Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 9.13
Bible en Swahili de l’est


1 Lakini yeye aliyekuwa katika dhiki hatakosa changamko. Hapo kwanza aliiingiza nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali katika hali ya kudharauliwa, lakini zamani za mwisho ameifanya kuwa tukufu, karibu na njia ya bahari; ng’ambo ya Yordani, Galilaya ya mataifa.
Matthieu 4.15-4.16 Esaïe 8.22 2 Chroniques 16.4 2 Rois 15.29 1 Rois 15.19-15.20
2 Watu wale waliokwenda katika giza Wameona nuru kuu; Wale waliokaa katika nchi ya uvuli wa mauti, Nuru imewaangaza.
Matthieu 4.16 Ephésiens 5.8 Luc 1.78-1.79 Luc 2.32 Jean 8.12
3 Umeliongeza taifa, umezidisha furaha yao; Wanafurahi mbele zako, Kama furaha ya wakati wa mavuno, Kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.
1 Samuel 30.16 Psaumes 119.162 Esaïe 66.10 Esaïe 65.18 Esaïe 26.15
4 Kwa maana umeivunja nira ya mzigo wake, na gongo la bega lake, na fimbo yake yeye aliyemwonea, kama katika siku ya Midiani.
Esaïe 14.25 Esaïe 10.26-10.27 Nahum 1.13 Esaïe 54.14 Juges 7.22-7.25
5 Maana silaha zote za mtu mwenye silaha wakati wa mshindo, na mavazi yaliyofingirishwa katika damu, yatakuwa tayari kuteketezwa, yatakuwa kuni za kutiwa motoni.
2 Thessaloniciens 1.8 Actes 2.19 Esaïe 37.36 Esaïe 30.33 Nahum 3.2
6 Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.
Luc 2.11 Matthieu 28.18 Esaïe 7.14 Jérémie 23.5-23.6 Apocalypse 19.16

Jugement d’Israël et de Juda

7 Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.
Daniel 2.44 Luc 1.32-1.33 Esaïe 37.32 Jérémie 33.15-33.21 Jérémie 23.5
8 Bwana alimpelekea Yakobo neno, likamfikilia Israeli.
Michée 1.1-1.9 Zacharie 5.1-5.4 Zacharie 1.6 Esaïe 8.4-8.8 Esaïe 7.7-7.8
9 Nao watu wote watajua, yaani, Efraimu na yeye akaaye Samaria, wasemao kwa kiburi na kwa kujisifu nafsi zao,
Esaïe 46.12 Ezéchiel 7.27 Esaïe 7.8-7.9 1 Pierre 5.5 Ezéchiel 33.33
10 Matofali yameanguka, lakini sisi tutajenga kwa mawe yaliyochongwa; mikuyu imekatwa lakini sisi tutaweka mierezi badala yake.
Malachie 1.4 1 Rois 7.9-7.12
11 Kwa sababu hiyo Bwana atawainua adui wa Resini juu yake, naye atawachochea adui zake;
Esaïe 7.8 Esaïe 10.9-10.11 2 Rois 16.9 Esaïe 17.1-17.5 Esaïe 8.4-8.7
12 Waashuri upande wa mbele, na Wafilisti upande wa nyuma, nao watamla Israeli kwa kinywa kilicho wazi. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.
2 Chroniques 28.18 Esaïe 5.25 2 Rois 16.6 Psaumes 79.7 Jérémie 10.25
13 Lakini watu hao hawakumwelekea yeye aliyewapiga, wala kumtafuta Bwana wa majeshi.
Osée 7.10 Esaïe 31.1 Jérémie 5.3 Esaïe 1.5 2 Chroniques 28.22
14 Kwa sababu hiyo Bwana atakata katika Israeli kichwa na mkia, kuti na nyasi, katika siku moja.
Esaïe 19.15 Apocalypse 18.8 Osée 4.5 Amos 9.1-9.9 Osée 1.4
15 Mzee mwenye kuheshimiwa ndiye kichwa, na nabii afundishaye uongo ndiye mkia.
Matthieu 24.24 Esaïe 3.2-3.3 Esaïe 29.10 Jérémie 28.15-28.16 Esaïe 28.17
16 Kwa maana wawaongozao watu hawa ndio wawakoseshao, na hao walioongozwa na watu hao wameangamia.
Matthieu 15.14 Esaïe 3.12 Nombres 6.23-6.26 Matthieu 23.16-23.36 2 Chroniques 30.27
17 Kwa sababu hiyo Bwana hatawafurahia vijana wao, wala hatawahurumia yatima zao wala wajane wao; maana kila mtu ni mnajisi, dhalimu, na kila ulimi hunena upumbavu. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.
Jérémie 18.21 Esaïe 10.6 Esaïe 27.11 Esaïe 5.25 Matthieu 12.34
18 Kwa maana uovu huteketeza kama moto; huila mibigili na miiba, naam, huwaka katika vichaka vya mwitu, nao hupaa juu katika mawingu mazito ya moshi.
Malachie 4.1 Psaumes 83.14 Nahum 1.10 Apocalypse 14.11 Deutéronome 32.22
19 Kwa sababu ya hasira ya Bwana wa majeshi nchi hii inateketea kabisa; watu hawa nao ni kama kuni zitiwazo motoni; hapana mtu amhurumiaye ndugu yake.
Michée 7.2 Michée 7.6 Esaïe 13.9 Esaïe 24.11-24.12 Ezéchiel 9.5
20 Hupokonya upande wa mkono wa kuume, nao huona njaa! Hula upande wa mkono wa kushoto, wala hawashibi! Watakula kila mtu nyama ya mkono wake mwenyewe.
Esaïe 49.26 Lamentations 4.10 Jérémie 19.9 Esaïe 8.21 Lévitique 26.26-26.29
21 Manase anamla Efraimu, naye Efraimu anamla Manase; nao wawili pamoja watakuwa juu ya Yuda. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.
Esaïe 5.25 Esaïe 9.12 2 Chroniques 28.6-28.8 Esaïe 9.17 Galates 5.15

Cette Bible est dans le domaine public.