Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 6.24
Bible en Swahili de l’est


1 Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.
Genèse 46.11 Exode 6.16 Nombres 26.57 1 Chroniques 23.6 1 Chroniques 6.16
2 Na wana wa Kohathi; Amramu, na Ishari, na Hebroni, na Uzieli.
Exode 6.18 1 Chroniques 23.12 Exode 6.21-6.24
3 Na wana wa Amramu; Haruni, na Musa, na Miriamu. Na wana wa Haruni; Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari.
Lévitique 10.1 Exode 6.20 Lévitique 10.12 Exode 15.20 1 Chroniques 23.13
4 Eleazari akamzaa Finehasi; na Finehasi akamzaa Abishua;
Esdras 7.1-7.5 1 Chroniques 6.50 Exode 6.25 Psaumes 106.30-106.31 Nombres 25.13
5 na Abishua akamzaa Buki; na Buki akamzaa Uzi;
6 na Uzi akamzaa Zerahia; na Zerahia akamzaa Merayothi,
7 na Merayothi akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;
8 na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Ahimaasi;
2 Samuel 8.17 2 Samuel 15.27 2 Samuel 15.35-15.36 2 Samuel 20.25 1 Rois 1.34
9 na Ahimaasi akamzaa Azaria; na Azaria akamzaa Yohana;
10 na Yohana akamzaa Azaria (ndiye huyo aliyefanya kazi ya ukuhani katika nyumba aliyoijenga Sulemani huko Yerusalemu)
2 Chroniques 3.4 1 Rois 6.1-6.7 2 Chroniques 3.1 2 Chroniques 26.17-26.20
11 na Azaria akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;
Esdras 7.3
12 na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Meshulamu;
Néhémie 11.11 1 Chroniques 9.11
13 na Meshulamu akamzaa Hilkia; na Hilkia akamzaa Azaria;
2 Rois 22.12-22.14 2 Chroniques 35.8 2 Rois 22.4 2 Chroniques 34.14-34.20
14 na Azaria akamzaa Seraya; na Seraya akamzaa Yehosadaki;
2 Rois 25.18 Néhémie 11.11 Esdras 7.1 Zacharie 6.11
15 na Yehosadaki akachukuliwa mateka, hapo Bwana alipowachukua mateka Yuda na Yerusalemu, kwa mkono wa Nebukadreza.
2 Rois 25.18 Aggée 1.14 Aggée 2.2 2 Rois 25.21 Aggée 1.1
16 Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.
Exode 6.16 1 Chroniques 6.1
17 Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni; Libni, na Shimei.
1 Chroniques 23.7 Exode 6.17 Nombres 3.21 Nombres 3.18
18 Na wana wa Kohathi walikuwa Amramu, na Ishari, na Hebroni, na Uzieli.
1 Chroniques 23.12 1 Chroniques 6.2-6.3
19 Wana wa Merari; Mali, na Mushi. Na hizi ndizo jamaa za Walawi, sawasawa na mbari za baba zao.
1 Chroniques 23.21 1 Chroniques 24.26 Nombres 3.20 Exode 6.19 Nombres 26.57-26.58
20 Wa Gershoni; mwanawe huyo ni Libni, na mwanawe huyo ni Yahathi, na mwanawe huyo ni Zima;
1 Chroniques 6.43
21 na mwanawe huyo ni Yoa, na mwanawe huyo ni Ido, na mwanawe huyo ni Zera, na mwanawe huyo ni Yeatherai.
22 Wana wa Kohathi; mwanawe huyo ni Ishari, na mwanawe huyo ni Kora, na mwanawe huyo ni Asiri;
Exode 6.24 1 Chroniques 6.18 Exode 6.21 1 Chroniques 6.2
23 na mwanawe huyo ni Elkana, na mwanawe huyo ni Ebiasafu, na mwanawe huyo ni Asiri;
24 na mwanawe huyo ni Tahathi, na mwanawe huyo ni Urieli, na mwanawe huyo ni Uzia, na mwanawe huyo ni Shauli.
