Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 27.4
Bible en Swahili de l’est


Chefs d’armée de David

1 Basi wana wa Israeli kwa hesabu yao, wakuu wa mbari za mababa, na maakida wa maelfu na wa mamia, na wasimamizi wao waliomtumikia mfalme, kwa neno lo lote la zamu za kuingia na za kutoka mwezi kwa mwezi, miezi yote ya mwaka, wa kila zamu, walikuwa watu ishirini na nne elfu.
Exode 18.25 Michée 5.2 Deutéronome 1.15 1 Rois 4.7 1 Rois 5.14
2 Juu ya zamu ya kwanza ya mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu, mwana wa Zabdieli; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
2 Samuel 23.8 1 Chroniques 11.11
3 Yeye alikuwa wa wana wa Peresi, mkuu wa maakida wote wa jeshi mwezi wa kwanza.
Nombres 26.20 Nombres 7.12 Nombres 10.14 Genèse 38.29 Genèse 49.8-49.10
4 Na juu ya zamu ya mwezi wa pili alikuwa Dodai, Mwahohi, na zamu yake; na Miklothi alikuwa amiri; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
2 Samuel 23.9 1 Chroniques 11.12
5 Akida wa tatu wa jeshi mwezi wa tatu alikuwa Benaya, mwana wa Yehoyada, kuhani; alikuwa mkuu, na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
1 Chroniques 18.17 1 Rois 4.4-4.5
6 Huyo Benaya ndiye yule aliyekuwa shujaa wa wale thelathini, na juu ya wale thelathini; na katika zamu yake alikuwa Amizabadi mwanawe.
2 Samuel 23.20-23.23 2 Samuel 22.20-22.23 1 Chroniques 11.22-11.25
7 Akida wa nne wa mwezi wa nne alikuwa Asaheli, nduguye Yoabu, na Zebadia mwanawe baada yake; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
1 Chroniques 11.26 2 Samuel 23.24 2 Samuel 2.18-2.23
8 Akida wa tano wa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi, Mwizrahi; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
1 Chroniques 11.27 2 Samuel 23.25 1 Chroniques 26.29
9 Akida wa sita wa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi, Mtekoi; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
1 Chroniques 11.28 2 Samuel 23.26
10 Akida wa saba wa mwezi wa saba alikuwa Heksi, Mpeloni, wa wana wa Efraimu; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
1 Chroniques 11.27 2 Samuel 23.26
11 Akida wa nane wa mwezi wa nane alikuwa Sibekai, Mhushathi, wa Wazera; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
2 Samuel 21.18 1 Chroniques 11.29 Nombres 26.20
12 Akida wa kenda wa mwezi wa kenda alikuwa Abiezeri, Mwanathothi, wa Wabenyamini; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
1 Chroniques 11.28 2 Samuel 23.27
13 Akida wa kumi wa mwezi wa kumi alikuwa Maharai, Mnetofathi, wa Wazera; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
1 Chroniques 11.30 2 Samuel 23.28
14 Akida wa kumi na moja wa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya, Mpirathoni, wa wana wa Efraimu; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
1 Chroniques 11.31 2 Samuel 23.30
15 Akida wa kumi na mbili wa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heledi, Mnetofathi, wa Othnieli; na katika zamu yake walikuwa watu ishirini na nne elfu.
2 Samuel 23.29 1 Chroniques 4.13 Juges 3.9 1 Chroniques 11.30

