Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 32.1
Bible en Swahili de l’est


Le bonheur du pécheur pardonné

1 Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake.
Romains 4.6-4.8 Psaumes 85.2 Actes 13.38-13.39 Esaïe 44.22 Psaumes 40.4
2 Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, Ambaye rohoni mwake hamna hila.
Jean 1.47 Lévitique 17.4 Romains 5.13 Apocalypse 14.5 2 Corinthiens 1.12
3 Niliponyamaza mifupa yangu ilichakaa Kwa kuugua kwangu mchana kutwa.
Psaumes 38.8 Psaumes 22.1 Lamentations 3.8 Job 3.24 Psaumes 102.3-102.5
4 Kwa maana mchana na usiku Mkono wako ulinilemea. Jasho langu likakauka hata nikawa Kama nchi kavu wakati wa kaskazi.
Job 33.7 1 Samuel 5.11 Psaumes 22.15 Psaumes 102.3-102.4 1 Samuel 5.9
5 Nalikujulisha dhambi yangu, Wala sikuuficha upotovu wangu. Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa Bwana, Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.
2 Samuel 12.13 Esaïe 65.24 Proverbes 28.13 Psaumes 38.18 Psaumes 86.5
6 Kwa hiyo kila mtu mtauwa Akuombe wakati unapopatikana. Hakika maji makuu yafurikapo, Hayatamfikia yeye.
Esaïe 55.6 Esaïe 43.2 Psaumes 42.7 Jean 7.34 2 Corinthiens 6.2
7 Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso, Utanizungusha nyimbo za wokovu.
Psaumes 9.9 Psaumes 119.114 Psaumes 31.20 Juges 5.1 Exode 15.1-15.3
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.
Proverbes 3.5-3.6 Matthieu 11.29 Esaïe 49.10 Psaumes 33.18 Proverbes 3.1
9 Msiwe kama farasi wala nyumbu, Walio hawana akili. Kwa matandiko ya lijamu na hatamu Sharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia.
Proverbes 26.3 Job 35.11 Jacques 3.3 Jacques 4.7-4.10 Jérémie 4.22
10 Naye mtu mwovu ana mapigo mengi, Bali amtumainiye Bwana fadhili zitamzunguka.
Proverbes 16.20 Proverbes 13.21 Psaumes 34.8 Psaumes 16.4 Psaumes 5.12
11 Mfurahieni Bwana; Shangilieni, enyi wenye haki Pigeni vigelegele vya furaha; Ninyi nyote mlio wanyofu wa moyo.
Psaumes 64.10 Psaumes 68.3 Philippiens 4.4 Psaumes 97.12 Psaumes 33.1

Cette Bible est dans le domaine public.