Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 56
Bible en Swahili de l’est


1 Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatende haki; kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa.
Matthieu 3.2 Psaumes 85.9 Romains 10.6-10.10 Psaumes 50.23 Esaïe 26.7-26.8
2 Heri afanyaye haya, na mwanadamu ayashikaye sana; azishikaye sabato asizivunje, auzuiaye mkono wake usifanye uovu wo wote.
Esaïe 58.13 Ezéchiel 20.12 Psaumes 112.1 Exode 31.13-31.16 Ezéchiel 20.20
3 Wala mgeni, aambatanaye na Bwana, asiseme hivi, Hakika yake Bwana atanitenga na watu wake; wala towashi asiseme, Mimi ni mti mkavu.
1 Corinthiens 6.17 Actes 13.47-13.48 Luc 7.6-7.8 Actes 10.1-10.2 Jérémie 38.7-38.13
4 Kwa maana Bwana awaambia hivi matowashi, wanaozishika sabato zangu, na kuyachagua mambo yanipendezayo, na kulishika sana agano langu;
Esaïe 56.6 Esaïe 56.2 Josué 24.15 Jérémie 50.5 Psaumes 119.111
5 Nitawapa hawa nyumbani mwangu, na ndani ya kuta zangu, kumbukumbu na jina, lililo jema kuliko kuwa na wana na binti; nitawapa jina lidumulo milele, lisilokatiliwa mbali.
Esaïe 55.13 Apocalypse 3.12 Jean 1.12 1 Timothée 3.15 Esaïe 48.19
6 Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu;
Jacques 2.5 Apocalypse 1.10 1 Corinthiens 16.22 Actes 11.23 2 Corinthiens 8.5
7 Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.
Marc 11.17 Luc 19.46 Matthieu 21.13 Malachie 1.11 Esaïe 2.2-2.3
8 Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli asema, Pamoja na hayo nitamkusanyia na wengine, zaidi ya hao walio wake waliokusanywa.
Jean 10.16 Esaïe 60.3-60.11 Ephésiens 2.14-2.16 Ephésiens 1.10 Jérémie 31.10

Reproches aux chefs et aux idolâtres

9 Enyi hayawani wote wa nyikani, njoni, Mle, enyi hayawani wote wa mwituni.
Jérémie 12.9 Ezéchiel 39.17 Apocalypse 19.17-19.18 Esaïe 18.6 Ezéchiel 29.5
10 Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.
Philippiens 3.2 Esaïe 29.10 Nahum 3.18 Jérémie 14.13-14.14 Matthieu 15.14
11 Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.
Michée 3.11 Ezéchiel 13.19 Ezéchiel 34.2-34.3 Jérémie 22.17 Ecclésiaste 5.10
12 Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa kama leo, Sikukuu kupita kiasi.
Psaumes 10.6 Esaïe 5.22 Proverbes 23.35 1 Corinthiens 15.32 Luc 12.19-12.20

Cette Bible est dans le domaine public.