Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 96
Bible en Swahili de l’est


Hymne à la grandeur et à la gloire de Dieu

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Mwimbieni Bwana, nchi yote.
Psaumes 33.3 1 Chroniques 16.23-16.33 Psaumes 98.1 Psaumes 149.1 Apocalypse 14.3
2 Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake, Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
Psaumes 71.15 Marc 16.15 Psaumes 72.17-72.18 Ephésiens 1.3 Psaumes 145.1
3 Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, Na watu wote habari za maajabu yake.
Matthieu 28.19 Psaumes 22.27 Psaumes 72.18-72.19 Daniel 6.26-6.27 Michée 4.2
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kusifiwa sana. Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
Psaumes 18.3 Psaumes 89.7 Psaumes 95.3 Psaumes 145.3 Jérémie 5.22
5 Maana miungu yote ya watu si kitu, Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu.
Psaumes 115.15 Esaïe 42.5 Jérémie 10.11-10.12 1 Corinthiens 8.4 Genèse 1.1
6 Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Psaumes 104.1 Psaumes 8.1 Hébreux 1.3 Psaumes 29.1-29.2 Psaumes 19.1
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za watu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Psaumes 22.27 Psaumes 29.1-29.2 Jude 1.24-1.25 Romains 15.9-15.10 Apocalypse 19.1
8 Mpeni Bwana utukufu wa jina lake, Leteni sadaka mkaziingie nyua zake.
Psaumes 100.4 Malachie 1.11 Psaumes 108.3-108.5 Hébreux 13.15-13.16 Psaumes 72.10
9 Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu, Tetemekeni mbele zake, nchi yote.
Psaumes 29.2 Psaumes 33.8 Psaumes 114.7 Psaumes 110.3 Esdras 7.27
10 Semeni katika mataifa, Bwana ametamalaki; Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike, Atawahukumu watu kwa adili.
Psaumes 93.1 Psaumes 9.8 Psaumes 67.4 Psaumes 46.10 Romains 2.5-2.6
11 Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie, Bahari na ivume na vyote viijazavyo,
Esaïe 49.13 Psaumes 69.34 Psaumes 97.1 Psaumes 98.7-98.9 Luc 2.13-2.14
12 Mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo, Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha;
Esaïe 55.12-55.13 Psaumes 65.12-65.13 Esaïe 42.10-42.11 Esaïe 44.23 Esaïe 35.1
13 Mbele za Bwana, kwa maana anakuja, Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa uaminifu wake.
Apocalypse 19.11 Psaumes 98.9 2 Pierre 3.12-3.14 Apocalypse 22.10 Psaumes 67.4

Cette Bible est dans le domaine public.