25 Na wana wa Elkana; Amasai, na Ahimothi.
Exode 6.24 1 Chroniques 6.35-6.36
26 Kwa habari za Elkana; wana wa Elkana; mwanawe huyo ni Sufu, na mwanawe huyo ni Tohu;
1 Samuel 1.1 1 Chroniques 6.35
27 na mwanawe huyo ni Elihu, na mwanawe huyo ni Yerohamu, na mwanawe huyo ni Elkana.
1 Samuel 1.1 1 Samuel 1.19-1.20
28 Na wana wa Samweli; Yoeli, mzaliwa wa kwanza, na wa pili Abia.
1 Chroniques 6.33 1 Samuel 8.2
29 Wana wa Merari; Mali, na mwanawe huyo ni Libni, na mwanawe huyo ni Shimei, na mwanawe huyo ni Uza;
1 Chroniques 6.19 Nombres 3.33
30 na mwanawe huyo ni Shimea, na mwanawe huyo ni Hagla, na mwanawe huyo ni Asaya.
31 Na hawa ndio watu aliowaweka Daudi juu ya kazi ya kuimba katika nyumba ya Bwana, sanduku lile lilipokwisha pata mahali pa kustarehe.
2 Samuel 6.17 1 Chroniques 15.16-15.22 Psaumes 132.14 1 Chroniques 15.25-16.1 Psaumes 132.8
32 Nao wakafanya kazi yao ya kuimba mbele ya maskani ya hema ya kukutania, hata Sulemani alipokuwa amejenga ile nyumba ya Bwana huko Yerusalemu; pia wakaisimamia huduma yao sawasawa na zamu zao.
2 Chroniques 31.2 Néhémie 12.45-12.47 1 Chroniques 16.37-16.42 2 Chroniques 29.25-29.30 1 Chroniques 9.33
33 Na hawa ndio waliofanya huduma pamoja na wana wao. Katika wana wa Wakohathi; Hemani mwimbaji, mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli;
1 Chroniques 6.28 1 Chroniques 15.17 1 Chroniques 16.41-16.42 2 Chroniques 29.14 Psaumes 88.1
34 mwana wa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu, mwana wa Tohu;
35 mwana wa Sufu, mwana wa Elkana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai;
36 mwana wa Elkana, mwana wa Shauli, mwana wa Uzia, mwana wa Urieli;
37 mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora;
Nombres 16.1-16.35 Psaumes 44.1 Psaumes 42.1 Nombres 26.10-26.11 Psaumes 84.1
38 mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli.
Nombres 3.19 1 Chroniques 16.1

Villes des prêtres et des Lévites

39 Na nduguye Asafu, aliyesimama upande wake wa kuume, huyo Asafu alikuwa mwana wa Berekia, mwana wa Shimea;
2 Chroniques 29.13 Néhémie 11.17 2 Chroniques 5.12 Néhémie 7.44 Esdras 2.41
40 mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya;
41 mwana wa Yeatherai, mwana wa Zera, mwana wa Ido;
42 mwana wa Yoa, mwana wa Zima, mwana wa Shimei;
43 mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
1 Chroniques 6.16-6.17 Exode 2.22 1 Chroniques 6.1 Nombres 3.17 Genèse 46.11
44 Na upande wa kushoto ndugu zao, wana wa Merari; Ethani, mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki;
1 Chroniques 25.6 Psaumes 89.1 1 Chroniques 25.3 1 Chroniques 25.1 1 Chroniques 15.17
45 mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia;
46 mwana wa Amzi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri;
47 mwana wa Mali, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
Nombres 7.8 Nombres 3.33-3.36 Josué 21.7 Nombres 3.20 Nombres 4.42
48 Na ndugu zao, Walawi, ndio waliowekwa ili kufanya huduma yote ya maskani ya nyumba ya Mungu.
Nombres 8.5-8.26 Nombres 3.1-3.4 1 Chroniques 23.2 1 Chroniques 25.1-25.26 Nombres 18.1-18.32
49 Lakini Haruni na wanawe ndio waliokuwa wakitoa sadaka juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na juu ya madhabahu ya kufukizia uvumba, kwa ajili ya kazi yote ya Patakatifu pa Patakatifu, ili kufanya upatanisho kwa Israeli, sawasawa na yote aliyokuwa ameyaamuru Musa, mtumishi wa Mungu.
