Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esther 7.8
Bible en Swahili de l’est


Plaidoyer d’Esther

1 Basi mfalme na Hamani walikuja kula karamu pamoja na malkia Esta.
Esther 5.8 Esther 3.15
2 Mfalme akamwambia Esta tena siku ya pili pale pale penye karamu ya divai, Malkia Esta, dua yako ni nini? Nawe utapewa; na haja yako ni nini? Hata nusu ya ufalme utafanyiziwa.
Jean 16.24 Esther 5.6 Esther 9.12 Esther 5.3
3 Ndipo malkia Esta alipojibu, akasema, Mfalme, ikiwa nimepata kibali machoni pako, na mfalme akiona vema, nipewe maisha yangu kuwa dua yangu, na watu wangu kuwa haja yangu.
Psaumes 122.6-122.9 Job 2.4 Esther 7.7 Jérémie 38.26 Esther 4.8
4 Maana tumeuzwa, mimi na watu wangu, ili tuharibiwe, na kuuawa, na kuangamia. Kama tungaliuzwa kuwa watumwa na wajakazi, ningalinyamaza; ila hata hivyo msiba wetu haulinganishwi na hasara ya mfalme.
Esther 3.9 Deutéronome 28.68 Esther 3.13 Esther 8.11 Josué 9.23
5 Ndipo mfalme Ahasuero aliponena, akamwambia malkia Esta, Ni nani huyu, tena yuko wapi, ambaye moyoni mwake alithubutu kufanya hivi?
Job 9.24 Actes 5.3 Genèse 27.33
6 Esta akasema, Ni mtesi, tena ni adui, ndiye huyu Hamani, mtu mbaya kabisa. Mara Hamani akaingiwa na hofu mbele ya mfalme na malkia.
Job 18.5-18.12 Psaumes 139.19-139.22 2 Thessaloniciens 2.8 Proverbes 16.14 Job 15.21-15.22
7 Mfalme akaondoka katika ghadhabu yake kutoka kwenye karamu ya divai, akaingia bustani ya ngome. Hamani naye akasimama ili ajitakie maisha yake kwa malkia Esta; kwa kuwa aliona ya kwamba amekusudiwa madhara na mfalme.
Esther 1.12 Proverbes 19.12 1 Samuel 20.7 1 Samuel 25.17 Apocalypse 3.9
8 Kisha mfalme akarudi kutoka katika bustani ya ngome hata mahali pa karamu ya divai. Ikawa Hamani amejitupa chini penye kitanda alipokuwapo Esta. Mfalme akasema, Namna gani! Je! Atamfanyia malkia jeuri hata machoni pangu nyumbani mwangu? Na neno lilipotoka kinywani mwa mfalme, wakamfunika uso Hamani.
Esther 1.6 Esther 6.12 Esaïe 22.17 Job 9.24 Esaïe 49.23
9 Ndipo aliposema Harbona, msimamizi-wa-nyumba mmojawapo wa wale waliohudhuria mbele ya mfalme, Tazama, basi, mti wa mikono hamsini urefu wake, Hamani aliomwekea tayari Mordekai, ambaye alinena vema kwa ajili ya mfalme, upo umesimamishwa nyumbani kwa Hamani. Mfalme akasema, Mtundikeni juu yake.
Psaumes 7.15-7.16 Proverbes 11.5-11.6 Esther 5.14 Psaumes 35.8 Esther 1.10
10 Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.
Daniel 6.24 Psaumes 7.16 Ezéchiel 5.13 Juges 15.7 Zacharie 6.8

Cette Bible est dans le domaine public.