Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 15.15
Bible en Swahili de l’est


Renouvellement des promesses à Abram

1 Baada ya mambo hayo neno la Bwana likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.
Esaïe 41.10 Genèse 26.24 Psaumes 84.11 Psaumes 119.114 Lamentations 3.24
2 Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini, nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu Eliezeri, Mdameski?
Actes 7.5 Genèse 25.21 Genèse 30.1-30.2 Genèse 39.9 Genèse 39.4-39.6
3 Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu.
Genèse 14.14 Proverbes 29.21 Ecclésiaste 2.7 Proverbes 13.12 Hébreux 10.35-10.36
4 Nalo neno la Bwana likamjia likinena, Huyu hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi.
Genèse 17.16 Galates 4.28 2 Chroniques 32.21 2 Samuel 7.12 Genèse 21.12
5 Akamleta nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu. Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.
Romains 4.18 Deutéronome 1.10 Hébreux 11.12 Exode 32.13 Genèse 22.17
6 Akamwamini Bwana, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.
Jacques 2.23 Galates 3.6-3.14 Romains 4.9 Romains 4.3-4.6 Romains 4.11
7 Kisha akamwambia, Mimi ni Bwana, niliyekuleta kutoka Uru wa Wakaldayo nikupe nchi hii ili uirithi.
Néhémie 9.7-9.8 Genèse 12.1 Psaumes 105.42 Psaumes 105.44 Actes 7.2-7.4
8 Akasema, Ee Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi?
Luc 1.18 Esaïe 7.11 2 Rois 20.8 Juges 6.36-6.40 Psaumes 86.17
9 Akamwambia, Unipatie ndama wa miaka mitatu, na mbuzi mke wa miaka mitatu, na kondoo mume wa miaka mitatu, na hua, na mwana njiwa.
Lévitique 14.22 Luc 2.24 Lévitique 14.30 Lévitique 9.4 Lévitique 9.2
10 Akampatia hao wote, akawapasua vipande viwili, akaweka kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege hakuwapasua.
Lévitique 1.17 Jérémie 34.18-34.19 2 Timothée 2.15 Genèse 15.17
11 Hata tai walipotua juu ya mizoga Abramu akawafukuza.
Matthieu 13.4 Ezéchiel 17.3 Psaumes 119.13 Ezéchiel 17.7
12 Na jua lilipokuwa likichwa usingizi mzito ulimshika Abramu, hofu ya giza kuu ikamwangukia.
Genèse 2.21 Daniel 10.8-10.9 Job 33.15 Psaumes 4.3-4.5 1 Samuel 26.12
13 Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne.
Actes 7.6-7.7 Galates 3.17 Exode 12.40-12.41 Psaumes 105.23-105.25 Exode 1.11
14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi.
Exode 6.5-6.6 Deutéronome 6.22 Deutéronome 11.2-11.4 Deutéronome 7.18-7.19 1 Samuel 12.8
15 Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema.
Job 5.26 2 Chroniques 34.28 Genèse 23.19 Genèse 23.4 Genèse 25.7-25.9
16 Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado.
1 Rois 21.26 Daniel 8.23 Matthieu 23.32-23.35 1 Thessaloniciens 2.16 Exode 12.40
17 Ikawa, jua lilipokuchwa likawa giza, tazama, tanuru ya moshi na mwenge unaowaka ulipita kati ya vile vipande vya nyama.
Jérémie 34.18-34.19 Juges 6.21 1 Chroniques 21.26 Deutéronome 4.20 Juges 13.20
18 Siku ile Bwana akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,
Deutéronome 1.7-1.8 Genèse 12.7 Néhémie 9.8 Exode 23.27-23.31 Nombres 34.5
19 Mkeni, na Mkenizi, na Mkadmoni,
Nombres 24.21-24.22
20 na Mhiti, na Mperizi, na Mrefai,
Genèse 14.5 Esaïe 17.5
21 na Mwamori, na Mkanaani, na Mgirgashi, na Myebusi.
Exode 33.2 Exode 34.11 Matthieu 8.28 Exode 23.23-23.28 Genèse 10.15-10.19

Cette Bible est dans le domaine public.