Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 27.8
Bible en Swahili de l’est


L’autel des holocaustes

1 Nawe fanya madhabahu ya mti wa mshita; urefu wake utakuwa ni dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano; hiyo madhabahu itakuwa mraba; na kwenda juu kwake kutakuwa dhiraa tatu.
Exode 38.1-38.7 Exode 24.4 Exode 20.24-20.26 2 Samuel 24.18 2 Chroniques 4.1
2 Nawe fanya pembe nne katika pembe zake nne; hizo pembe zitakuwa za kitu kimoja na madhabahu; nawe utayafunika shaba.
Psaumes 118.27 Lévitique 4.7 Exode 29.12 1 Rois 1.50 1 Rois 2.28
3 Na vyombo vyake vya kuyaondoa majivu yake utavifanya, na majembe yake, na mabakuli yake, na uma zake, na meko yake; vyombo vyake vyote utavifanya vya shaba.
1 Rois 7.45 Jérémie 52.18-52.20 Lévitique 16.12 2 Chroniques 4.11 2 Rois 25.15
4 Nawe uifanyie hiyo madhabahu wavu wa shaba; kisha utie pete nne za shaba katika hizo pembe nne za ule wavu.
Exode 38.4-38.5 Exode 25.12 Exode 35.16
5 Nawe tia huo wavu chini ya kizingo kiizungukacho madhabahu upande wa chini, ili huo wavu ufikilie katikati ya hiyo madhabahu.
Exode 38.4
6 Nawe fanya miti kwa ajili ya madhabahu, miti ya mshita, na kuifunika shaba.
Nombres 4.44 Exode 35.13-35.15 Exode 30.4
7 Na hiyo miti itatiwa katika pete, na ile miti itakuwa katika pande mbili za madhabahu, wakati wa kuichukua.
Nombres 4.13-4.14 Exode 30.4 Exode 25.28
8 Uifanye ya mbao, yenye mvungu ndani yake; kama ulivyoonyeshwa mlimani, ndivyo watakavyoifanya.
Exode 25.40 Hébreux 8.5 Exode 25.9 Colossiens 2.20-2.23 1 Chroniques 28.19

Le parvis et son entrée

9 Nawe fanya ua wa maskani; upande wa kusini wa kuelekea kusini kutakuwa na chandarua ya nguo ya kitani nzuri yenye kusokotwa, kwa huo ua, urefu wake upande mmoja utakuwa ni dhiraa mia;
Exode 38.9-38.20 Ezéchiel 40.44 Ezéchiel 46.20-46.24 Ezéchiel 42.19-42.20 Ezéchiel 40.32
10 na nguzo zake zitakuwa nguzo ishirini, na matako yake ishirini, matako yake yatakuwa ya shaba; kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
Exode 26.19-26.21 Jérémie 52.21 Exode 36.38
11 Ni vivyo upande wa kaskazini, urefu wake hiyo chandarua utakuwa ni dhiraa mia, na nguzo zake ishirini, na matako yake ishirini yatakuwa ya shaba; kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
12 Na upande wa magharibi, upana wa ua kutakuwa na chandarua ya dhiraa hamsini; nguzo zake kumi, na matako yake kumi.
13 Na upana wa ule ua upande wa mashariki kuelekea mashariki utakuwa ni dhiraa hamsini.
14 Chandarua upande mmoja wa lango itakuwa dhiraa kumi na tano upana wake; nguzo zake zitakuwa tatu na matako yake matatu.
Exode 26.36 Exode 27.9
15 Upande wa pili ni vivyo chandarua ya dhiraa kumi na tano; nguzo zake tatu, na matako yake matatu.
16 Na kwa lile lango la ua patakuwa na kisitiri cha dhiraa ishirini, kitakuwa cha nguo ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshona taraza; nguzo zake zitakuwa nne, na matako yake manne.
Exode 26.36 Exode 26.31 Exode 36.37 Exode 28.39 Exode 39.29
17 Nguzo zote za ule ua ziuzungukazo pande zote zitakuwa na vitanzi vya fedha; kulabu zake za fedha, na matako yake ya shaba.
18 Urefu wa huo ua utakuwa dhiraa mia, na upana wake utakuwa dhiraa hamsini kotekote, na kwenda juu kwake dhiraa tano; yawe ya nguo ya kitani nzuri, na matako yake yatakuwa ya shaba.
19 Vyombo vyote vya maskani vitumiwavyo katika utumishi wake wote, na vigingi vyake vyote, na vigingi vyote vya ule ua, vitakuwa vya shaba.
Exode 39.40 Ecclésiaste 12.11 Nombres 4.32 Nombres 3.37 Esdras 9.8

L’huile pour les lampes

20 Nawe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima.
Apocalypse 11.4 Exode 39.37 Psaumes 23.5 Juges 9.9 Exode 25.31-25.37
21 Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza tangu jioni hata asubuhi mbele ya Bwana; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israeli.
Nombres 19.21 Nombres 18.23 2 Chroniques 13.11 1 Samuel 3.3 Lévitique 3.17

Cette Bible est dans le domaine public.