Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 96.13
Bible en Swahili de l’est


Hymne à la grandeur et à la gloire de Dieu

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Mwimbieni Bwana, nchi yote.
Psaumes 33.3 1 Chroniques 16.23-16.33 Psaumes 98.1 Psaumes 149.1 Apocalypse 14.3
2 Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake, Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
Psaumes 71.15 Marc 16.15 Esaïe 52.7-52.8 1 Chroniques 29.20 Psaumes 72.17-72.18
3 Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, Na watu wote habari za maajabu yake.
Daniel 4.1-4.3 Psaumes 117.1-117.2 Matthieu 28.19 Psaumes 22.27 Psaumes 72.18-72.19
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kusifiwa sana. Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
Psaumes 18.3 Psaumes 89.7 Psaumes 95.3 Psaumes 145.3 Psaumes 86.10
5 Maana miungu yote ya watu si kitu, Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu.
Psaumes 115.15 Esaïe 42.5 Jérémie 10.11-10.12 Psaumes 135.15 1 Corinthiens 8.4
6 Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Psaumes 104.1 Psaumes 93.1 Psaumes 50.2 Psaumes 8.1 Hébreux 1.3
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za watu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Psaumes 22.27 Psaumes 29.1-29.2 Matthieu 6.13 Jude 1.24-1.25 Romains 15.9-15.10
8 Mpeni Bwana utukufu wa jina lake, Leteni sadaka mkaziingie nyua zake.
Psaumes 100.4 Malachie 1.11 Psaumes 108.3-108.5 Hébreux 13.15-13.16 Psaumes 72.10
9 Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu, Tetemekeni mbele zake, nchi yote.
Psaumes 29.2 Psaumes 33.8 Psaumes 110.3 Psaumes 114.7 Psaumes 76.7
10 Semeni katika mataifa, Bwana ametamalaki; Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike, Atawahukumu watu kwa adili.
Psaumes 93.1 Psaumes 9.8 Psaumes 67.4 Apocalypse 19.11 Matthieu 3.2
11 Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie, Bahari na ivume na vyote viijazavyo,
Esaïe 49.13 Psaumes 69.34 Psaumes 97.1 Psaumes 98.7-98.9 Esaïe 44.23
12 Mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo, Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha;
Esaïe 55.12-55.13 Psaumes 65.12-65.13 Esaïe 42.10-42.11 Esaïe 44.23 Esaïe 35.1
13 Mbele za Bwana, kwa maana anakuja, Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa uaminifu wake.
Apocalypse 19.11 Psaumes 98.9 2 Timothée 4.8 2 Pierre 3.12-3.14 Apocalypse 22.10

Cette Bible est dans le domaine public.