Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 142.2
Bible en Swahili de l’est


1 Kwa sauti yangu nitamlilia Bwana, Kwa sauti yangu nitamwomba Bwana dua.Psaumes 57.1 Psaumes 30.8 Psaumes 54.1 Psaumes 141.1 Psaumes 28.2
2 Nitafunua mbele zake malalamiko yangu, Shida yangu nitaitangaza mbele zake.Hébreux 5.7 Romains 8.26 Psaumes 102.1-102.28 Esaïe 26.16 Psaumes 62.8
3 Nilipozimia roho uliyajua mapito yangu; Katika njia niendayo wamenifichia mtego.Psaumes 140.5 Psaumes 143.4 Psaumes 102.4 Job 23.10 Psaumes 35.7-35.8
4 Utazame mkono wa kuume ukaone, Kwa maana sina mtu anijuaye. Makimbilio yamenipotea, Hakuna wa kunitunza roho.Psaumes 31.11 Psaumes 88.18 Psaumes 69.20 Psaumes 88.8 Jérémie 25.35
5 Bwana, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu, Fungu langu katika nchi ya walio hai.Psaumes 16.5 Psaumes 27.13 Psaumes 46.1 Jean 16.32 Psaumes 73.26
6 Ukisikilize kilio changu, Kwa maana nimedhilika sana. Uniponye nao wanaonifuatia, Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi.Psaumes 79.8 Psaumes 116.6 Psaumes 17.1 Psaumes 44.24-44.26 Romains 8.33
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni. Nipate kulishukuru jina lako. Wenye haki watanizunguka, Kwa kuwa Wewe unanikirimu.Psaumes 13.6 Psaumes 143.11 Psaumes 146.7 Psaumes 9.3 Psaumes 119.74

Cette Bible est dans le domaine public.