Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 10.8
Bible en Swahili de l’est


Engagement envers la loi et le culte

1 Basi hawa ndio waliotia muhuri; Nehemia, ndiye Tirshatha, mwana wa Hakalia, na Sedekia;
Néhémie 9.38 Néhémie 8.9 Néhémie 1.1 Esdras 2.63 Néhémie 7.70
2 Seraya, Azaria, Yeremia;
Néhémie 3.23 Néhémie 12.1 Néhémie 12.33-12.34 Néhémie 11.11
3 Pashuri, Amaria, Malkiya;
Néhémie 8.4 Néhémie 12.13 Néhémie 11.12 Néhémie 3.11 Néhémie 12.2
4 Hamshi, Shekania, Maluki;
Néhémie 12.14 Néhémie 12.2 Néhémie 3.10
5 Harimu, Meremothi, Obadia;
Néhémie 3.4 Néhémie 3.21 Néhémie 3.11 Néhémie 12.3
6 Danieli, Ginethoni, Baruki;
Néhémie 12.4 Néhémie 3.20
7 Meshulamu, Abiya, Miyamini;
Néhémie 11.11 Néhémie 12.17 Néhémie 8.4 Néhémie 12.25-12.33 Néhémie 3.6
8 Maazia, Bilgai, Shemaya; hao ndio waliokuwa makuhani.
Néhémie 3.29 Néhémie 12.5-12.6 Néhémie 12.18 Esdras 10.21 Néhémie 12.42
9 Na Walawi; ndio, Yeshua, mwana wa Azania, Binui wa wana wa Henadadi, Kadmieli;
Néhémie 3.18-3.19 Néhémie 3.24 Néhémie 8.7 Néhémie 12.8 Néhémie 7.43
10 na ndugu zao, Shebania, Hodia, Kelita, Pelaya, Hanani;
Néhémie 8.7 Néhémie 9.4-9.5 Esdras 10.23
11 Mika, Rehobu, Hashabia;
Esdras 8.19 Néhémie 11.15 Néhémie 11.22 Esdras 8.24 Néhémie 12.24
12 Zakuri, Sherebia, Shebania;
Néhémie 8.7 Néhémie 9.4 Néhémie 12.8
13 Hodia, Bani, Beninu;
14 Na wakuu wa watu; Paroshi, Pahath-Moabu, Elamu, Zatu, Bani;
Néhémie 7.15 Néhémie 7.11-7.13 Néhémie 7.8 Esdras 2.3-2.70 Néhémie 3.11
15 Buni, Azgadi, Bebai;
Esdras 2.11-2.12 Néhémie 7.16-7.17 Esdras 8.11-8.12 Esdras 10.28
16 Adonikamu, Bigwai, Adini;
Esdras 8.14 Esdras 2.14-2.16 Néhémie 7.19-7.21
17 Ateri, Hezakia, Azuri;
18 Hodia, Hashumu, Besai;
Esdras 2.17-2.70 Néhémie 7.22-7.73
19 Harifu, Anathothi, Nobai;
20 Magpiashi, Meshulamu, Heziri;
21 Meshezabeli, Sadoki, Yadua;
22 Pelatia, Hanani, Anaya;
23 Hoshea, Hanania, Hashubu;
24 Haloheshi, Pilha, Shobeki;
25 Rehumu, Hashabna, Maaseya;
Néhémie 3.17-3.32
26 Ahia, Hanani, Anani;
27 Maluki, Harimu, na Baana.
28 Na watu waliosalia, makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji, Wanethini, na hao wote waliojitenga katika watu wa nchi kwa torati ya Mungu; wake zao, na wana wao, na binti zao, kila mwenye maarifa na akili;
Néhémie 9.2 Esdras 2.36-2.54 Psaumes 47.7 Néhémie 7.72-7.73 Jérémie 4.2
29 wakaambatana na ndugu zao, wakuu wao, nao wakaingia katika laana na kiapo, ya kuwa wataiendea torati ya Mungu, iliyotolewa kwa mkono wa Musa, mtumishi wa Mungu, na kuziangalia, na kuzitenda, amri zote za Bwana, Bwana wetu, na hukumu zake na sheria zake;
Psaumes 119.106 2 Chroniques 34.31 Néhémie 5.12-5.13 2 Rois 23.3 Romains 12.9
30 wala tusiwaoze watu wa nchi binti zetu, wala kuwatwalia wana wetu binti zao;
Exode 34.16 Deutéronome 7.3 Esdras 10.10-10.12 Esdras 9.12-9.14 Esdras 9.1-9.3
