Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 15.13
Bible en Swahili de l’est


Un jugement inéluctable

1 Ndipo Bwana akaniambia, Hata wangesimama mbele zangu Musa na Samweli, moyo wangu usingewaelekea watu hawa; watupe, watoke mbele za macho yangu, wakaende zao.
2 Rois 17.20 Ezéchiel 14.14 Psaumes 99.6 Jérémie 23.39 1 Samuel 7.9
2 Kisha itakuwa, hapo watakapokuambia, Tutoke, tuende wapi? Utawaambia, Bwana asema hivi, Walioandikiwa kufa, watakwenda kufa; au kufa kwa upanga, watakufa kwa upanga; au kufa kwa njaa, watakufa kwa njaa, au kutekwa nyara, watakuwa mateka.
Jérémie 43.11 Jérémie 14.12 Ezéchiel 5.12 Zacharie 11.9 Ezéchiel 5.2
3 Nami nitaamrisha juu yao namna nne, asema Bwana; upanga uue, na mbwa wararue, na ndege wa angani, na wanyama wakali wa nchi, wale na kuangamiza.
Lévitique 26.22 Deutéronome 28.26 Lévitique 26.16 Lévitique 26.25 Esaïe 18.6
4 Nami nitawafanya kuwa kitu cha kutisha katika falme zote za duniani, kwa sababu ya Manase, mwana wa Hezekia mfalme wa Yuda, kwa sababu ya mambo aliyoyatenda katika Yerusalemu.
Jérémie 24.9 2 Rois 24.3-24.4 Jérémie 29.18 Deutéronome 28.25 2 Rois 23.26-23.27
5 Maana ni nani atakayekuhurumia, Ee Yerusalemu? Au ni nani atakayekulilia? Au ni nani atakayegeuka upande ili kuuliza habari za hali yako?
Esaïe 51.19 Nahum 3.7 Jérémie 21.7 Psaumes 69.20 Jérémie 13.14
6 Umenikataa mimi, asema Bwana, umerudi nyuma; ndiyo maana nimenyosha mkono wangu juu yako, na kukuangamiza; nimechoka kwa kughairi.
Jérémie 7.24 Sophonie 1.4 Esaïe 1.4 Jérémie 6.11 Osée 13.14
7 Nami nimewapepea kwa kipepeo katika malango ya nchi nimewaondolea watoto wao, nimewaharibu watu wangu; hata hivyo hawakurudi na kuziacha njia zao.
Esaïe 9.13 Jérémie 18.21 Jérémie 8.4-8.5 Esaïe 41.16 Jérémie 5.3
8 Wajane wao wameongezeka kwangu kuliko mchanga wa bahari; nimeleta mwenye kuteka wakati wa adhuhuri juu ya mama wa vijana; nimeleta hamu na maogofyo yampate ghafula.
Esaïe 3.25-4.1 Luc 21.35 Jérémie 6.4-6.5 Jérémie 5.6 Jérémie 4.16
9 Mwanamke aliyezaa watoto saba anazimia; ametoa roho; jua lake limekuchwa, ungali ni wakati wa mchana; ametahayarika na kufedheheka; na mabaki yao nitawatoa kwa upanga mbele ya adui zao, asema Bwana.
1 Samuel 2.5 Esaïe 47.9 Amos 8.9-8.10 Lamentations 1.1 Lamentations 4.10

Souffrance et plainte de Jérémie

10 Ole wangu, mama yangu, kwa kuwa umenizaa mtu wa kuteta, na mtu wa kushindana na dunia yote! Mimi sikukopesha kwa riba, wala watu hawakunikopesha kwa riba; lakini kila mmoja wao hunilaani.
Exode 22.25 Psaumes 15.5 Jérémie 1.18-1.19 Jérémie 20.7-20.8 Jérémie 15.20
11 Bwana akasema, Hakika nitakutia nguvu upate mema; hakika nitamlazimisha adui akusihi wakati wa uovu, na wakati wa taabu.
Proverbes 16.7 Psaumes 106.46 Jérémie 29.11-29.14 Jérémie 21.2 Proverbes 21.1
12 Je! Mtu aweza kuvunja chuma, naam, chuma kitokacho kaskazini, au shaba?
Habakuk 1.5-1.10 Jérémie 1.18-1.19 Jérémie 28.14 Esaïe 45.9 Jérémie 21.4-21.5
13 Mali yako na hazina zako nitazitoa kuwa nyara, bila kulipwa thamani yake; naam, kwa sababu ya dhambi zako zote, hata katika mipaka yako yote.
Psaumes 44.12 Jérémie 17.3 Esaïe 52.3 Jérémie 20.5 Esaïe 52.5
14 Nami nitakulazimisha kuwatumikia adui zako katika nchi usiyoijua; maana moto umewashwa katika hasira yangu, utakaowateketeza ninyi.
Jérémie 16.13 Deutéronome 32.22 Jérémie 17.4 Deutéronome 28.36 Psaumes 21.9
15 Ee Bwana, unajua wewe; unikumbuke, unijilie, ukanilipie kisasi juu yao wanaoniudhi; usiniondoe kwa uvumilivu wako; ujue ya kuwa ni kwa ajili yako nilivyopatikana na mashutumu.
Jérémie 12.3 Psaumes 69.7-69.9 Jérémie 17.16 Jérémie 20.12 Jérémie 20.8
16 Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi.
Apocalypse 10.9-10.10 Ezéchiel 3.1-3.3 Psaumes 119.101-119.103 Job 23.12 Psaumes 119.111
17 Sikuketi katika mkutano wao wanaojifurahisha, wala sikufurahi, naliketi peke yangu kwa sababu ya mkono wako; kwa maana umenijaza ghadhabu.
Lamentations 3.28 Psaumes 1.1 Psaumes 26.4-26.5 Jérémie 6.11 2 Corinthiens 6.17
18 Mbona maumivu yangu ni ya daima, na jeraha yangu haina dawa, inakataa kuponywa? Je! Yamkini wewe utakuwa kwangu kama kijito kidanganyacho, na kama maji yasiyodumu?
Jérémie 30.15 Job 34.6 Michée 1.9 Jérémie 20.7 Jérémie 14.3
19 Kwa sababu hiyo Bwana asema hivi, Ukirudi, ndipo mimi nitakapokurejeza, upate kusimama mbele zangu; nawe ukitoa kilicho cha thamani katika kilicho kibovu, utakuwa kama kinywa changu; nao watakurudia wewe, bali hutawarudia wao.
Zacharie 3.7 Ezéchiel 22.26 Jérémie 15.1 Ezéchiel 44.23 Lévitique 10.10
20 Nami nitakufanya kuwa kama ukuta wa boma la shaba juu ya watu hawa; nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya, asema Bwana.
Jérémie 1.18-1.19 Ezéchiel 3.9 Psaumes 129.1-129.2 Esaïe 41.10 Jérémie 1.8
21 Nami nitakuokoa na mkono wa watu wabaya, nami nitakukomboa katika mkono wao wenye kutisha.
Genèse 48.16 Esaïe 29.5 Psaumes 37.40 Psaumes 27.2 Esaïe 25.3-25.5

Cette Bible est dans le domaine public.