Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 62.1
Bible en Swahili de l’est


Le salut de Jérusalem

1 Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo.
Esaïe 62.6-62.7 Proverbes 4.18 1 Pierre 2.9 Luc 2.30-2.32 Philippiens 2.15-2.16
2 Na mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha Bwana.
Esaïe 62.12 Esaïe 62.4 Genèse 17.15 Esaïe 65.15 Genèse 17.5
3 Nawe utakuwa taji ya uzuri katika mkono wa Bwana, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.
Zacharie 9.16 1 Thessaloniciens 2.19 Esaïe 28.5 Luc 2.14
4 Hutaitwa tena Aliyeachwa, wala nchi yako haitaitwa tena, Ukiwa; bali utaitwa Hefsiba; na nchi yako Beula;kwa kuwa Bwana anakufurahia ,na nchi yako itaolewa.
Sophonie 3.17 Jérémie 32.41 Esaïe 54.1 Osée 2.19-2.20 1 Pierre 2.10
5 Maana kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.
Esaïe 65.19 Hébreux 12.2 Jérémie 32.41 Esaïe 49.18-49.22 Psaumes 45.11-45.16
6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya;
Esaïe 52.8 Esaïe 56.10 2 Chroniques 8.14 Jérémie 6.17 Ezéchiel 3.17-3.21
7 wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani.
Sophonie 3.19-3.20 Jérémie 33.9 Luc 18.1-18.8 Apocalypse 11.15 Esaïe 60.18
8 Bwana ameapa kwa mkono wake wa kuume, na kwa mkono wa nguvu zake, Hakika sitawapa adui zako nafaka yako tena kuwa chakula chao; wala wageni hawatakunywa divai yako, uliyoifanyia kazi.
Deutéronome 28.33 Jérémie 5.17 Esaïe 65.21-65.23 Deutéronome 28.31 Juges 6.3-6.6
9 Lakini walioivuna, ndio watakaoila, na kumhimidi Bwana; na walioichuma, ndio watakaoinywa, ndani ya nyua za patakatifu pangu.
Deutéronome 12.12 Deutéronome 12.7 Deutéronome 14.23-14.29 Deutéronome 16.14 Deutéronome 16.11
10 Piteni, piteni, katika malango; Itengenezeni njia ya watu; Tutieni, tutieni barabara; toeni mawe yake; Twekeni bendera kwa ajili ya kabila za watu.
Esaïe 57.14 Esaïe 49.22 Esaïe 11.10 Esaïe 40.3 Hébreux 12.13
11 Tazama, Bwana ametangaza habari mpaka mwisho wa dunia, Mwambieni binti Sayuni, Tazama, wokovu wako unakuja; Tazama, thawabu yake i pamoja naye, Na malipo yake yako mbele zake.
Zacharie 9.9 Matthieu 21.5 Apocalypse 22.12 Jean 12.15 Esaïe 49.4
12 Nao watawaita, Watu watakatifu, Waliokombolewa na Bwana; Nawe utaitwa, Aliyetafutwa, Mji usioachwa.
1 Pierre 2.9 Esaïe 62.4 Deutéronome 26.19 Esaïe 35.9 Deutéronome 7.6

Cette Bible est dans le domaine public.