Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 7.12
Bible en Swahili de l’est


Guerre contre Juda

1 Hata ikawa katika siku za Ahazi, mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, mfalme wa Yuda, Resini, mfalme wa Shamu, na Peka, mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, wakapanda wakaenda Yerusalemu ili kupigana nao, lakini hawakuweza kuushinda.
2 Rois 15.37 2 Rois 16.1 Psaumes 83.3-83.5 Esaïe 8.9-8.10 2 Rois 15.25
2 Kisha watu wa nyumba ya Daudi wakaambiwa kwamba Shamu wamefanya mapatano na Efraimu. Na moyo wake ukataharuki, na moyo wa watu wake, kama miti ya mwituni itikiswavyo na upepo.
Esaïe 7.13 Esaïe 8.12 Esaïe 9.9 Lévitique 26.36-26.37 Ezéchiel 37.16-37.19
3 Basi Bwana akamwambia Isaya, Haya, toka, umlaki Ahazi, wewe na Shear-yashubu mwana wako, huko mwisho wa mfereji wa birika la juu, katika njia kuu ya uwanja wa dobi;
Esaïe 36.2 2 Rois 18.17 Romains 9.27 Esaïe 6.13 Jérémie 22.1
4 ukamwambie, Angalia, ukatulie; usiogope wala usife moyo, kwa sababu ya mikia hii miwili ya vinga hivi vitokavyo moshi; kwa sababu ya hasira kali ya Resini na Shamu, na mwana wa Remalia.
Esaïe 30.15 Deutéronome 20.3 Amos 4.11 Esaïe 35.4 1 Samuel 17.32
5 Kwa kuwa Shamu amekusudia mabaya juu yako, pamoja na Efraimu na mwana wa Remalia, wakisema,
Zacharie 1.15 Psaumes 2.2 Psaumes 83.3-83.4 Nahum 1.11
6 Haya, na tupande ili kupigana na Yuda na kuwasumbua, tukabomoe mahali tupate kuingia, na kummilikisha mfalme ndani yake, huyo mwana wa Tabeeli.
7 Bwana MUNGU asema hivi, Neno hili halitasimama wala halitakuwa.
Esaïe 8.10 Actes 4.25-4.28 Esaïe 46.10-46.11 Daniel 4.35 Psaumes 2.4-2.6
8 Kwa maana kichwa cha Shamu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini; na katika muda wa miaka sitini na mitano Efraimu atavunjika vipande vipande, asiwe kabila ya watu tena;
Esaïe 17.1-17.3 Genèse 14.15 2 Rois 17.5-17.23 2 Samuel 8.6 Esaïe 8.4
9 tena kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia. Kwamba hamtaki kusadiki, bila shaka hamtathibitika.
2 Chroniques 20.20 Esaïe 8.6-8.8 Actes 27.25 Romains 11.20 1 Jean 5.10

Annonce de la naissance d’Emmanuel

10 Tena Bwana akasema na Ahazi akinena,
Esaïe 10.20 Esaïe 1.5 Esaïe 1.13 Esaïe 8.5 Osée 13.2
11 Jitakie ishara ya Bwana, Mungu wako; itake katika mahali palipo chini sana, au katika mahali palipo juu sana.
Esaïe 38.7-38.8 Esaïe 37.30 Esaïe 38.22 Jérémie 51.63-51.64 Juges 6.36-6.40
12 Lakini Ahazi akasema, Sitaitaka, wala sitamjaribu Bwana.
Ezéchiel 33.31 Malachie 3.15 Deutéronome 6.16 2 Chroniques 28.22 Actes 5.9
13 Naye akasema, Sikilizeni sasa, enyi nyumba ya Daudi; Je! Ni neno dogo kwenu kuwachosha wanadamu, hata mkataka kumchosha Mungu wangu pia?
Esaïe 43.24 Esaïe 7.2 Malachie 2.17 Esaïe 65.3-65.5 Genèse 30.15
14 Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.
Matthieu 1.23 Esaïe 9.6 Luc 1.31 Jean 1.14 Esaïe 8.8
15 Siagi na asali atakula, wakati ajuapo kuyakataa mabaya na kuyachagua mema.
Esaïe 7.22 Psaumes 51.5 Philippiens 1.9-1.10 Romains 12.9 Luc 2.40
16 Kwa maana kabla mtoto huyo hajajua kuyakataa mabaya na kuyachagua mema, nchi ile, ambayo wewe unawachukia wafalme wake wawili, itaachwa ukiwa.
Esaïe 8.4 Deutéronome 1.39 Osée 5.9 Esaïe 17.1-17.3 2 Rois 15.29-15.30

Jugement d’Israël

17 Bwana ataleta juu yako, na juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako, siku zisizokuja bado, tangu siku ile aliyoondoka Efraimu kutoka katika Yuda; yaani, mfalme wa Ashuru.
Esaïe 8.7-8.8 Esaïe 10.5-10.6 1 Rois 12.16-12.19 2 Chroniques 32.1-32.33 Esaïe 36.1-36.22
18 Tena itakuwa katika siku hiyo Bwana atampigia kelele inzi aliye katika pande za mwisho za mito ya Misri, na nyuki aliye katika nchi ya Ashuru
Esaïe 5.26 Josué 24.12 Exode 8.24 Exode 8.21 2 Rois 23.33-23.34
19 Nao watakuja na kutulia katika mabonde yaliyo ukiwa, na katika pango za majabali, na juu ya michongoma yote, na juu ya malisho yote.
Esaïe 2.19 Jérémie 16.16 2 Chroniques 33.11 Esaïe 2.21 Michée 7.17
20 Katika siku hiyo Bwana atanyoa kichwa na malaika ya miguuni, kwa wembe ulioajiriwa pande za ng’ambo ya Mto, yaani, kwa mfalme wa Ashuru, nao utazimaliza ndevu nazo.
Esaïe 8.7 Ezéchiel 5.1-5.4 Esaïe 10.15 Esaïe 1.5 Ezéchiel 29.20
21 Katika siku hiyo itakuwa ya kwamba mtu atalisha ng’ombe mke mchanga na kondoo wake wawili;
Jérémie 39.10 Esaïe 5.17 Esaïe 7.25 Esaïe 17.2 Esaïe 37.30
22 kisha itakuwa, kwa sababu wanyama hao watatoa maziwa mengi, atakula siagi; kwa maana kila mtu aliyesalia katika nchi hii atakula siagi na asali.
Esaïe 7.15 2 Samuel 17.29 Matthieu 3.4
23 Tena itakuwa katika siku hiyo kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu, iliyopata fedha elfu, patakuwa mahali pa mbigili na miiba tu.
Esaïe 5.6 Matthieu 21.33 Jérémie 4.26 Cantique 8.11-8.12 Hébreux 6.8
24 Mtu atakayekwenda huko atakwenda na mishale na upinde; kwa sababu nchi yote itakuwa ina mibigili na miiba.
Genèse 27.3
25 Na vilima vyote vilivyolimwa kwa jembe, hutafika huko kwa sababu ya kuiogopa mibigili na miiba, lakini hapo patakuwa mahali pa kupeleka ng’ombe, mahali pa kukanyagwa na kondoo.
Esaïe 7.21-7.22 Esaïe 5.17 Esaïe 13.20-13.22 Esaïe 17.2 Sophonie 2.6

Cette Bible est dans le domaine public.