Chefs des tribus d’Israël

16 Tena wakuu wa kabila za Israeli walikuwa hawa; wa Wareubeni, Eliezeri mwana wa Zikri; wa Wasimeoni, Shefatia mwana wa Maaka;
17 wa Lawi, Hashabia mwana wa Kemueli; wa Haruni, Sadoki;
1 Chroniques 26.30 1 Chroniques 24.4 1 Chroniques 24.31 1 Chroniques 12.27-12.28
18 wa Yuda, Elihu, mmojawapo wa nduguze Daudi; wa Isakari, Omri mwana wa Mikaeli;
1 Samuel 17.29 1 Samuel 16.6 1 Samuel 17.13
19 wa Zabuloni, Ishmaya mwana wa Obadia; wa Naftali, Yeromothi mwana wa Azrieli;
20 wa wana wa Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia, wa nusu kabila ya Manase, Yoeli mwana wa Pedaya;
21 wa nusu kabila ya Manase katika Gileadi, Ido mwana wa Zekaria; wa Benyamini, Yaasieli mwana wa Abneri;
2 Samuel 3.27 1 Samuel 14.50-14.51 1 Rois 4.14 2 Samuel 3.37
22 wa Dani, Azareli mwana wa Yerohamu. Hao walikuwa maakida wa kabila za Israeli.
1 Chroniques 28.1
23 Lakini Daudi hakufanya hesabu yao wenye miaka ishirini na waliopungua; kwa kuwa Bwana alikuwa amesema, ya kwamba atawaongeza Israeli mfano wa nyota za mbinguni.
Genèse 15.5 Hébreux 11.12 Nombres 1.18 1 Chroniques 21.2-21.5
24 Yoabu, mwana wa Seruya, akaanza kuhesabu, lakini hakumaliza; na ghadhabu ikawapata Israeli kwa hayo; wala haikuhesabiwa hesabu hiyo ndani ya taarifa za mfalme Daudi.
2 Samuel 24.1-24.15 1 Chroniques 21.1-21.17

Administrateurs et conseillers de David

25 Na juu ya hazina za mfalme alikuwa Azmawethi mwana wa Adieli; na juu ya hazina za mashambani, za mijini, na vijijini, na ngomeni, alikuwa Yonathani mwana wa Uzia;
2 Chroniques 16.2 2 Rois 18.15 2 Chroniques 26.10 Genèse 41.48 Jérémie 41.8
26 na juu ya hao wenye kazi ya shamba kuilima ardhi alikuwa Ezri mwana wa Kelubu;
27 na juu ya mashamba ya mizabibu alikuwa Shimei, Mramathi; na juu ya mazao ya mizabibu kwa ghala za mvinyo alikuwa Zabdi, Mshifmi;
28 na juu ya mizeituni na mikuyu iliyokuwamo katika Shefela alikuwa Baal-hanani, Mgederi; na juu ya ghala za mafuta alikuwa Yoashi;
1 Rois 10.27 2 Chroniques 1.15 1 Rois 20.27 1 Rois 4.7
29 na juu ya makundi ya ng’ombe waliolishwa katika Sharoni alikuwa Shitrai, Msharoni; na juu ya makundi waliokuwamo mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai;
1 Chroniques 5.16 Esaïe 65.10
30 na juu ya ngamia alikuwa Obili, Mwishmaeli; na juu ya punda alikuwa Yedeya, Mmeronothi;
Job 1.3 Genèse 47.6
31 na juu ya makundi ya kondoo alikuwa Yazizi, Mhagri. Hao wote walikuwa maakida wa akiba alizokuwa nazo mfalme Daudi.
1 Chroniques 5.10
32 Naye Yonathani, mjombawe Daudi, alikuwa mshauri, na mtu wa akili, na mwandishi; Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa pamoja na wana wa mfalme;
2 Samuel 21.21 1 Chroniques 11.11 2 Samuel 13.3
33 na Ahithofeli alikuwa mshauri wake mfalme; na Hushai, Mwarki, alikuwa rafiki yake mfalme;
2 Samuel 15.12 2 Samuel 15.37 2 Samuel 15.32 Psaumes 55.13 2 Samuel 16.16-16.17
34 na, baada ya Ahithofeli, walikuwa Yehoyada mwana wa Benaya, na Abiathari; na jemadari wa jeshi la mfalme alikuwa Yoabu.
1 Chroniques 11.6 1 Rois 1.7 1 Chroniques 27.5

Cette Bible est dans le domaine public.