Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 28.23
Bible en Swahili de l’est


1 Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
Deutéronome 28.7 Psaumes 53.5 Lévitique 26.17 1 Thessaloniciens 2.2 Actes 14.3
2 Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi; Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa
Genèse 45.5-45.8 1 Rois 16.8-16.29 2 Rois 15.8-15.31 Ecclésiaste 9.15 2 Chroniques 32.20-32.26
3 Mtu mhitaji awaoneaye maskini, Ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza chakula.
Matthieu 18.28-18.30
4 Wao waiachao sheria huwasifu waovu; Bali wao waishikao hushindana nao.
Ephésiens 5.11 Romains 1.32 1 Rois 18.18 Matthieu 14.4 Matthieu 3.7
5 Watu wabaya hawaelewi na hukumu; Bali wamtafutao Bwana huelewa na yote.
Psaumes 92.6 Jean 7.17 1 Jean 2.27 1 Jean 2.20 Jacques 1.5
6 Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotofu wa njia angawa ni tajiri.
Proverbes 19.1 Luc 16.19-16.23 Proverbes 28.18 Proverbes 19.22 Actes 24.24-24.27
7 Yeye aishikaye sheria ni mwana mwenye hekima; Bali aliye rafiki wa walafi humwaibisha babaye.
Proverbes 2.1-2.6 Proverbes 29.3 1 Pierre 4.3-4.4 Proverbes 19.26 Luc 15.30
8 Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
Proverbes 13.22 Lévitique 25.36 Proverbes 14.31 Exode 22.25 Ezéchiel 18.13
9 Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria, Hata sala yake ni chukizo.
Psaumes 109.7 Psaumes 66.18 Zacharie 7.11-7.13 Esaïe 1.15-1.16 Proverbes 15.8
10 Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya, Ataanguka katika rima lake mwenyewe; Bali wakamilifu watarithi mema.
Proverbes 26.27 Matthieu 6.33 Psaumes 37.25-37.26 Proverbes 15.6 2 Pierre 2.18-2.20
11 Mtu tajiri ana hekima machoni pake mwenyewe; Bali maskini mwenye ufahamu humchunguza sana.
Romains 12.16 Proverbes 26.16 Ecclésiaste 9.15-9.17 Esaïe 10.13-10.14 1 Corinthiens 3.18-3.19
12 Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi; Bali waovu waondokapo, watu hujificha.
Proverbes 29.2 Proverbes 11.10 Proverbes 28.28 Hébreux 11.37-11.38 1 Rois 17.3-17.24
13 Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.
Job 31.33 Psaumes 32.3-32.5 1 Jean 1.8-1.10 Jérémie 2.22-2.23 Daniel 9.20-9.23
14 Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote; Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.
Proverbes 23.17 Esaïe 66.2 Jérémie 32.40 Romains 11.20 Romains 2.4
15 Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa; Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.
Matthieu 2.16 1 Pierre 5.8 2 Rois 21.16 Exode 1.22 Proverbes 19.12
16 Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana; Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake.
Esaïe 3.12 Exode 18.21 1 Rois 12.14 Amos 4.1 Néhémie 5.15
17 Aliyelemewa na damu ya mtu Atalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.
Genèse 9.6 Exode 21.14 2 Chroniques 24.21-24.25 1 Rois 21.23 1 Rois 21.19
18 Aendaye kwa unyofu ataokolewa; Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.
Proverbes 10.9 Proverbes 28.6 1 Thessaloniciens 5.3 2 Pierre 2.1-2.3 Proverbes 10.25
19 Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.
Proverbes 12.11 Juges 9.4 Proverbes 23.20-23.21 Proverbes 27.23-27.27 Proverbes 13.20
20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.
Proverbes 20.21 Proverbes 13.11 Luc 16.10-16.12 Proverbes 28.22 Néhémie 7.2
21 Kupendelea watu si kwema; Wala mtu kuasi kwa ajili ya kipande cha mkate.
Ezéchiel 13.19 Proverbes 18.5 Proverbes 24.23 Michée 7.3 Michée 3.5
22 Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri; Wala haufikiri uhitaji utakaomjilia.
Proverbes 23.6 Proverbes 28.20 1 Timothée 6.9 Genèse 19.17 Genèse 13.10-13.13
23 Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali; Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.
Proverbes 27.5-27.6 Matthieu 18.15 1 Rois 1.23 Galates 2.11 Proverbes 29.5
24 Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa; Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.
Proverbes 18.9 Proverbes 19.26 Proverbes 28.7 Matthieu 15.4-15.6 Juges 17.2
25 Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina; Bali amtumainiye Bwana atawandishwa.
Proverbes 15.18 Proverbes 11.25 1 Timothée 6.6 Proverbes 13.4 Proverbes 21.24
26 Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga; Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.
Proverbes 3.5 Jacques 3.13-3.18 Job 28.28 Romains 8.7 Marc 14.27-14.31
27 Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu; Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.
Proverbes 19.17 Deutéronome 15.7 Proverbes 22.9 Proverbes 11.26 Psaumes 41.1-41.3
28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.
Proverbes 28.12 Proverbes 29.2 Actes 12.23-12.24 Job 24.4 Esther 8.17

Cette Bible est dans le domaine public.