Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 56.1
Bible en Swahili de l’est


1 Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatende haki; kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa.
Matthieu 3.2 Psaumes 85.9 Psaumes 24.4-24.6 Romains 1.17 Esaïe 51.5
2 Heri afanyaye haya, na mwanadamu ayashikaye sana; azishikaye sabato asizivunje, auzuiaye mkono wake usifanye uovu wo wote.
Esaïe 58.13 Exode 31.13-31.16 Ezéchiel 20.20 Jérémie 17.21-17.22 Ezéchiel 20.12
3 Wala mgeni, aambatanaye na Bwana, asiseme hivi, Hakika yake Bwana atanitenga na watu wake; wala towashi asiseme, Mimi ni mti mkavu.
Esaïe 14.1 Jérémie 39.16-39.17 Ephésiens 2.12 Sophonie 2.11 Ephésiens 2.22
4 Kwa maana Bwana awaambia hivi matowashi, wanaozishika sabato zangu, na kuyachagua mambo yanipendezayo, na kulishika sana agano langu;
Esaïe 56.6 Psaumes 119.111 Esaïe 27.5 Luc 10.42 Esaïe 55.3
5 Nitawapa hawa nyumbani mwangu, na ndani ya kuta zangu, kumbukumbu na jina, lililo jema kuliko kuwa na wana na binti; nitawapa jina lidumulo milele, lisilokatiliwa mbali.
Esaïe 55.13 Jean 1.12 1 Timothée 3.15 Apocalypse 3.12 1 Samuel 1.8
6 Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu;
Apocalypse 1.10 Jacques 2.5 Esaïe 60.10 Marc 12.30-12.34 Romains 8.28
7 Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.
Marc 11.17 Luc 19.46 Matthieu 21.13 Malachie 1.11 Esaïe 2.2-2.3
8 Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli asema, Pamoja na hayo nitamkusanyia na wengine, zaidi ya hao walio wake waliokusanywa.
Jean 10.16 Esaïe 60.3-60.11 Esaïe 66.18-66.21 Zacharie 10.8-10.10 Esaïe 54.7

Reproches aux chefs et aux idolâtres

9 Enyi hayawani wote wa nyikani, njoni, Mle, enyi hayawani wote wa mwituni.
Jérémie 12.9 Esaïe 18.6 Ezéchiel 29.5 Deutéronome 28.26 Ezéchiel 39.17
10 Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.
Philippiens 3.2 Esaïe 29.10 Jérémie 14.13-14.14 Nahum 3.18 Ezéchiel 33.6
11 Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.
Ezéchiel 13.19 Michée 3.11 Esaïe 1.3 Tite 1.7 Ezéchiel 34.2-34.3
12 Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa kama leo, Sikukuu kupita kiasi.
Esaïe 5.22 Psaumes 10.6 1 Corinthiens 15.32 Luc 12.19-12.20 Proverbes 23.35

Cette Bible est dans le domaine public.