Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 36
Bible en Swahili de l’est


Le méchant et sa punition

1 Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake, Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
Romains 3.18 Psaumes 18.1 1 Samuel 15.13-15.14 Tite 1.1 Proverbes 8.13
2 Kwa maana hujipendekeza machoni pake Kuwa upotovu wake hautaonekana na kuchukiwa.
Deutéronome 29.19 Psaumes 49.18 Psaumes 10.3 1 Chroniques 10.13-10.14 Luc 16.14-16.15
3 Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila, Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.
Psaumes 55.21 Jérémie 4.22 Psaumes 10.7 Psaumes 140.3 1 Samuel 18.21
4 Huwaza maovu kitandani pake, Hujiweka katika njia mbaya; ubaya hauchukii.
Esaïe 65.2 Michée 2.1 Proverbes 4.16 Romains 12.9 Psaumes 97.10
5 Ee Bwana, fadhili zako zafika hata mbinguni, Uaminifu wako hata mawinguni.
Psaumes 103.11 Psaumes 108.4 Psaumes 57.10 Psaumes 89.2 Psaumes 92.2
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu, Hukumu zako ni vilindi vikuu, Ee Bwana, unawaokoa wanadamu na wanyama.
Romains 11.33 Psaumes 71.19 Psaumes 77.19 Psaumes 145.9 Psaumes 92.5
7 Ee Mungu, jinsi zilivyo na thamani fadhili zako! Wanadamu huukimbilia uvuli wa mbawa zako.
Ruth 2.12 Psaumes 91.4 Psaumes 17.8 Psaumes 31.19 Psaumes 57.1
8 Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako, Nawe utawanywesha mto wa furaha zako.
Psaumes 65.4 Psaumes 16.11 Esaïe 25.6 Jérémie 31.12-31.14 Esaïe 58.11
9 Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima, Katika nuru yako tutaona nuru.
Jérémie 2.13 1 Pierre 2.9 Jean 4.14 Jean 4.10 Jean 8.12
10 Uwadumishie wakujuao fadhili zako, Na wanyofu wa moyo uaminifu wako.
Jérémie 22.16 Psaumes 97.10-97.11 2 Timothée 4.7-4.8 Hébreux 8.11 Psaumes 18.24-18.25
11 Mguu wa kiburi usinikaribie, Wala mkono wa wasio haki usinifukuze.
Psaumes 17.8-17.14 Psaumes 119.122 Psaumes 21.7-21.8 Daniel 4.37 Job 40.11-40.12
12 Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu; Wameangushwa chini wasiweze kusimama.
Psaumes 1.5 Psaumes 18.38 Psaumes 55.23 Apocalypse 15.4 Psaumes 58.10-58.11

Cette Bible est dans le domaine public.