Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 13.11
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Abija

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu, akaanza Abiya kutawala juu ya Yuda.
2 Chroniques 12.16 1 Rois 15.1-15.8
2 Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Maaka binti Urieli wa Gibea. Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
2 Chroniques 11.20 1 Rois 15.6-15.7 1 Rois 15.2 Josué 18.28 Juges 19.14
3 Abiya akapanga vita mwenye jeshi la watu hodari wa vita, watu wateule mia nne elfu; naye Yeroboamu akapanga vita juu yake mwenye watu wateule mia nane elfu, waliokuwa waume mashujaa.
1 Chroniques 21.5 2 Chroniques 26.12-26.13 2 Chroniques 14.8-14.9 2 Chroniques 11.1 2 Chroniques 17.14-17.18
4 Basi Abiya akasimama juu ya kilima cha Semaraimu, kilichoko milimani mwa Efraimu, akasema, Nisikieni, enyi Yeroboamu na Israeli wote;
Josué 18.22 Genèse 10.18 2 Chroniques 15.2 Juges 9.7
5 je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?
Nombres 18.19 Lévitique 2.13 2 Samuel 7.12-7.16 Marc 9.49-9.50 Juges 11.21-11.24
6 Lakini Yeroboamu mwana wa Nebati, mtumwa wa Sulemani mwana wa Daudi, akainuka, akamfanyia fitina bwana wake.
1 Rois 11.26 1 Rois 12.20 2 Chroniques 10.19 1 Rois 12.27
7 Wakamkusanyikia watu mabaradhuli, wasiofaa kitu, waliojitia nguvu juu ya Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana na wa moyo mwororo, asiweze kuwazuia.
2 Chroniques 12.13 Juges 9.4 1 Rois 21.10 1 Samuel 22.2 1 Corinthiens 14.20
8 Hata sasa mwajidhania kuwa mtauzuia ufalme wa Bwana mikononi mwa wana wa Daudi; nanyi mmekuwa jamii kubwa, na kwenu mna ndama za dhahabu alizowafanyia Yeroboamu kuwa miungu.
1 Rois 12.28 2 Chroniques 11.15 2 Chroniques 20.12 Luc 19.27 1 Rois 14.9
9 Je! Hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Haruni, na Walawi; mkajifanyia makuhani kama wafanyavyo watu wa nchi nyingine? Hata ye yote ajaye kujifanya wakfu na ndama, na kondoo waume saba, aweza kuwa kuhani wa hiyo isiyo miungu.
2 Chroniques 11.14-11.15 Jérémie 2.11 Exode 29.35 Lévitique 16.32 1 Rois 13.33
10 Lakini sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala sisi hatukumwacha; tena tunao makuhani wanaomtumikia Bwana, wana wa Haruni, na Walawi, kwa kazi yao;
Nombres 18.1-18.7 2 Chroniques 11.16-11.17 Exode 19.5-19.6 Zacharie 13.9 Nombres 16.40
11 nao humtolea Bwana kila asubuhi, na kila jioni, sadaka za kuteketezwa na fukizo la manukato; mikate ya wonyesho pia huiweka kwa taratibu yake juu ya meza takatifu, na kinara cha dhahabu chenye taa zake, kuwaka kila jioni; kwa maana sisi twayalinda malinzi ya Bwana, Mungu wetu; bali ninyi mmemwacha.
2 Chroniques 2.4 Lévitique 24.2-24.9 Exode 27.20-27.21 Exode 29.38 Exode 25.30-25.39
12 Na tazama, Mungu yu pamoja nasi atutangulie, na makuhani wake wenye mapanda, ili wapige sauti ya kugutusha juu yenu. Enyi wana wa Israeli, msipigane na Bwana, Mungu wa baba zenu; kwani hamtafanikiwa.
Actes 5.39 Nombres 10.8-10.9 Zacharie 10.5 Romains 8.31 Deutéronome 28.29
13 Lakini Yeroboamu aliwazungushia waviziao kwa nyuma; basi wao wakawa mbele ya Yuda, na wale waviziao nyuma yao.
Josué 8.9 Josué 8.4 Proverbes 21.30 Jérémie 4.22 2 Chroniques 20.22
14 Na Yuda walipotazama nyuma, angalia, vita vikawa mbele na nyuma; wakamlilia Bwana, na makuhani wakapiga mapanda.
2 Chroniques 14.11 Psaumes 91.5 Juges 20.33-20.43 2 Samuel 10.8-10.14 Exode 14.10
15 Ndipo wakapiga kelele watu wa Yuda; ikawa, watu na Yuda walipopiga kelele, Mungu akampiga Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Abiya na Yuda.
2 Chroniques 14.12 Josué 6.20 2 Rois 5.1 Psaumes 47.5 Josué 6.16
16 Wana wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda; naye Mungu akawaua mikononi mwao.
2 Chroniques 16.8 Juges 11.21 Josué 10.12 1 Samuel 23.7 Deutéronome 3.3
17 Abiya na watu wake wakawapiga mapigo makuu; hata wakaanguka wameuawa wa Israeli mia tano elfu, watu wateule.
2 Chroniques 28.6 Esaïe 37.36 2 Chroniques 13.12 2 Chroniques 13.3 1 Corinthiens 10.22
18 Ndivyo walivyotiishwa wana wa Israeli wakati ule, wakashinda wana wa Yuda, kwa kuwa walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
2 Chroniques 14.11 1 Chroniques 5.20 Psaumes 22.4-22.5 2 Rois 18.5 Psaumes 146.5
19 Abiya akamfuata Yeroboamu, akamnyang’anya miji, Betheli na miji yake, na Yeshana na miji yake, na Efroni na miji yake.
Josué 15.9 2 Chroniques 15.8 Josué 11.12 Josué 10.19 Jean 11.54
20 Wala Yeroboamu hakupata nguvu tena siku za Abiya; kisha Bwana akampiga, akafa.
1 Samuel 25.38 1 Rois 14.20 1 Rois 15.9 Actes 12.23 Psaumes 18.37-18.38
21 Ila Abiya akapata nguvu, akaoa wake kumi na wanne, akazaa wana ishirini na wawili, na binti kumi na sita.
Juges 8.30-8.31 2 Chroniques 11.21 Juges 10.4 Juges 9.5 2 Samuel 5.12-5.13
22 Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
2 Chroniques 9.29 2 Chroniques 12.15 2 Chroniques 24.27

Cette Bible est dans le domaine public.