Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 3.28
Bible en Swahili de l’est


Reconstruction de la muraille

Répartition du travail

1 Ndipo akaondoka Eliashibu, kuhani mkuu, pamoja na nduguze makuhani, wakalijenga lango la kondoo; wakazitia boriti zake, wakaisimamisha milango yake; mpaka mnara wa Hamea wakalitakasa, mpaka mnara wa Hananeli.
Néhémie 12.39 Jérémie 31.38 Zacharie 14.10 Néhémie 3.32 Jean 5.2
2 Na baada yao wakajenga watu wa Yeriko. Na baada yao akajenga Zakuri, mwana wa Imri.
Néhémie 7.36 Esdras 2.34 Néhémie 10.12
3 Na lango la samaki wakalijenga wana wa Senaa; wakazitia boriti zake, wakaisimamisha milango yake, na vyuma vyake, na makomeo yake.
2 Chroniques 33.14 Néhémie 12.39 Sophonie 1.10 Néhémie 2.8 Néhémie 7.1
4 Na baada yao akafanyiza Meremothi, mwana wa Uria, mwana wa Hakosi. Na baada yao akafanyiza Meshulamu, mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli. Na baada yao akafanyiza Sadoki, mwana wa Baana.
Esdras 8.33 Néhémie 3.21 Néhémie 10.15 Néhémie 10.7
5 Na baada yao wakafanyiza Watekoi; lakini wakuu wao hawakutia shingo zao kazini mwa bwana wao.
2 Samuel 14.2 Néhémie 3.27 Matthieu 11.29 1 Timothée 6.17-6.18 Juges 5.23
6 Na lango la kale wakalifanyiza Yoyada, mwana wa Pasea, na Meshulamu, mwana wa Besodeya; wakazitia boriti zake, wakaisimamisha milango yake, na vyuma vyake, na makomeo yake.
Néhémie 12.39
7 Na baada yao wakafanyiza Melatia, Mgibeoni, na Yadoni, Mmeronothi, watu wa Gibeoni, na wa Mispa, raia wa kiti cha enzi cha liwali wa ng’ambo ya Mto.
2 Samuel 21.2 2 Chroniques 16.6 Néhémie 3.19 Néhémie 2.7-2.8 Josué 9.3-9.27
8 Na baada yao akafanyiza Uzieli, mwana wa Harhaya, mmoja wa mafundi wa dhahabu. Na baada yake akafanyiza Hanania, mmoja wa mafundi wa manukato, nao wakaujengea Yerusalemu buruji mpaka ule ukuta mpana.
Néhémie 12.38 Néhémie 3.31-3.32 Genèse 50.2 Ecclésiaste 10.1 Exode 30.25
9 Na baada yao akafanyiza Refaya, mwana wa Huri, akida wa nusu ya Yerusalemu.
Néhémie 3.12 Néhémie 3.17
10 Na baada yao akafanyiza Yedaya, mwana wa Harumafu, kuielekea nyumba yake. Na baada yake akafanyiza Hatushi, mwana wa Hashabneya.
Néhémie 3.28-3.30 Néhémie 10.4 Néhémie 3.23
11 Malkiya, mwana wa Harimu, na Hashubu, mwana wa Pahath-moabu, wakafanyiza sehemu nyingine, na mnara wa tanuu.
Néhémie 12.38 Esdras 2.6 Néhémie 10.14 Néhémie 7.11 Esdras 8.4
12 Na baada yake akafanyiza Shalumu, mwana wa Haloheshi, akida wa nusu ya Yerusalemu, yeye na binti zake.
Néhémie 3.9 Philippiens 4.3 Néhémie 3.14-3.18 Exode 35.25 Actes 21.8-21.9
13 Lango la bondeni wakalifanyiza Hanuni, nao wakaao Zanoa; wakalijenga, wakaisimamisha milango yake, na vyuma vyake, na makomeo yake, na huo ukuta wa dhiraa elfu mpaka lango la jaa.
Néhémie 2.13 Josué 15.34 2 Chroniques 26.9 Josué 15.56 1 Chroniques 4.18
14 Na lango la jaa akalifanyiza Malkiya, mwana wa Rekabu, akida wa mtaa wa Beth-hakeremu; akalijenga, akaisimamisha milango yake, na vyuma vyake, na makomeo yake.
Jérémie 6.1 Néhémie 2.13 Néhémie 3.12-3.13 Néhémie 3.9 Néhémie 3.15-3.18
15 Na lango la chemchemi akalifanyiza Shalumu, mwana wa Kolhoze, akida wa mtaa wa Mispa; akalijenga na kulifunika, akaisimamisha milango yake, na vyuma vyake, na makomeo yake, na huo ukuu wa birika la Shiloa karibu na bustani ya mfalme, mpaka madaraja yashukayo kutoka mji wa Daudi.