Exode 27.1-27.8 Exode 30.1-30.7 Lévitique 4.20 Exode 30.10-30.16 Exode 29.36-29.37
50 Na hawa ndio wana wa Haruni; mwanawe huyo ni Eleazari, na mwanawe huyo ni Finehasi, na mwanawe huyo ni Abishua;
Esdras 8.33 Lévitique 10.16 Nombres 20.26-20.28 Nombres 3.4 Exode 28.1
51 na mwanawe huyo ni Buki, na mwanawe huyo ni Uzi, na mwanawe huyo ni Serahia;
52 na mwanawe huyo ni Merayothi, na mwanawe huyo ni Amaria, na mwanawe huyo Ahitubu;
53 na mwanawe huyo ni Sadoki, na mwanawe huyo ni Ahimaasi.
2 Samuel 8.17 2 Samuel 15.24-15.27 1 Samuel 2.35 1 Chroniques 12.28 1 Rois 2.35
54 Basi haya ndiyo makao yao, sawasawa na marago yao mipakani mwao; wana wa Haruni, katika jamaa za Wakohathi; kwani walikuwa na kura ya kwanza;
Genèse 25.16 Nombres 35.1-35.8 Josué 21.3-21.8 Nombres 31.10 Josué 21.10
55 wakapewa Hebroni, katika nchi ya Yuda, na vijiji vyake vilivyouzunguka;
Josué 14.13 Josué 15.13 Juges 1.20 Josué 21.11-21.13
56 bali mashamba ya mji huo, na vijiji vyake, alipewa Kalebu, mwana wa Yefune.
Josué 15.13 Josué 14.13
57 Na wana wa Haruni wakapewa miji ile ya kukimbilia, nayo ni Hebroni, tena Libna pamoja na viunga vyake, na Yatiri, na Eshtemoa pamoja na viunga vyake;
Josué 21.13-21.14 Josué 15.48 Josué 21.19 1 Chroniques 4.17 Nombres 35.13-35.15
58 na Holoni pamoja na viunga vyake, na Debiri pamoja na viunga vyake;
Josué 10.3 Josué 15.49 Josué 21.15 Josué 15.51 Josué 10.38
59 na Ashani pamoja na viunga vyake, na Beth-shemeshi pamoja na viunga vyake;
Josué 21.16 Josué 15.42 Jérémie 43.13 1 Chroniques 4.32 Josué 15.10
60 tena katika kabila ya Benyamini; Geba pamoja na viunga vyake, na Alemethi pamoja na viunga vyake, na Anathothi pamoja na viunga vyake. Miji yao yote katika jamaa zao ilikuwa miji kumi na mitatu.
Jérémie 1.1 Esaïe 10.30 Josué 18.24 1 Rois 2.26 1 Chroniques 8.6
61 Nao waliobaki wa wana wa Kohathi walipewa kwa kura miji kumi, katika jamaa ya kabila hiyo, yaani, nusu-kabila, nusu ya Manase.
1 Chroniques 6.18 1 Chroniques 6.1-6.2 1 Chroniques 6.66-6.70 1 Chroniques 6.33 Josué 21.20-21.26
62 Na wana wa Gershoni walipewa kwa kura miji kumi na mitatu, sawasawa na jamaa zao, katika kabila ya Isakari, na katika kabila ya Asheri, na katika kabila ya Naftali, na katika kabila ya Manase waliokaa Bashani.
Exode 2.22 1 Chroniques 6.71-6.76 Josué 21.27-21.33
63 Na wana wa Merari walipewa kwa kura miji kumi na miwili, sawasawa na jamaa zao, katika kabila ya Reubeni, na katika kabila ya Gadi, na katika kabila ya Zabuloni.