31 tena watu wa nchi wakitembeza biashara, au chakula cho chote, siku ya sabato, tusinunue kwao siku ya sabato, au siku takatifu; tena kwamba tuuache mwaka wa saba, na madai ya kila deni.
Exode 23.10-23.11 Néhémie 13.15-13.22 Lévitique 23.3 Exode 20.10 Lévitique 25.1-25.7
32 Tena tukajifanyia maagizo, kujitoza mwaka kwa mwaka theluthi ya shekeli kwa huduma ya nyumba ya Mungu wetu;
Exode 30.11-30.16 Genèse 28.22 Matthieu 17.24-17.27 Proverbes 3.9 2 Corinthiens 8.12
33 kwa mikate ya wonyesho, na kwa sadaka ya unga ya daima, na kwa sadaka ya kuteketezwa ya daima, ya sabato, na ya siku za mwezi mpya, na ya sikukuu, tena kwa vitu vile vitakatifu, na kwa sadaka za dhambi, za kuwafanyia Israeli upatanisho, na kwa ajili ya kazi yote ya nyumba ya Mungu wetu.
2 Chroniques 2.4 Nombres 28.1-28.29 Lévitique 24.5-24.6 2 Chroniques 24.5-24.14 Hébreux 10.11
34 Kisha tukapiga kura, makuhani, na Walawi, na watu, juu ya matoleo ya kuni, ili kuzileta nyumbani kwa Mungu wetu, kwa kadiri ya mbari za baba zetu, kwa nyakati zilizoamriwa, mwaka kwa mwaka, kukoka moto madhabahuni mwa Bwana, Mungu wetu, kama ilivyoandikwa katika torati;
Néhémie 13.31 Esaïe 40.16 Lévitique 6.12-6.13 Hébreux 10.3-10.7 Proverbes 18.18
35 tena kuleta malimbuko ya ardhi yetu, na malimbuko ya matunda yote ya miti ya namna zote, mwaka kwa mwaka, nyumbani kwa Bwana;
Deutéronome 26.2 Exode 23.19 Nombres 18.12 Exode 34.26 2 Chroniques 31.3-31.10
36 tena wazaliwa wa kwanza wa wana wetu, na wa wanyama wetu, kama ilivyoandikwa katika torati, na wazaliwa wa kwanza wa ng’ombe zetu na kondoo zetu, ili kuwaleta nyumbani mwa Mungu wetu, kwa makuhani watumikao nyumbani mwa Mungu wetu;
Exode 13.2 Lévitique 27.26-27.27 Nombres 18.9-18.19 Galates 6.6 Exode 13.12-13.15
37 tena tuyalete malimbuko ya unga wetu, na sadaka zetu za kuinuliwa, na matunda ya miti ya namna zote, mvinyo, na mafuta, kwa makuhani, hapo vyumbani kwa nyumba ya Mungu wetu; na zaka za ardhi yetu kwa Walawi; kwa kuwa hao Walawi wazitwaa zaka mijini mwote mwa kulima kwetu.
Lévitique 23.17 Nombres 18.21 Néhémie 13.9 Néhémie 13.5 Deutéronome 18.4
38 Naye kuhani, mwana wa Haruni, atakuwako pamoja na Walawi, watwaapo zaka Walawi; nao Walawi wataipandisha zaka ya hizo zaka nyumbani kwa Mungu wetu, vyumbani, katika nyumba ya hazina.
Néhémie 13.12-13.13 2 Chroniques 31.11-31.12 1 Chroniques 9.26 Nombres 18.26-18.28
39 Kwa kuwa wana wa Israeli na wana wa Lawi wataleta sadaka ya kuinuliwa ya nafaka, na mvinyo, na mafuta, vyumbani, kwa kuwa ndimo vilimo vyombo vya patakatifu, na makuhani watumikao, na mabawabu, na waimbaji; wala sisi hatutaiacha nyumba ya Mungu wetu.
2 Chroniques 31.12 Deutéronome 12.6-12.11 Nombres 18.30 Psaumes 122.9 Néhémie 13.10-13.12

Cette Bible est dans le domaine public.