Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 13.2
Bible en Swahili de l’est


1 Na tazama, akatoka mtu wa Mungu katika Yuda kwa neno la Bwana, akafika Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa akisimama penye madhabahu, afukize uvumba.
2 Rois 23.17 1 Rois 12.32-12.33 1 Rois 12.22 1 Thessaloniciens 4.15 1 Rois 13.26
2 Basi mtu huyo akapiga kelele juu ya madhabahu, kwa neno la Bwana akasema, Ee madhabahu, madhabahu, Bwana asema hivi, Angalia, mtoto atazaliwa katika nyumba ya Daudi, jina lake Yosia; na juu yako atawachinja makuhani wa mahali pa juu, wanaofukiza uvumba juu yako, na mifupa ya watu itateketezwa juu yako.
Ezéchiel 38.4 Esaïe 48.5-48.7 Esaïe 46.10 2 Rois 22.1-22.2 Esaïe 42.9
3 Akatoa ishara siku ile ile, akasema, Hii ndiyo ishara aliyoinena Bwana, Tazama, madhabahu itapasuka, na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.
1 Corinthiens 1.22 Exode 4.3-4.5 Juges 6.17 Jean 2.18 Esaïe 38.22
4 Ikawa, mfalme Yeroboamu alipoyasikia maneno ya yule mtu wa Mungu, alipopiga kelele juu ya madhabahu huko Betheli, alinyosha mkono wake pale madhabahuni, akasema, Mkamateni. Basi ule mkono wake aliounyosha ukakatika, wala hakuweza kuurudisha kwake tena.
Jean 18.6 Marc 14.44-14.46 Matthieu 26.57 Actes 13.8-13.11 Jérémie 26.8-26.11
5 Madhabahu ikapasuka, majivu ya madhabahuni yakamwagika, sawasawa na ishara aliyoitoa mtu wa Mungu kwa neno la Bwana.
Actes 5.1-5.10 1 Rois 22.28 Nombres 16.23-16.35 Exode 9.18-9.25 1 Rois 13.3
6 Mfalme akajibu, akamwambia yule mtu wa Mungu, Umsihi sasa Bwana, Mungu wako, ukaniombee, ili nirudishiwe mkono wangu tena. Yule mtu wa Mungu akamwomba Bwana mkono wa mfalme ukarudishwa tena, ukawa kama ulivyokuwa kwanza.
Actes 8.24 Exode 8.8 Exode 9.28 Exode 10.17 Luc 6.27-6.28
7 Mfalme akamwambia mtu wa Mungu, Karibu nyumbani kwangu ujiburudishe, nami nitakupa thawabu.
2 Rois 5.15 1 Samuel 9.7-9.8 1 Pierre 5.2 Actes 8.18-8.20 Genèse 18.5
8 Mtu wa Mungu akamwambia mfalme, Ujaponipa nusu ya nyumba yako, sitaingia pamoja nawe, wala sitakula chakula, wala sitakunywa maji mahali hapa;
Nombres 24.13 Nombres 22.18 2 Corinthiens 11.9-11.10 1 Rois 13.16-13.17 2 Rois 5.16
9 maana ndivyo nilivyoagizwa kwa neno la Bwana, kusema, Usile chakula cho chote wala usinywe maji, wala usirudi kwa njia ile uliyoijia.
Ephésiens 5.11 1 Rois 13.1 Jean 15.14 Jean 15.9-15.10 Jean 13.17
10 Basi akaenda zake kwa njia nyingine, wala hakurudi kwa njia ile aliyoijia Betheli.
11 Basi nabii mmoja mzee alikuwa akikaa katika Betheli; na wanawe wakamwendea wakamwambia kila neno alilolitenda yule mtu wa Mungu siku ile katika Betheli; na maneno aliyomwambia mfalme, hayo nayo walimwambia baba yao.
2 Rois 23.18 1 Samuel 10.11 2 Pierre 2.16 Ezéchiel 13.2 Ezéchiel 13.16
12 Baba yao akawaambia, Amekwenda zake kwa njia ipi? Kwa maana wanawe walikuwa wameiona njia ile aliyoiendea yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda.
13 Akawaambia wanawe, Nitandikieni punda. Wakamtandikia punda, naye akampanda.
Juges 5.10 1 Rois 13.27 2 Samuel 19.26 Nombres 22.21 Juges 10.4
14 Akamfuata mtu wa Mungu, akamkuta ameketi chini ya mwaloni, akamwambia, Je! Wewe ndiwe yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda? Akamwambia, Mimi ndiye.
1 Rois 19.4 1 Corinthiens 4.11-4.12 Philippiens 4.12-4.13 2 Corinthiens 11.27 Jean 4.6
15 Akamwambia, Karibu kwangu nyumbani, ule chakula.
16 Naye akamwambia, Siwezi kurudi pamoja nawe, wala kuingia pamoja nawe; wala sili chakula wala sinywi maji pamoja nawe hapa;
1 Rois 13.8-13.9 Matthieu 4.10 Nombres 22.19 Matthieu 16.23 Genèse 3.1-3.3
17 kwani nimeambiwa kwa neno la Bwana, Usile chakula wala usinywe maji huko, wala usirudi kwa njia ile uliyoijia.
