Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 30.4
Bible en Swahili de l’est


Louange après la délivrance

1 Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya.
3 Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni.
4 Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.
5 Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha.
6 Nami nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele.
7 Bwana, kwa radhi yako Wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha uso wako, Nami nikafadhaika.
8 Ee Bwana, nalikulilia Wewe, Naam, kwa Bwana naliomba dua.
9 Mna faida gani katika damu yangu Nishukapo shimoni? Mavumbi yatakusifu? Yataitangaza kweli yako?
10 Ee Bwana, usikie, unirehemu, Bwana, uwe msaidizi wangu.
11 Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha.
12 Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele.

Cette Bible est dans le domaine public.