Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 16
Bible en Swahili de l’est


Alliance d’Asa avec la Syrie

1 Katika mwaka wa thelathini na sita wa kutawala kwake Asa, Baasha mfalme wa Israeli akapanda juu ya Yuda, akaujenga Rama, ili asimwache mtu ye yote kutoka wala kuingia kwa Asa mfalme wa Yuda.
2 Chroniques 15.9 2 Chroniques 15.5 1 Rois 12.27 1 Rois 15.16-15.22 2 Chroniques 11.13-11.17
2 Ndipo Asa akatoa fedha na dhahabu katika hazina za nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme, akampelekea Ben-hadadi mfalme wa Shamu, aliyekaa Dameski, akasema,
2 Rois 16.8 2 Chroniques 28.21 2 Rois 18.15 2 Rois 12.18
3 Kwangu na kwako na liwe agano kama lilivyokuwa kwa baba yangu na baba yako; angalia, nimekuletea fedha na dhahabu; basi, uvunje agano lako na Baasha, mfalme wa Israeli, ili aniondokee mimi.
2 Chroniques 18.3 2 Corinthiens 6.16 2 Chroniques 19.2 Exode 32.21 2 Samuel 21.2
4 Naye Ben-hadadi akamsikiliza mfalme Asa, akawapeleka maakida wa majeshi yake juu ya miji ya Israeli; wakapiga Iyoni, na Dani, na Abel-maimu, na miji ya hazina yote ya Naftali.
Genèse 14.14 2 Pierre 2.15 Exode 1.11 1 Rois 15.20 1 Timothée 6.10
5 Ikawa Baasha aliposikia habari hiyo, akaacha kuujenga Rama, akaikomesha kazi yake.
6 Ndipo mfalme Asa akawatwaa Yuda wote; nao wakayachukua mawe ya Rama, na miti yake, aliyoijengea Baasha; naye akajenga kwa vitu hivyo Geba na Mispa.
1 Samuel 10.17 1 Chroniques 6.60 1 Samuel 7.6 1 Rois 15.22 1 Samuel 7.16
7 Wakati ule Hanani mwonaji akamwendea Asa mfalme wa Yuda, akamwambia, Kwa kuwa umemtegemea mfalme wa Shamu, wala hukumtegemea Bwana, Mungu wako, kwa hiyo limeokoka jeshi la mfalme wa Shamu mkononi mwako.
1 Rois 16.1 2 Chroniques 19.2 Esaïe 31.1 2 Chroniques 32.7-32.8 Ephésiens 1.12-1.13
8 Je! Hao Wakushi na Walubi hawakuwa jeshi kubwa mno, wenye magari na wapanda farasi wengi sana? Lakini, kwa kuwa ulimtegemea Bwana, aliwatia mkononi mwako.
2 Chroniques 12.3 2 Chroniques 13.16 2 Chroniques 13.18 2 Chroniques 14.9-14.12 Psaumes 37.39-37.40
9 Kwa maana macho ya Bwana hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake. Kwa hayo umetenda upumbavu; kwani tangu sasa utakuwa na vita.
Zacharie 4.10 Proverbes 15.3 Jérémie 16.17 Proverbes 5.21 1 Pierre 3.12
10 Ndipo Asa akamkasirikia mwonaji, akamtia nyumbani mwa mkatale; maana amemghadhibikia kwa sababu ya neno hilo. Na Asa akawaonea baadhi ya watu wakati ule ule.
2 Chroniques 18.26 Actes 16.23-16.24 Job 20.19 Luc 3.20 2 Samuel 12.13
11 Na tazama, mambo yake Asa, ya kwanza na ya mwisho, angalia, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
2 Chroniques 20.34 2 Chroniques 25.26 1 Rois 15.23-15.24 2 Chroniques 9.29 2 Chroniques 32.32
12 Akashikwa Asa na ugonjwa wa miguu katika mwaka wa thelathini na kenda wa kumiliki kwake; ugonjwa wake ukazidi sana; lakini hakumtafuta Bwana katika ugonjwa wake, bali waganga.
Jérémie 17.5 2 Chroniques 28.22 Marc 5.26 Matthieu 9.12 1 Chroniques 10.14
13 Asa akalala na babaze, akafa katika mwaka wa arobaini na mmoja wa kumiliki kwake.
1 Rois 15.24
14 Wakamzika katika makaburi yake mwenyewe, aliyojichimbia katika mji wa Daudi, wakamlaza juu ya kitanda kilichojazwa manukato, na kila namna ya machanganyiko ya hao mafundi wa dawa; wakamfukizia mafukizo makuu sana.
Genèse 50.2 2 Chroniques 21.19 Jérémie 34.5 Marc 16.1 2 Chroniques 35.24

Cette Bible est dans le domaine public.