Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 13.10
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Abija

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu, akaanza Abiya kutawala juu ya Yuda.
2 Chroniques 12.16 1 Rois 15.1-15.8
2 Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Maaka binti Urieli wa Gibea. Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
2 Chroniques 11.20 1 Rois 15.6-15.7 Josué 18.28 Juges 19.14 1 Samuel 10.26
3 Abiya akapanga vita mwenye jeshi la watu hodari wa vita, watu wateule mia nne elfu; naye Yeroboamu akapanga vita juu yake mwenye watu wateule mia nane elfu, waliokuwa waume mashujaa.
2 Chroniques 26.12-26.13 2 Chroniques 14.8-14.9 2 Chroniques 11.1 2 Chroniques 17.14-17.18 1 Samuel 17.1-17.3
4 Basi Abiya akasimama juu ya kilima cha Semaraimu, kilichoko milimani mwa Efraimu, akasema, Nisikieni, enyi Yeroboamu na Israeli wote;
Josué 18.22 2 Chroniques 15.2 Juges 9.7 Genèse 10.18
5 je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?
Nombres 18.19 Lévitique 2.13 2 Samuel 7.12-7.16 Marc 9.49-9.50 Psaumes 89.19-89.37
6 Lakini Yeroboamu mwana wa Nebati, mtumwa wa Sulemani mwana wa Daudi, akainuka, akamfanyia fitina bwana wake.
1 Rois 11.26 1 Rois 12.20 1 Rois 12.27 2 Chroniques 10.19
7 Wakamkusanyikia watu mabaradhuli, wasiofaa kitu, waliojitia nguvu juu ya Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana na wa moyo mwororo, asiweze kuwazuia.
Juges 9.4 2 Chroniques 12.13 Deutéronome 13.13 Job 30.8 Hébreux 5.12
8 Hata sasa mwajidhania kuwa mtauzuia ufalme wa Bwana mikononi mwa wana wa Daudi; nanyi mmekuwa jamii kubwa, na kwenu mna ndama za dhahabu alizowafanyia Yeroboamu kuwa miungu.
1 Rois 12.28 2 Chroniques 11.15 Psaumes 2.1-2.6 2 Chroniques 9.8 Osée 8.5-8.6
9 Je! Hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Haruni, na Walawi; mkajifanyia makuhani kama wafanyavyo watu wa nchi nyingine? Hata ye yote ajaye kujifanya wakfu na ndama, na kondoo waume saba, aweza kuwa kuhani wa hiyo isiyo miungu.
2 Chroniques 11.14-11.15 Jérémie 2.11 Exode 29.35 1 Chroniques 29.5 Actes 19.26
10 Lakini sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala sisi hatukumwacha; tena tunao makuhani wanaomtumikia Bwana, wana wa Haruni, na Walawi, kwa kazi yao;
2 Chroniques 11.16-11.17 Exode 19.5-19.6 Zacharie 13.9 Nombres 16.40 Exode 29.1-29.37
11 nao humtolea Bwana kila asubuhi, na kila jioni, sadaka za kuteketezwa na fukizo la manukato; mikate ya wonyesho pia huiweka kwa taratibu yake juu ya meza takatifu, na kinara cha dhahabu chenye taa zake, kuwaka kila jioni; kwa maana sisi twayalinda malinzi ya Bwana, Mungu wetu; bali ninyi mmemwacha.
2 Chroniques 2.4 Lévitique 24.2-24.9 Exode 29.38 Exode 25.30-25.39 Exode 27.20-27.21
12 Na tazama, Mungu yu pamoja nasi atutangulie, na makuhani wake wenye mapanda, ili wapige sauti ya kugutusha juu yenu. Enyi wana wa Israeli, msipigane na Bwana, Mungu wa baba zenu; kwani hamtafanikiwa.
Nombres 10.8-10.9 Actes 5.39 Zacharie 10.5 Josué 6.13-6.20 Psaumes 20.7
13 Lakini Yeroboamu aliwazungushia waviziao kwa nyuma; basi wao wakawa mbele ya Yuda, na wale waviziao nyuma yao.
Josué 8.9 Josué 8.4 Jérémie 4.22 2 Chroniques 20.22 Proverbes 21.30
14 Na Yuda walipotazama nyuma, angalia, vita vikawa mbele na nyuma; wakamlilia Bwana, na makuhani wakapiga mapanda.
2 Chroniques 14.11 Juges 20.33-20.43 2 Samuel 10.8-10.14 Exode 14.10 Josué 8.20
15 Ndipo wakapiga kelele watu wa Yuda; ikawa, watu na Yuda walipopiga kelele, Mungu akampiga Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Abiya na Yuda.
2 Chroniques 14.12 Psaumes 118.4-118.7 Juges 4.15 2 Chroniques 20.21 Nombres 32.4
16 Wana wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda; naye Mungu akawaua mikononi mwao.
2 Chroniques 16.8 1 Samuel 23.7 Deutéronome 3.3 Josué 21.44 Genèse 14.20
17 Abiya na watu wake wakawapiga mapigo makuu; hata wakaanguka wameuawa wa Israeli mia tano elfu, watu wateule.
Esaïe 37.36 2 Chroniques 13.12 2 Chroniques 13.3 1 Corinthiens 10.22 Nahum 1.5
18 Ndivyo walivyotiishwa wana wa Israeli wakati ule, wakashinda wana wa Yuda, kwa kuwa walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
2 Chroniques 14.11 1 Chroniques 5.20 Daniel 3.28 2 Chroniques 16.8-16.9 2 Chroniques 20.20
19 Abiya akamfuata Yeroboamu, akamnyang’anya miji, Betheli na miji yake, na Yeshana na miji yake, na Efroni na miji yake.
2 Chroniques 15.8 Josué 15.9 Josué 11.12 Josué 10.19 Jean 11.54
20 Wala Yeroboamu hakupata nguvu tena siku za Abiya; kisha Bwana akampiga, akafa.
1 Samuel 25.38 1 Rois 14.20 Actes 12.23 Psaumes 18.37-18.38 1 Samuel 26.10
21 Ila Abiya akapata nguvu, akaoa wake kumi na wanne, akazaa wana ishirini na wawili, na binti kumi na sita.
2 Chroniques 11.21 Juges 10.4 Juges 9.5 2 Samuel 5.12-5.13 Juges 8.30-8.31
22 Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
2 Chroniques 9.29 2 Chroniques 12.15 2 Chroniques 24.27

Cette Bible est dans le domaine public.