Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 6.2
Bible en Swahili de l’est


Les filles de Jérusalem

1 Mpendwa wako amekwenda wapi, Wewe uliye mzuri katika wanawake? Mpendwa wako amegeukia upande upi, Ili tumtafute pamoja nawe?
Cantique 1.8 Cantique 5.9 Esaïe 2.5 Actes 5.11-5.14 Zacharie 8.21-8.23

La jeune femme

2 Mpendwa wangu ameshukia bustani yake, Kwenye matuta ya rihani; Ili kulisha penye bustani, Ili kuchuma nyinyoro.
Cantique 5.13 Jean 4.34-4.35 Cantique 1.7-1.8 Jean 17.24 Esaïe 58.11
3 Mimi ni wake mpendwa wangu, naye ni wangu, Hulisha kundi lake penye nyinyoro.
Cantique 2.16 Cantique 7.10 Hébreux 8.10 Apocalypse 21.2-21.4

Le jeune homme

4 Mpenzi wangu, u mzuri kama Tirza, Mwenye kupendeza kama Yerusalemu, Wa kutisha kama wenye bendera.
Cantique 6.10 Psaumes 48.2 1 Rois 14.17 Lamentations 2.15 Psaumes 50.2
5 Uyageuzie macho yako mbali nami, Kwa maana yamenitisha sana. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi, Wakijilaza mbavuni pa Gileadi.
Genèse 32.26-32.28 Exode 32.10 Matthieu 15.27-15.28 Cantique 4.1-4.3 Jérémie 15.1
6 Meno yako kama kundi la kondoo, Wakipanda kutoka kuoshwa; Ambao kila mmoja amezaa mapacha, Wala hakuna aliyefiwa kati yao.
Cantique 4.2 Matthieu 21.19 Matthieu 25.30
7 Mashavu yako ni kama kipande cha komamanga, Nyuma ya barakoa yako.
Cantique 4.3
8 Wako malkia sitini, na masuria themanini, Na wanawali wasiohesabika;
Psaumes 45.14 2 Chroniques 11.21 1 Rois 11.3 Psaumes 45.9 1 Rois 11.1
9 Hua wangu, mkamilifu wangu, ni mmoja tu, Mtoto wa pekee wa mamaye. Ndiye kipenzi chake aliyemzaa, Binti wakamwona wakamwita heri; Malkia na masuria nao wakamwona, Wakamsifu, wakisema,
Cantique 5.2 Cantique 2.14 Psaumes 45.9 Proverbes 31.28-31.29 Deutéronome 33.29

Les filles de Jérusalem

10 Ni nani huyu atazamaye kama alfajiri, Mzuri kama mwezi, safi kama jua, Wa kutisha kama wenye bendera?
Cantique 6.4 Job 31.26 Apocalypse 10.1 Ephésiens 5.27 Apocalypse 22.5

Le jeune homme

11 Nalishukia bustani ya milozi, Ili kuyatazama machipuko ya bondeni; Nione kama mzabibu umechanua, Kama mikomamanga imetoa maua.
Cantique 7.12 Actes 15.36 Psaumes 92.12-92.15 Marc 11.13 Luc 13.7
12 Kabla sijajua, roho yangu ilinileta Katikati ya magari ya wakuu wangu.
Osée 11.8-11.9 Jérémie 31.18-31.20 Luc 15.20
13 Rudi, rudi, Mshulami, Rudi, rudi, ili sisi tukutazame.
Genèse 32.2 Cantique 1.6 Luc 7.44 Osée 14.1-14.4 Jean 10.16

Cette Bible est dans le domaine public.