Règne d’Abija
 1 Katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu, akaanza Abiya kutawala juu ya Yuda.
2 Chroniques 12.16  1 Rois 15.1-15.8  
 2 Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Maaka binti Urieli wa Gibea. Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
2 Chroniques 11.20  1 Rois 15.6-15.7  1 Rois 15.2  Josué 18.28  Juges 19.14  
 3 Abiya akapanga vita mwenye jeshi la watu hodari wa vita, watu wateule mia nne elfu; naye Yeroboamu akapanga vita juu yake mwenye watu wateule mia nane elfu, waliokuwa waume mashujaa.
1 Chroniques 21.5  2 Chroniques 26.12-26.13  2 Chroniques 14.8-14.9  2 Chroniques 11.1  2 Chroniques 17.14-17.18  
 4 Basi Abiya akasimama juu ya kilima cha Semaraimu, kilichoko milimani mwa Efraimu, akasema, Nisikieni, enyi Yeroboamu na Israeli wote;Josué 18.22  Genèse 10.18  2 Chroniques 15.2  Juges 9.7  
 5 je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?
Nombres 18.19  Lévitique 2.13  2 Samuel 7.12-7.16  Marc 9.49-9.50  Juges 11.21-11.24  
 6 Lakini Yeroboamu mwana wa Nebati, mtumwa wa Sulemani mwana wa Daudi, akainuka, akamfanyia fitina bwana wake.
1 Rois 11.26  1 Rois 12.20  2 Chroniques 10.19  1 Rois 12.27  
 7 Wakamkusanyikia watu mabaradhuli, wasiofaa kitu, waliojitia nguvu juu ya Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana na wa moyo mwororo, asiweze kuwazuia.
2 Chroniques 12.13  Juges 9.4  1 Rois 21.10  1 Samuel 22.2  1 Corinthiens 14.20  
 8 Hata sasa mwajidhania kuwa mtauzuia ufalme wa Bwana mikononi mwa wana wa Daudi; nanyi mmekuwa jamii kubwa, na kwenu mna ndama za dhahabu alizowafanyia Yeroboamu kuwa miungu.
1 Rois 12.28  2 Chroniques 11.15  2 Chroniques 20.12  Luc 19.27  1 Rois 14.9  
 9 Je! Hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Haruni, na Walawi; mkajifanyia makuhani kama wafanyavyo watu wa nchi nyingine? Hata ye yote ajaye kujifanya wakfu na ndama, na kondoo waume saba, aweza kuwa kuhani wa hiyo isiyo miungu.
2 Chroniques 11.14-11.15  Jérémie 2.11  Exode 29.35  Lévitique 16.32  1 Rois 13.33  
 10 Lakini sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala sisi hatukumwacha; tena tunao makuhani wanaomtumikia Bwana, wana wa Haruni, na Walawi, kwa kazi yao;
Nombres 18.1-18.7  2 Chroniques 11.16-11.17  Exode 19.5-19.6  Zacharie 13.9  Nombres 16.40  
 11 nao humtolea Bwana kila asubuhi, na kila jioni, sadaka za kuteketezwa na fukizo la manukato; mikate ya wonyesho pia huiweka kwa taratibu yake juu ya meza takatifu, na kinara cha dhahabu chenye taa zake, kuwaka kila jioni; kwa maana sisi twayalinda malinzi ya Bwana, Mungu wetu; bali ninyi mmemwacha.
2 Chroniques 2.4  Lévitique 24.2-24.9  Exode 27.20-27.21  Exode 29.38  Exode 25.30-25.39  
 12 Na tazama, Mungu yu pamoja nasi atutangulie, na makuhani wake wenye mapanda, ili wapige sauti ya kugutusha juu yenu. Enyi wana wa Israeli, msipigane na Bwana, Mungu wa baba zenu; kwani hamtafanikiwa.
Actes 5.39  Nombres 10.8-10.9  Zacharie 10.5  Romains 8.31  Deutéronome 28.29  
 13 Lakini Yeroboamu aliwazungushia waviziao kwa nyuma; basi wao wakawa mbele ya Yuda, na wale waviziao nyuma yao.
Josué 8.9  Josué 8.4  Proverbes 21.30  Jérémie 4.22  2 Chroniques 20.22  
 14 Na Yuda walipotazama nyuma, angalia, vita vikawa mbele na nyuma; wakamlilia Bwana, na makuhani wakapiga mapanda.
2 Chroniques 14.11  Psaumes 91.5  Juges 20.33-20.43  2 Samuel 10.8-10.14  Exode 14.10  
 15 Ndipo wakapiga kelele watu wa Yuda; ikawa, watu na Yuda walipopiga kelele, Mungu akampiga Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Abiya na Yuda.
2 Chroniques 14.12  Josué 6.20  2 Rois 5.1  Psaumes 47.5  Josué 6.16  
 16 Wana wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda; naye Mungu akawaua mikononi mwao.
2 Chroniques 16.8  Juges 11.21  Josué 10.12  1 Samuel 23.7  Deutéronome 3.3  
 17 Abiya na watu wake wakawapiga mapigo makuu; hata wakaanguka wameuawa wa Israeli mia tano elfu, watu wateule.
2 Chroniques 28.6  Esaïe 37.36  2 Chroniques 13.12  2 Chroniques 13.3  1 Corinthiens 10.22  
 18 Ndivyo walivyotiishwa wana wa Israeli wakati ule, wakashinda wana wa Yuda, kwa kuwa walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
2 Chroniques 14.11  1 Chroniques 5.20  Psaumes 22.4-22.5  2 Rois 18.5  Psaumes 146.5  
 19 Abiya akamfuata Yeroboamu, akamnyang’anya miji, Betheli na miji yake, na Yeshana na miji yake, na Efroni na miji yake.
Josué 15.9  2 Chroniques 15.8  Josué 11.12  Josué 10.19  Jean 11.54  
 20 Wala Yeroboamu hakupata nguvu tena siku za Abiya; kisha Bwana akampiga, akafa.
1 Samuel 25.38  1 Rois 14.20  1 Rois 15.9  Actes 12.23  Psaumes 18.37-18.38  
 21 Ila Abiya akapata nguvu, akaoa wake kumi na wanne, akazaa wana ishirini na wawili, na binti kumi na sita.
Juges 8.30-8.31  2 Chroniques 11.21  Juges 10.4  Juges 9.5  2 Samuel 5.12-5.13  
 22 Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
2 Chroniques 9.29  2 Chroniques 12.15  2 Chroniques 24.27