Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 39.6
Bible en Swahili de l’est


Chute de Jérusalem

1 Hata ikawa, Yerusalemu ulipotwaliwa, (katika mwaka wa kenda wa Sedekia, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na jeshi lake lote, wakaja juu ya Yerusalemu, wakauhusuru;
Jérémie 52.4-52.7 Ezéchiel 24.1-24.2 Zacharie 8.19 2 Rois 25.1-25.12
2 katika mwaka wa kumi na mmoja wa Sedekia, mwezi wa nne, siku ya kenda ya mwezi, sehemu ya ukuta wa mji ilibomolewa;)
Jérémie 52.6-52.7 Ezéchiel 33.21 2 Rois 25.3-25.4 Jérémie 5.10 Sophonie 1.10
3 wakuu wote wa mfalme wa Babeli wakaingia, wakaketi katika lango la katikati, yaani, Nergal-Shareza, mnyweshaji, Nebu-Sarseki, mkuu wa matowashi, Nergal-Shareza, mkuu wa wanajimu, pamoja na wakuu wengine wote wa mfalme wa Babeli.
Jérémie 21.4 Jérémie 38.17 Jérémie 39.13 Jérémie 1.15 2 Rois 17.30
4 Ikawa Sedekia, mfalme wa Yuda, na watu wote wa vita walipowaona, ndipo wakakimbia, wakatoka mjini usiku, kwa njia ya bustani ya mfalme, kwa lango lililokuwa kati ya zile kuta mbili; naye akatoka kwa njia ya Araba.
Amos 2.14 2 Chroniques 32.5 Jérémie 52.7-52.11 Esaïe 30.15-30.16 Jérémie 38.18-38.20
5 Lakini jeshi la Wakaldayo wakawafuatia, wakampata Sedekia katika nchi tambarare ya Yeriko; nao walipomkamata, wakamleta kwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, huko Ribla katika nchi ya Hamathi, naye akatoa hukumu juu yake.
2 Rois 23.33 Josué 5.10 Jérémie 52.26-52.27 Josué 4.13 Jérémie 52.8-52.9
6 Ndipo mfalme wa Babeli akawaua wana wa Sedekia huko Ribla mbele ya macho yake; pia mfalme wa Babeli akawaua wakuu wote wa Yuda.
Jérémie 52.10 2 Rois 25.7 Jérémie 24.8-24.10 Jérémie 34.19-34.21 Jérémie 21.7
7 Pamoja na hayo akampofusha macho Sedekia, akamfunga kwa pingu ili amchukue mpaka Babeli.
Ezéchiel 12.13 2 Rois 25.7 Jérémie 52.11 Jérémie 32.4-32.5 Juges 16.21
8 Nao Wakaldayo wakaiteketeza nyumba ya mfalme, na nyumba za watu kwa moto, wakazibomoa kuta za Yerusalemu.
Néhémie 1.3 Jérémie 21.10 Jérémie 38.18 Jérémie 52.13-52.14 2 Rois 25.9-25.10
9 Basi, Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawachukua mateka mabaki ya watu waliosalia katika mji mpaka Babeli, na hao pia waliouacha mji na kujiunga naye, na mabaki ya watu waliosalia.
Jérémie 40.1 Genèse 37.36 Jérémie 52.12-52.16 2 Rois 25.20 2 Rois 25.11
10 Lakini Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawaacha baadhi ya maskini wa watu, waliokuwa hawana kitu, katika nchi ya Yuda, akawapa mashamba ya mizabibu na makonde wakati uo huo.
2 Rois 25.12 Jérémie 40.7 Ezéchiel 33.24 Jérémie 52.16

Sort de Jérémie et d’Ebed-Mélec

11 Basi Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akamwagiza Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, katika habari za Yeremia, akisema,
Actes 24.23 Jérémie 15.21 Job 5.19 Jérémie 37.2 Jérémie 15.11
12 Mtwae, umtunze sana, wala usimtende neno baya lo lote; lakini umtendee kama atakavyokuambia.
Proverbes 16.7 Proverbes 21.1 Jérémie 40.4 Psaumes 105.14-105.15 1 Pierre 3.12-3.13
13 Basi Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, na Nebu-Shazbani, mkuu wa matowashi, na Nergal-Shareza, mkuu wa wanajimu, na maakida wakuu wote wa mfalme wa Babeli.
Jérémie 39.3 Jérémie 39.9
14 wakatuma watu wakamwondoa Yeremia katika uwanda wa walinzi, wakamweka katika mikono ya Gedalia, mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, ili ampeleke nyumbani kwake; basi akakaa pamoja na hao watu.
Jérémie 38.28 Jérémie 26.24 2 Rois 25.22-25.25 2 Rois 22.12 Jérémie 40.1-41.3
15 Basi neno la Bwana likamjia Yeremia, wakati ule alipokuwa amefungwa katika uwanda wa walinzi, kusema,
2 Timothée 2.9 Jérémie 32.1-32.2 Jérémie 36.1-36.5 Jérémie 39.14 Jérémie 37.21
16 Haya! Enenda ukaseme na Ebedmeleki, Mkushi, kusema, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitaupatiliza mji huu maneno yangu kwa mabaya, wala si kwa mema; nayo yatatimizwa mbele yako katika siku hiyo.
Daniel 9.12 Zacharie 1.6 Jérémie 34.22 Jérémie 19.11-19.12 Jérémie 32.28-32.29
17 Lakini nitakuokoa wewe katika siku hiyo, asema Bwana; wala hutatiwa katika mikono ya watu wale unaowaogopa.
Psaumes 50.15 Psaumes 41.1-41.2 2 Samuel 24.14 Jérémie 1.19 Job 5.19-5.21
18 Kwa maana ni yakini, nitakuokoa, wala hutaanguka kwa upanga, lakini nafsi yako itakuwa kama nyara kwako; kwa kuwa ulinitumaini mimi, asema Bwana.
Jérémie 21.9 Jérémie 38.2 Psaumes 34.22 Jérémie 17.7-17.8 1 Chroniques 5.20

Cette Bible est dans le domaine public.