Jérémie 17.3
11 Kisha litie juu ya makaa yake, tupu, lipate moto, na shaba yake iteketee, uchafu wake uyeyushwe, na kutu yake iteketee.
Jérémie 21.10 Malachie 4.1 Ezéchiel 36.25 Zacharie 13.8-13.9 Esaïe 1.25
12 Amejidhoofisha kwa taabu, lakini kutu yake nyingi haikumtoka; kutu yake haitoki kwa moto.
Jérémie 9.5 Genèse 8.21 Jérémie 2.13 Genèse 6.5-6.7 Ezéchiel 24.6
13 Katika uchafu wako mna uasherati, kwa maana nimekusafisha, ila wewe hukusafika; hutasafishwa tena uchafu wako ukutoke, hata nitakapokuwa nimeituliza hasira yangu kwako.
Jérémie 6.28-6.30 Ezéchiel 5.13 Ezéchiel 22.24 Ezéchiel 8.18 Ezéchiel 16.42
14 Mimi, Bwana, nimenena neno hili, nalo litakuwa; nami nitalifanya; sitaachilia, wala sitahurumia, wala sitajuta; sawasawa na njia zako, na sawasawa na matendo yako, ndivyo watakavyokuhukumu, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 18.30 Ezéchiel 9.10 Psaumes 33.9 Nombres 23.19 Ezéchiel 5.11
15 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
16 Mwanadamu, tazama, ninakuondolea kwa pigo moja tunu, mteule wa macho yako; walakini hutaomboleza wala kulia, wala yasichuruzike machozi yako.
Jérémie 13.17 Jérémie 22.10 Ezéchiel 24.18 Cantique 7.10 Proverbes 5.19
17 Ugua lakini si kwa sauti ya kusikiwa; usifanye matanga kwa ajili yake yeye aliyekufa; jipige kilemba chako, ukavae viatu vyako, wala usiifunike midomo yako, wala usile chakula cha watu.
Osée 9.4 Lévitique 21.10 Lévitique 10.6 2 Samuel 15.30 Ezéchiel 24.22-24.23
18 Basi nalisema na watu asubuhi, na jioni mke wangu akafa; nami nalifanya asubuhi kama nilivyoagizwa.
1 Corinthiens 7.29-7.30
19 Watu hao wakaniambia, Je! Hutaki kutuambia maana ya mambo haya kwetu, hata umefanya kama vile ufanyavyo.
Ezéchiel 12.9 Ezéchiel 37.18 Malachie 3.7-3.8 Malachie 3.13 Ezéchiel 17.12
20 Nikawaambia, Neno la Bwana lilinijia, kusema,
21 Uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Angalieni, nitapatia unajisi patakatifu pangu, fahari ya uwezo wenu, mahali pa kutamaniwa na macho yenu, ambapo roho zenu zinapahurumia na wana wenu na binti zenu, mliowaacha nyuma, wataanguka kwa upanga.
Ezéchiel 23.47 Jérémie 7.14 Psaumes 27.4 Ezéchiel 23.25 Jérémie 16.3-16.4
22 Nanyi mtafanya kama mimi nilivyofanya; hamtaifunika midomo yenu, wala kula chakula cha watu.
Amos 6.9-6.10 Job 27.15 Psaumes 78.64 Jérémie 16.4-16.7 Ezéchiel 24.16-24.17
23 Na vilemba vyenu vitakuwa juu ya vichwa vyenu, na viatu vyenu miguuni mwenu; hamtaomboleza wala kulia; lakini mtafifia katika maovu yenu, na kuugua kila mtu pamoja na mwenziwe.
Ezéchiel 33.10 Ezéchiel 4.17 Lévitique 26.39 Job 27.15 Psaumes 78.64
24 Basi ndivyo Ezekielii atakavyokuwa ishara kwenu; ninyi mtatenda sawasawa na yote aliyoyatenda yeye; litakapokuja jambo hili, ndipo mtakapojua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.
Ezéchiel 4.3 Ezéchiel 12.11 Esaïe 20.3 Ezéchiel 6.7 Luc 11.29-11.30
25 Nawe, mwanadamu, je! Haitakuwa hivi katika siku hiyo nitakapowaondolea nguvu zao, na furaha ya utukufu wao, na kilichotamaniwa na macho yao, ambacho walikiinulia mioyo yao, wana wao na binti zao,
Ezéchiel 24.21 Psaumes 48.2 Psaumes 50.2 Jérémie 11.22 Deutéronome 28.32
26 kwamba katika siku iyo hiyo yeye atakayeokoka atakuja kwako, akusikize jambo hili kwa masikio yako?
Job 1.15-1.19 Ezéchiel 33.21-33.22 1 Samuel 4.12-4.18
27 Siku hiyo kinywa chako kitafumbuliwa kwake aliyeokoka, nawe utasema; hutakuwa bubu tena; ndivyo utakavyokuwa ishara kwao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 33.22 Ezéchiel 29.21 Ezéchiel 3.26-3.27 Exode 6.11-6.12 Ephésiens 6.19

Cette Bible est dans le domaine public.