Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 42.11
Bible en Swahili de l’est


Le serviteur de l’Éternel

1 Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu.
Philippiens 2.7 Esaïe 52.13 Esaïe 43.10 Luc 3.22 Esaïe 61.1
2 Hatalia, wala hatapaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu.
Matthieu 12.16-12.20 Zacharie 9.9 Luc 17.20 2 Timothée 2.24 Matthieu 11.29
3 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi utokao moshi hatauzima; atatokeza hukumu kwa kweli.
Matthieu 11.28 Psaumes 96.13 Psaumes 147.3 Ezéchiel 34.16 Jérémie 31.25
4 Hatazimia, wala hatakata tamaa, hata atakapoweka hukumu duniani; na visiwa vitaingojea sheria yake.
Esaïe 55.5 Genèse 49.10 Esaïe 60.9 Esaïe 53.2-53.12 Esaïe 9.7
5 Mungu Bwana anena, yeye aliyeziumba mbingu, na kuzitanda; yeye aliyeitandaza nchi na mazao yake; yeye awapaye pumzi watu walio juu yake; yeye awapaye roho wao waendao ndani yake.
Esaïe 45.18 Esaïe 45.12 Actes 17.25 Zacharie 12.1 Psaumes 24.1-24.2
6 Mimi, Bwana, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa;
Luc 2.32 Esaïe 49.8 Actes 13.47 Esaïe 49.6 Jérémie 23.5-23.6
7 kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa.
Esaïe 61.1 Esaïe 35.5 Esaïe 49.9 Hébreux 2.14-2.15 Jean 9.39
8 Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.
Esaïe 48.11 Exode 20.3-20.5 Psaumes 83.18 Exode 34.14 Exode 3.13-3.15
9 Tazama, mambo ya kwanza yamekuwa, nami nayahubiri mambo mapya; kabla hayajatokea nawapasheni habari zake.
Esaïe 43.19 Esaïe 46.9-46.10 2 Pierre 1.19-1.21 1 Rois 8.15-8.20 1 Rois 11.36
10 Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Na sifa zake tokea mwisho wa dunia; Ninyi mshukao baharini, na vyote vilivyomo, Na visiwa, nao wakaao humo.
Psaumes 33.3 Psaumes 40.3 Esaïe 42.4 Romains 15.9-15.11 Esaïe 49.13
11 Jangwa na miji yake na ipaze sauti zao, Vijiji vinavyokaliwa na Kedari; Na waimbe wenyeji wa Sela, Wapige kelele toka vilele vya milima.
Esaïe 32.16 Esaïe 60.7 Esaïe 41.18-41.19 Psaumes 120.5 Esaïe 35.6
12 Na wamtukuze Bwana, Na kutangaza sifa zake visiwani.
Psaumes 22.27 Apocalypse 7.9-7.12 Esaïe 66.18-66.19 Apocalypse 5.9-5.10 Esaïe 24.15-24.16
13 Bwana atatokea kama shujaa; Ataamsha wivu kama mtu wa vita; Atalia, naam, atapiga kelele; Atawatenda adui zake mambo makuu.
Nahum 1.2 Psaumes 78.65 Osée 11.10 Esaïe 66.14 Joël 3.16
14 Siku nyingi nimenyamaza kimya; nimenyamaza, nikajizuia; sasa nitapiga kelele kama mwanamke aliye katika kuzaa; nitaugua na kutweta pamoja.
Ecclésiaste 8.11-8.12 2 Pierre 3.9-3.10 2 Pierre 3.15 Job 32.20 Jérémie 15.6
15 Nitaharibu milima na vilima, nitavikausha vyote vimeavyo; nitaifanya mito ya maji kuwa visiwa, na kuyakausha maziwa ya maji.
Esaïe 50.2 Nahum 1.4-1.6 Esaïe 2.12-2.16 Esaïe 44.27 Habakuk 3.6-3.10
16 Nitawaleta vipofu kwa njia wasiyoijua; katika mapito wasiyoyajua nitawaongoza; nitafanya giza kuwa nuru mbele yao; na mahali palipopotoka kuwa pamenyoka. Haya nitayatenda, wala sitawaacha.
Ephésiens 5.8 Esaïe 30.21 Esaïe 40.4 Esaïe 29.18 Esaïe 32.3
17 Watarudishwa nyuma, wataaibishwa sana, hao wanaotumainia sanamu za mawe, na kuziambia sanamu za madini, Ninyi ndinyi miungu yetu.
Esaïe 1.29 Esaïe 44.11 Psaumes 97.7 Habakuk 2.18-2.20 Esaïe 44.17
18 Sikilizeni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona.
Esaïe 29.18 Marc 7.34-7.37 Esaïe 43.8 Proverbes 20.12 Luc 7.22
19 Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu? Au aliye kiziwi, kama mjumbe wangu nimtumaye? Ni nani aliye kipofu, kama yeye aliye na amani? Naam, kipofu kama mtumishi wa Bwana?
2 Corinthiens 4.4 Ezéchiel 12.2 Jérémie 5.21 Jérémie 4.22 Esaïe 41.8
20 Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake ya wazi, lakini hasikii.
Jean 9.37-9.40 Jérémie 6.10 Marc 6.19-6.20 Actes 28.22-28.27 Deutéronome 4.9
21 Bwana akapendezwa, kwa ajili ya haki yake, kuitukuza sheria, na kuiadhimisha.
2 Corinthiens 5.19-5.21 Matthieu 5.17-5.20 Matthieu 17.5 Hébreux 8.10 Galates 5.22-5.23
22 Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.
Esaïe 14.17 Luc 21.20-21.24 Jérémie 50.17 Esaïe 45.13 Jérémie 51.34-51.35
23 Ni nani miongoni mwenu atakayetega sikio lake kuyasikia hayo? Atakayesikiliza na kusikia kwa wakati ujao?
Esaïe 48.18 Proverbes 1.22-1.23 Esaïe 1.18-1.20 Actes 3.22-3.23 Deutéronome 32.29
24 Ni nani aliyemtoa Yakobo awe mateka, aliyemtia Israeli katika mikono ya wanyang’anyi? Si yeye, Bwana? Yeye tuliyemkosa, ambaye hawakutaka kwenda katika njia zake, wala hawakuitii sheria yake.
2 Chroniques 36.17 Lamentations 1.14 Esaïe 30.15 Deutéronome 28.49 Jérémie 5.15
25 Kwa sababu hiyo alimwaga ukali wa hasira yake juu yake, na nguvu za vita; ukawasha moto wa kumzunguka pande zote, wala hakujua; ukamteketeza, wala hakuyatia hayo moyoni mwake.
Osée 7.9 Esaïe 57.11 Esaïe 57.1 2 Rois 25.9 Ezéchiel 20.34

Cette Bible est dans le domaine public.