Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 2.18
Bible en Swahili de l’est


Enlèvement d’Élie

1 Ikawa, hapo Bwana alipopenda kumpandisha Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya alitoka Gilgali pamoja na Elisha.
Genèse 5.24 Hébreux 11.5 1 Rois 19.16-19.21 1 Rois 19.11 Josué 5.9
2 Eliya akamwambia Elisha, Tafadhali, kaa hapa; maana Bwana amenituma niende mpaka Betheli.
1 Samuel 1.26 2 Rois 2.6 1 Rois 12.29 2 Rois 4.30 2 Rois 2.4
3 Elisha akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha, Basi wakashuka mpaka Betheli. Basi wana wa manabii, waliokuwako Betheli, wakatoka kuonana na Elisha, wakamwambia, Je! Unajua ya kuwa Bwana atamwondoa bwana wako leo, asiwe mkubwa wako? Akasema, Naam, najua; nyamazeni.
2 Rois 4.1 2 Rois 4.38 2 Rois 9.1 1 Rois 20.35 1 Samuel 19.20
4 Eliya akamwambia, Tafadhali, kaa hapa, Elisha; maana Bwana amenituma niende mpaka Yeriko. Akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha. Nao wakafika Yeriko.
2 Rois 2.2 Josué 6.26 1 Rois 16.34 2 Rois 4.30 Actes 11.23
5 Basi wana wa manabii, waliokuwako Yeriko, wakamkaribia Elisha, wakamwambia, Je! Unajua ya kuwa Bwana atamwondoa bwana wako leo, asiwe mkubwa wako? Akajibu, Naam, najua, nyamazeni.
2 Rois 2.3 Luc 24.51 Genèse 48.19 Habakuk 2.20 Actes 26.25
6 Eliya akamwambia, Tafadhali kaa hapa; maana Bwana amenituma niende mpaka Yordani. Akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha. Wakaendelea mbele wote wawili.
2 Rois 2.2 Josué 3.15
7 Basi watu hamsini wa wale wana wa manabii wakaenda wakasimama, kuwakabili kwa mbali; na hao wawili wakasimama karibu na Yordani.
2 Rois 2.17 1 Rois 18.4 1 Rois 18.13
8 Eliya akalitwaa vazi lake la juu, akalikunja, akayapiga maji, yakagawanyika huku na huku, na hao wawili wakavuka pakavu.
1 Rois 19.19 2 Rois 2.14 Exode 14.21-14.22 1 Rois 19.13 Esaïe 11.15
9 Hata ikawa, walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, Omba kwangu lo lote utakalo nikutendee, kabla sijaondolewa kwako. Elisha akasema, Nakuomba, sehemu maradufu ya roho yako na iwe juu yangu.
Nombres 11.17 Deutéronome 21.17 Nombres 11.25 1 Timothée 5.17 Nombres 27.16-27.23
10 Akasema, Umeomba neno gumu; lakini, ukiniona nitakapoondolewa kwako, utalipata; la hukuniona, hulipati.
Actes 1.9-1.10 Marc 11.22-11.24 Jean 16.24 2 Rois 2.12
11 Ikawa, walipokuwa wakiendelea mbele na kuongea, tazama! Kukatokea gari la moto, na farasi wa moto, likawatenga wale wawili; naye Eliya akapanda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli.
2 Rois 6.17 Psaumes 104.3-104.4 Psaumes 68.17 Hébreux 1.14 Zacharie 6.1-6.8
12 Naye Elisha akaona, akalia, Baba yangu, baba yangu, gari la Israeli na wapanda farasi wake! Asimwone tena kabisa; akashika mavazi yake mwenyewe, akayararua vipande viwili.
2 Rois 13.14 Ephésiens 4.8 Proverbes 11.11 Job 1.20-1.21 Ecclésiaste 9.16-9.18
13 Kisha akaliokota lile vazi la Eliya lililomwangukia, akarudi, akasimama katika ukingo wa Yordani.
1 Rois 9.26 1 Rois 19.19 2 Rois 2.8
14 Akalitwaa lile vazi la Eliya lililomwangukia, akayapiga maji, akasema, Yuko wapi Bwana, Mungu wa Eliya? Naye alipoyapiga maji, yakagawanyika huku na huku, Elisha akavuka.
Psaumes 42.10 Psaumes 115.2 Jean 14.12 Actes 3.12-3.13 1 Rois 18.36-18.39
15 Na hao wana wa manabii, waliokuwako Yeriko wakimkabili, walipomwona, walisema, Roho ya Eliya inakaa juu ya Elisha. Wakaja kuonana naye, wakainama kifudifudi mbele yake.
1 Pierre 4.14 Actes 1.8 2 Rois 4.1-4.4 Nombres 27.20 Jean 15.26-15.27
16 Wakamwambia, Angalia, wako hapa pamoja nasi watumishi wako watu hamsini walio hodari; waende, twakuomba, wamtafute bwana wako; isiwe labda roho ya Bwana imemtwaa na kumtupa juu ya mlima mmoja, au katika bonde moja. Akasema, Msiwatume.
1 Rois 18.12 Actes 8.39 Ezéchiel 3.14 2 Corinthiens 12.2-12.3 Ezéchiel 40.2
17 Wakamsisitiza hata akaona haya, akasema, Haya! Watumeni. Basi wakatuma watu hamsini; nao wakatafuta siku tatu, wasimwone.
2 Rois 8.11 Hébreux 11.5 Romains 10.2 2 Samuel 18.22-18.23 Luc 11.8
18 Wakamrudia, alipokuwa anakawia Yeriko; akawaambia, Je! Mimi sikuwaambia, Msiende?
19 Watu wa mjini wakamwambia Elisha, Angalia, twakusihi, mahali pa mji huu ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo; lakini maji yake hayafai, na nchi huzaa mapooza.
1 Rois 18.7 Deutéronome 28.15-28.18 Deutéronome 28.11 Josué 6.17 Exode 15.23
20 Akasema, Nileteeni chombo kipya, mtie chumvi ndani yake. Wakamletea.
Juges 9.45 Sophonie 2.9 Ezéchiel 47.11
21 Akatoka akaenda mpaka chemchemi ya maji, akatupa ile chumvi humo ndani, akasema, Bwana asema hivi, Nimeyaponya maji haya; hakutatoka huko tena kufa wala kuzaa mapooza.
2 Rois 4.41 2 Rois 6.6 Exode 15.25-15.26 Lévitique 2.13 Apocalypse 22.2-22.3
22 Hivyo yale maji yakapona hata leo, sawasawa na neno la Elisha alilolinena.
23 Akakwea kutoka huko mpaka Betheli; naye alipokuwa akienda njiani, wakatoka vijana katika mji, wakamfanyizia mzaha, wakamwambia, Paa wewe mwenye upaa! Paa wewe mwenye upaa!
2 Chroniques 36.16 Job 30.1 Job 19.18 Galates 4.29 Psaumes 31.18
24 Akatazama nyuma akawaona, akawalaani kwa jina la Bwana. Wakatoka dubu wawili wa kike mwituni, wakawararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.
Proverbes 28.15 2 Corinthiens 10.6 Deutéronome 28.15-28.26 1 Rois 20.36 Actes 5.5
25 Akatoka huko akaenda mlima wa Karmeli, na toka huko akarudi mpaka Samaria.
2 Rois 4.25 1 Rois 18.19-18.20 1 Rois 18.42

Cette Bible est dans le domaine public.