Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 107.35
Bible en Swahili de l’est


Cinquième livre

La grâce divine

1 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Psaumes 106.1 2 Chroniques 7.3 1 Chroniques 16.34 2 Chroniques 5.13 Psaumes 118.1
2 Na waseme hivi waliokombolewa na Bwana, Wale aliowakomboa na mkono wa mtesi.
Galates 3.13 Psaumes 106.10 1 Pierre 1.18-1.19 Deutéronome 7.8 Esaïe 35.9
3 Akawakusanya kutoka nchi zote, Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini.
Psaumes 106.47 Deutéronome 30.3 Ezéchiel 39.27 Jérémie 31.8 Esaïe 43.5-43.6
4 Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa.
Deutéronome 32.10 Nombres 14.33 Ezéchiel 34.12 Job 12.24 Ezéchiel 34.6
5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.
Juges 15.18-15.19 Jérémie 14.18 1 Samuel 30.11-30.12 Marc 8.2-8.3 Lamentations 2.19
6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
Psaumes 50.15 Psaumes 107.28 Psaumes 107.13 Psaumes 107.19 Jérémie 29.12-29.14
7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa.
Psaumes 107.36 Psaumes 107.4 Jérémie 31.9 Esaïe 35.8-35.10 Psaumes 78.52
8 Na wamshukuru Bwana, kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
Psaumes 107.15 Psaumes 107.21 Psaumes 107.31 Daniel 4.2-4.3 Psaumes 34.3
9 Maana hushibisha nafsi yenye shauku, Na nafsi yenye njaa huijaza mema.
Luc 1.53 Psaumes 34.10 Jérémie 31.14 Psaumes 132.15 Jérémie 31.25
10 Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma,
Luc 1.79 Matthieu 4.16 Romains 6.20-6.21 Matthieu 22.13 Job 3.5
11 Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, Wakalidharau shauri lake Aliye juu.
Psaumes 106.7 Psaumes 73.24 Proverbes 1.25 Luc 7.30 Psaumes 106.43
12 Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa wala hakuna msaidizi.
Psaumes 22.11 Exode 5.18-5.19 Esaïe 52.5 Néhémie 9.37 Juges 10.16-10.18
13 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
Psaumes 107.6 Psaumes 18.6 Psaumes 107.28 Psaumes 116.3-116.6 2 Chroniques 33.18-33.19
14 Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akayavunja mafungo yao.
Psaumes 116.16 Psaumes 107.10 Esaïe 42.16 Esaïe 61.1 Jérémie 52.31-52.34
15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
Psaumes 107.31 Psaumes 107.8 Psaumes 107.21 Psaumes 116.17-116.19
16 Maana ameivunja milango ya shaba, Ameyakata mapingo ya chuma.
Esaïe 45.1-45.2 Michée 2.13 Juges 16.3
17 Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao, Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa.
Lamentations 3.39 Psaumes 38.1-38.8 Nombres 21.5-21.9 Proverbes 7.7 Esaïe 57.17-57.18
18 Nafsi zao zachukia kila namna ya chakula, Wameyakaribia malango ya mauti.
Psaumes 88.3 Psaumes 9.13 Job 33.19-33.22 Job 38.17 Esaïe 38.10
19 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
Psaumes 107.28 Psaumes 30.8-30.12 Psaumes 107.6 Jérémie 33.3 Psaumes 107.13
20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.
Job 33.28-33.30 2 Rois 20.4-20.5 Psaumes 147.15 Matthieu 8.8 Psaumes 103.3-103.4
21 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
Psaumes 107.15 Psaumes 107.31 Psaumes 107.8 Psaumes 66.5 Luc 17.18