1 Rois 20.35 1 Thessaloniciens 4.15 1 Rois 13.1
18 Akamwambia, Mimi nami ni nabii kama wewe, na malaika akaniambia kwa neno la Bwana, kusema, Mrudishe pamoja nawe nyumbani kwako, ale chakula, akanywe maji. Lakini alisema uongo.
1 Jean 4.1 Matthieu 7.15 Nombres 22.35 2 Corinthiens 11.13-11.15 Ezéchiel 13.9-13.10
19 Basi mtu yule akarudi pamoja naye, akala chakula, akanywa maji nyumbani mwake.
Deutéronome 13.3 Deutéronome 13.5 Deutéronome 18.20 Deutéronome 13.1 Actes 4.19
20 Hata ikawa, walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia nabii yule aliyemrudisha;
Jean 11.51 Nombres 24.16-24.24 Matthieu 7.22 Nombres 23.16 1 Corinthiens 13.2
21 akamlilia yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda, akinena, Bwana asema hivi, Kwa sababu umeiasi kauli ya Bwana, wala hukuishika amri ile aliyokuamuru Bwana, Mungu wako,
Galates 1.8-1.9 2 Samuel 6.7 Jérémie 2.19 1 Samuel 4.18 Esther 6.13
22 bali umerudi, ukala chakula ukanywa maji, hapo alipokuambia, Usile chakula, wala usinywe maji; maiti yako haitaliingia kaburi la baba zako.
Jérémie 22.18-22.19 Esaïe 14.18-14.20 2 Chroniques 21.19-21.20 1 Rois 14.13 1 Rois 13.30
23 Basi ikawa, alipokwisha kula chakula na kunywa maji, yule nabii aliyemrudisha akamtandikia punda.
24 Na alipokuwa amekwenda zake, simba alimkuta njiani, akamwua. Maiti yake ikatupwa njiani, na yule punda akasimama karibu naye; na yule simba naye akasimama karibu na maiti.
1 Rois 20.36 Proverbes 22.13 Proverbes 26.13 1 Pierre 4.17-4.18 2 Rois 2.24
25 Na tazama, watu wakapita, wakauona mzoga umetupwa njiani, na yule simba akisimama karibu na mzoga, wakaenda, wakatoa habari katika mji ule alimokaa yule nabii mzee.
1 Rois 13.11
26 Na yule nabii aliyemrudisha njiani alipopata habari, akasema; Ndiye yule mtu wa Mungu, aliyeiasi kauli ya Bwana; kwa hiyo Bwana amempambanisha na simba, simba akamrarua, akamwua, sawasawa na neno la Bwana alilomwambia.
2 Samuel 12.14 Hébreux 12.28-12.29 Lévitique 10.3 Proverbes 11.31 1 Corinthiens 11.30
27 Akawaambia wanawe, akasema, Nitandikieni punda. Wakamtandikia.
28 Akaenda, akamwona yule maiti ametupwa njiani, na punda na simba wamesimama karibu na maiti; yule simba alikuwa hakumla maiti, wala hakumrarua punda.
Daniel 3.27-3.28 Jérémie 5.22-5.23 Job 38.11 Psaumes 148.7-148.8 Lévitique 10.5
29 Nabii yule akamtwaa maiti wa yule mtu wa Mungu, akamweka juu ya punda wake, akamrudisha; yule nabii mzee akaenda mjini mwake, kukaa matanga, na kumzika.
30 Akamweka maiti katika kaburi lake mwenyewe; wakamlilia, wakisema, Aa! Ndugu yangu!
Jérémie 22.18 Actes 8.2 1 Rois 14.13
31 Hata ikawa, alipokwisha kumzika, akawaambia wanawe, akasema, Nikifa mimi, nizikeni katika kaburi hili alimozikwa yule mtu wa Mungu; iwekeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.
2 Rois 23.17-23.18 Luc 16.22-16.23 Nombres 23.10 Ecclésiaste 8.10 Psaumes 26.9
32 Kwa maana neno hilo alilolia juu ya madhabahu katika Betheli, kwa neno la Bwana, na juu ya nyumba zote za mahali pa juu zilizo katika miji ya Samaria, hakika litatimizwa.
1 Rois 16.24 1 Rois 13.2 1 Rois 12.31 Lévitique 26.30 2 Rois 23.16-23.19
33 Baada ya hayo Yeroboamu hakuiacha njia yake mbovu, lakini akafanya tena makuhani wa mahali pa juu, wa watu wo wote.
2 Chroniques 13.9 2 Chroniques 11.15 Amos 6.11 Nombres 1.51 1 Rois 12.31-12.33
34 Kila aliyetaka akamfanya wakfu, ili wawepo makuhani wa mahali pa juu. Jambo hilo likawa dhambi kwa nyumba ya Yeroboamu, hata kuiharibu, na kuifuta usoni pa nchi.
1 Rois 12.30 1 Rois 14.10 2 Rois 17.21 1 Rois 15.29-15.30 2 Rois 10.31

Cette Bible est dans le domaine public.