Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 2.11
Bible en Swahili de l’est


Deuxième épreuve

1 Tena kulikuwa na siku hao wana wa Mungu walipokwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao, ili kujihudhurisha mbele za Bwana.
Job 1.6 Luc 1.19 Hébreux 1.14 Esaïe 6.1-6.2
2 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi? Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
1 Pierre 5.8 Genèse 16.8 Job 1.7 2 Corinthiens 4.4 Jean 14.30
3 Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu.
Job 1.8 Job 9.17 Job 1.1 Job 27.5-27.6 1 Pierre 5.10
4 Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.
Jérémie 41.8 Esther 7.3-7.4 Esaïe 2.20-2.21 Actes 27.18-27.19 Philippiens 3.8-3.10
5 Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako.
Job 1.11 Job 1.5 Esaïe 8.21 Psaumes 38.2-38.7 Psaumes 39.10
6 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake.
Job 1.12 Apocalypse 20.1-20.2 Apocalypse 20.7 Apocalypse 2.10 Job 38.10-38.11
7 Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.
Deutéronome 28.35 Esaïe 1.6 Job 30.30 Deutéronome 28.27 Job 7.5
8 Naye akashika kigae cha kujikunia; akaketi majivuni.
Job 42.6 Ezéchiel 27.30 Jonas 3.6 Matthieu 11.21 Luc 16.20-16.21
9 Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe.
Job 2.3 Job 2.5 Genèse 3.12 Genèse 3.6 Job 21.14-21.15
10 Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.
Job 1.21-1.22 Jacques 1.12 Psaumes 39.1 Jacques 5.10-5.11 Matthieu 16.23

Arrivée des amis de Job

11 Basi ikawa hao rafikize Ayubu watatu walipopata habari ya mabaya hayo yote yaliyomfikilia, wakaja kila mtu kutoka mahali pake; nao ni Elifazi Mtemani, na Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi; wakapatana pamoja ili waende kumlilia Ayubu na kumtuliza moyo.
Romains 12.15 Job 42.11 Genèse 25.2 Jérémie 49.7 Genèse 36.11
12 Basi walipovua macho yao, nao wakali mbali, wasimtambue, wakainua sauti zao na kulia; kila mmoja akararua joho yake, wakarusha mavumbi juu ya vichwa vyao kuelekea mbinguni.
Lamentations 2.10 Ezéchiel 27.30 Néhémie 9.1 Josué 7.6 Job 1.20
13 Kisha wakaketi nchi pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lo lote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.
Genèse 50.10 Néhémie 1.4 Ezéchiel 3.15 Esdras 9.3 Esaïe 47.1

Cette Bible est dans le domaine public.