22 Na wamtolee dhabihu za kushukuru, Na kuyasimulia matendo yake kwa kuimba.
Psaumes 118.17 Psaumes 50.14 Psaumes 9.11 Psaumes 116.17 Lévitique 7.12
23 Washukao baharini katika merikebu, Wafanyao kazi yao katika maji mengi,
Actes 27.9-27.28 Psaumes 48.7 Ezéchiel 27.26 Esaïe 42.10 Apocalypse 18.17
24 Hao huziona kazi za Bwana, Na maajabu yake vilindini.
Psaumes 95.5 Psaumes 104.24-104.27 Job 38.8-38.11
25 Maana husema, akavumisha upepo wa dhoruba, Ukayainua juu mawimbi yake.
Jonas 1.4 Psaumes 148.8 Psaumes 93.3 Psaumes 105.31 Psaumes 105.34
26 Wapanda mbinguni, watelemka vilindini, Nafsi yao yayeyuka kwa hali mbaya.
Psaumes 22.14 Psaumes 119.28 Nahum 2.10 2 Samuel 17.10 Esaïe 13.7
27 Wayumba-yumba, wapepesuka kama mlevi, Akili zao zote zawapotea.
Job 12.25 Esaïe 19.14 Esaïe 19.3 Esaïe 29.9 Job 37.20
28 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
Actes 27.23-27.25 Psaumes 107.19 Matthieu 8.25 Psaumes 107.13 Psaumes 107.6
29 Huituliza dhoruba, ikawa shwari, Mawimbi yake yakanyamaza.
Matthieu 8.26 Psaumes 65.7 Psaumes 89.9 Jonas 1.15 Marc 4.39-4.41
30 Ndipo walipofurahi kwa kuwa yametulia Naye huwaleta mpaka bandari waliyoitamani.
Jean 6.21
31 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
Psaumes 107.8 Psaumes 107.21 Psaumes 107.15 Psaumes 103.2 Hébreux 13.15
32 Na wamtukuze katika kusanyiko la watu, Na wamhimidi katika baraza ya wazee.
Psaumes 22.25 Psaumes 22.22 Psaumes 99.5 Esaïe 25.1 Psaumes 35.18
33 Amegeuza mito ikawa jangwa, Na chemchemi za maji zikawa nchi ya kiu.
Esaïe 50.2 Esaïe 42.15 Joël 1.20 Psaumes 74.15 Nahum 1.4
34 Nchi ya matunda mengi ikawa uwanda wa chumvi, Kwa sababu ya ubaya wao walioikaa.
Genèse 14.3 Genèse 13.10 Ezéchiel 47.11 Esaïe 32.13-32.15 Deutéronome 29.23-29.28
35 Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji, Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.
Psaumes 114.8 Esaïe 41.17-41.19 Esaïe 35.6-35.7 Esaïe 44.3-44.5 Nombres 21.16-21.18
36 Maana amewakalisha huko wenye njaa, Nao wametengeneza mji wa kukaa.
Psaumes 107.7 Luc 1.53 Actes 17.26 Psaumes 146.7
37 Wakapanda mbegu katika mashamba, Na kutia mizabibu iliyotoa matunda yake.
1 Corinthiens 3.7 Ezéchiel 28.26 Zacharie 8.12 Genèse 26.12 Aggée 1.10-1.11
38 Naye huwabariki wakaongezeka sana, Wala hayapunguzi makundi yao.
Exode 1.7 Genèse 12.2 Genèse 17.20 Deutéronome 7.14 Genèse 17.16
39 Kisha wakapungua na kudhilika, Kwa kuonewa na mabaya na huzuni.
2 Rois 10.32 Genèse 45.11 Job 1.10-1.17 2 Rois 13.22 Ruth 1.20-1.21
40 Akawamwagia wakuu dharau, Na kuwazungusha katika nyika isiyo na njia.
Job 12.24 Job 12.21 Exode 8.17 Psaumes 107.4 Exode 8.24
41 Akamweka mhitaji juu mbali na mateso, Akamfanyia jamaa kama kundi la kondoo.
1 Samuel 2.8 Job 21.11 Esther 8.15-8.17 Psaumes 78.52 Job 5.11
42 Wanyofu wa moyo wataona na kufurahi, Na uovu wa kila namna utajifumba kinywa.
Job 22.19 Psaumes 63.11 Romains 3.19 Psaumes 52.6 Proverbes 10.11
43 Aliye na hekima na ayaangalie hayo; Na wazitafakari fadhili za Bwana.
Jérémie 9.12 Psaumes 64.9 Osée 14.9 Psaumes 50.23 Esaïe 5.12

Cette Bible est dans le domaine public.