Josué 21.7 Josué 21.34-21.40 1 Chroniques 6.77-6.81 Genèse 46.11 Nombres 3.20
64 Na wana wa Israeli waliwapa Walawi miji hiyo pamoja na viunga vyake.
Josué 21.41-21.42 Josué 21.3 Nombres 35.1-35.8
65 Tena wakawapa kwa kura miji hiyo iliyotajwa majina yake, katika kabila ya wana wa Yuda, na katika kabila ya wana wa Simeoni, na katika kabila ya wana wa Benyamini.
1 Chroniques 6.57-6.60
66 Na jamaa nyingine za wana wa Kohathi walikuwa na miji ya mipakani mwao katika kabila ya Efraimu.
Josué 21.20-21.26
67 Basi wakapewa miji ya kukimbilia, yaani, Shekemu pamoja na viunga vyake katika nchi ya milima milima ya Efraimu; na Gezeri pamoja na viunga vyake;
Josué 21.21 Genèse 33.18 Josué 16.3 Genèse 35.4 1 Rois 9.16
68 na Yokmeamu pamoja na viunga vyake, na Beth-horoni pamoja na viunga vyake;
Josué 16.5 1 Rois 4.12 1 Samuel 13.18 Josué 10.11 Josué 21.22
69 na Aiyaloni pamoja na viunga vyake, na Gath-rimoni pamoja na viunga vyake;
Josué 10.12 Josué 21.24-21.25
70 na katika nusu-kabila ya Manase; Taanaki pamoja na viunga vyake, na Ibleamu pamoja na viunga vyake; kwa mabaki ya jamaa ya wana wa Kohathi.
Josué 17.11 Josué 21.25
71 Na wana wa Gershoni wakapewa, katika jamaa ya nusu-kabila ya Manase; Golani katika Bashani pamoja na viunga vyake, na Ashtarothi pamoja na viunga vyake;
Josué 21.27 Josué 9.10 Josué 20.8 Deutéronome 1.4 Deutéronome 4.43
72 na katika kabila ya Isakari; Kishioni pamoja na viunga vyake, na Daberathi pamoja na viunga vyake;
Josué 21.28-21.29 Juges 4.9 Josué 21.32 Josué 19.37
73 na Remethi pamoja na viunga vyake, na En-gaminu pamoja na viunga vyake;
74 na katika kabila ya Asheri; Mishali pamoja na viunga vyake, na Abdoni pamoja na viunga vyake;
Josué 21.30 Josué 19.26
75 na Helkathi pamoja na viunga vyake, na Rehobu pamoja na viunga vyake;
Josué 21.31
76 na katika kabila ya Naftali; Kedeshi katika Galilaya pamoja na viunga vyake, na Hamothi pamoja na viunga vyake, na Kiriathaimu pamoja na viunga vyake.
Josué 21.32 Josué 20.7 Juges 4.6 Josué 19.37 Josué 12.22
77 Nao mabaki ya Walawi, wana wa Merari, wakapewa, katika kabila ya Zabuloni; Rimona pamoja na viunga vyake, na Tabori pamoja na viunga vyake;
Josué 21.34-21.35
78 na ng’ambo ya mto wa Yordani huko Yeriko, upande wa mashariki wa Yordani, katika kabila ya Reubeni; Bezeri katika nyika pamoja na viunga vyake, na Yahasa pamoja na viunga vyake,
Josué 20.8 Josué 21.36-21.37 Deutéronome 4.41-4.43
79 na Kedemothi pamoja na viunga vyake, na Mefaathi pamoja na viunga vyake;
80 na katika kabila ya Gadi; Ramothi katika Gileadi pamoja na viunga vyake, na Mahanaimu pamoja na viunga vyake;
Genèse 32.2 2 Rois 9.1 2 Samuel 19.32 1 Rois 22.3-22.28 2 Samuel 17.24
81 na Heshboni pamoja na viunga vyake, na Yazeri pamoja na viunga vyake.
Josué 21.39 Nombres 32.3 Nombres 32.1 Nombres 21.25 Josué 13.25-13.26

Cette Bible est dans le domaine public.