Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 16.9
Bible en Swahili de l’est


Naissance d’Ismaël

1 Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri.
Galates 4.24 Genèse 12.16 Genèse 15.2-15.3 Genèse 21.21 Genèse 25.21
2 Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, Bwana amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai.
Genèse 30.6 Genèse 3.17 Genèse 25.21 Exode 21.4 Ruth 4.11
3 Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe.
Genèse 12.4-12.5 Genèse 16.5 Genèse 25.6 Galates 4.25 1 Rois 11.3
4 Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake.
1 Corinthiens 4.6 1 Samuel 1.6-1.8 1 Corinthiens 13.4-13.5 2 Samuel 6.16 Proverbes 30.23
5 Sarai akamwambia Abramu, Ubaya ulionipata na uwe juu yako; nimekupa mjakazi wangu kifuani mwako, naye alipoona kwamba amepata mimba, mimi nimekuwa duni machoni pake. Bwana na ahukumu kati ya mimi na wewe.
Genèse 31.53 Exode 5.21 2 Chroniques 24.22 Psaumes 7.8 Psaumes 43.1
6 Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake.
Proverbes 27.8 Proverbes 14.29 Exode 2.15 Genèse 13.8-13.9 1 Pierre 3.7
7 Malaika wa Bwana akamwona kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri.
Genèse 25.18 Exode 15.22 Genèse 21.17 Genèse 22.15 1 Samuel 15.7
8 Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai.
Genèse 3.9 Ecclésiaste 10.4 Genèse 4.10 1 Timothée 6.1-6.2 Jérémie 2.17-2.18
9 Malaika wa Bwana akamwambia, Rudi kwa bibi yako, ukanyenyekee chini ya mikono yake.
1 Pierre 5.5-5.6 Ephésiens 5.21 Tite 2.9 1 Pierre 2.18-2.25 Ecclésiaste 10.4
10 Malaika wa Bwana akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi.
Genèse 17.20 Genèse 22.15-22.18 Genèse 25.12-25.18 Genèse 21.13 Actes 7.30-7.38
11 Malaika wa Bwana akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana Bwana amesikia kilio cha mateso yako.
Exode 3.7 Exode 2.23-2.24 Luc 1.31 Matthieu 1.21-1.23 Genèse 29.32-29.35
12 Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.
Genèse 25.18 Job 39.5-39.8 Genèse 21.20 Job 11.12 Genèse 27.40
13 Akaliita jina la Bwana aliyesema naye, Wewe U Mungu uonaye, kwani alisema, Hata hapa nimemwona yeye anionaye?
Genèse 32.30 Psaumes 139.1-139.12 Proverbes 15.3 Proverbes 5.21 Genèse 28.17
14 Kwa hiyo kisima kile kiliitwa Beer-lahai-roi.Tazama,kiko kati ya kadeshi na beredi.
Nombres 13.26 Genèse 24.62 Genèse 25.11 Genèse 21.31 Genèse 14.7
15 Hajiri akamzalia Abramu mwana wa kiume; Abramu akamwita jina lake Ishmaeli, yule mwanawe, ambaye Hajiri alimzaa.
Genèse 25.12 Genèse 37.27 Genèse 16.11 Genèse 17.18 Galates 4.22-4.23
16 Naye Abramu alikuwa mtu wa miaka themanini na sita, hapo Hajiri alipomzalia Abramu Ishmaeli.

Cette Bible est dans le domaine public.