Jean 9.7 Néhémie 12.37 Luc 13.4 Néhémie 2.14 Esaïe 8.6
16 Baada yake akafanyiza Nehemia, mwana wa Azbuki, akida wa nusu ya mtaa wa Beth-suri, mpaka mahali paelekeapo makaburi ya Daudi, na mpaka birika lililofanyizwa, na mpaka nyumba ya mashujaa.
2 Rois 20.20 Actes 2.29 Néhémie 3.12 Esaïe 7.3 Josué 15.58
17 Baada yake wakafanyiza Walawi, Rehumi, mwana wa Bani. Baada yake akafanyiza Hashabia, akida wa nusu ya mtaa wa Keila, kwa mtaa wake.
Josué 15.44 1 Chroniques 23.4 Néhémie 3.16 1 Samuel 23.1-23.13
18 Baada yake wakafanyiza ndugu zao, Binui, mwana wa Henadadi, akida wa nusu ya mtaa wa Keila.
19 Na baada yake akafanyiza Ezeri, mwana wa Yeshua, akida wa Mispa, sehemu nyingine, kupaelekea penye kupanda kwa ghala ya silaha, ukuta ugeukapo.
2 Chroniques 26.9 Néhémie 12.8 Néhémie 10.9
20 Baada yake Baruki, mwana wa Zakai, akafanyiza kwa bidii sehemu nyingine, toka ugeukapo ukuta mpaka mlango wa nyumba ya Eliashibu, kuhani mkuu.
Néhémie 3.1 Ecclésiaste 9.10 Romains 12.11 Néhémie 3.21 Néhémie 13.4
21 Baada yake akafanyiza Meremothi, mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, sehemu nyingine, toka mlango wa nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.
Esdras 2.61 Néhémie 7.63
22 Na baada yake wakafanyiza makuhani, watu wa Uwandani.
Néhémie 12.28 Néhémie 6.2
23 Baada yao wakafanyiza Benyamini na Hashubu, kuielekea nyumba yao. Baada yao akafanyiza Azaria, mwana wa Maaseya, mwana wa Anania, kando ya nyumba yake.
Néhémie 8.4 Néhémie 3.29-3.30 Néhémie 3.10 Néhémie 8.7 Néhémie 10.2
24 Baada yake akafanyiza Binui, mwana wa Henadadi, sehemu nyingine, toka nyumba ya Azaria mpaka ugeukapo ukuu, na mpaka pembeni.
Néhémie 3.19 Néhémie 3.11 Néhémie 3.27 Néhémie 10.9
25 Baada yake akafanyiza Palali, mwana wa Uzai, kuelekea ugeukapo ukuta, nao mnara utokezao penye nyumba ya juu ya kifalme, iliyopo karibu na uwanda wa walinzi. Baada yake akafanyiza Pedaya, mwana wa Paroshi,
Jérémie 32.2 Jérémie 37.21 Jérémie 33.1 Néhémie 12.39 Esdras 2.3
26 (basi Wanethini hukaa Ofeli), mpaka mahali paelekeapo lango la maji kukabili mashariki, nao mnara utokezao.
Néhémie 8.1 Néhémie 11.21 Néhémie 12.37 Néhémie 8.3 2 Chroniques 27.3
27 Baada yake wakafanyiza Watekoi sehemu nyingine, kuuelekea mnara mkubwa utokezao, na mpaka ukuta wa Ofeli.
Néhémie 3.5
28 Juu ya lango la farasi wakafanyiza makuhani, kila mtu kuielekea nyumba yake. Baada yao akafanyiza Sadoki, mwana wa Imeri, kuielekea nyumba yake.
2 Chroniques 23.15 2 Rois 11.16 Jérémie 31.40 Néhémie 3.23 Néhémie 3.10
29 Na baada yake akafanyiza Shemaya, mwana wa Shekania, mlinzi wa lango la mashariki.
Esdras 10.2 Esdras 2.37 Néhémie 7.40 Jérémie 19.2
30 Baada yake wakafanyiza Hanania, mwana wa Shelemia, na Hanuni, mwana wa sita wa Salafu, sehemu nyingine. Baada yake akafanyiza Meshulamu, mwana wa Berekia, sehemu nyingine kuelekea chumba chake.
31 Baada yake akafanyiza Malkiya, mmoja wa mafundi wa dhahabu, mpaka nyumba ya Wanethini, na ya wafanya biashara, kulielekea lango la gereza, na mpaka chumba cha juu cha pembeni.
Néhémie 3.32 Néhémie 3.8
32 Na kati ya chumba cha juu cha pembeni na lango la kondoo wakafanyiza mafundi wa dhahabu na wafanya biashara.
Néhémie 3.1 Jean 5.2 Néhémie 12.39 Néhémie 3.8 Néhémie 3.31

Cette Bible est dans le domaine public.