Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 13.2
Bible en Swahili de l’est


Séparation d’avec Lot

1 Abramu akapanda kutoka Misri, yeye, na mkewe, na kila alichokuwa nacho, na Lutu pamoja naye, mpaka kusini.
2 Samuel 24.7 Genèse 21.33 Genèse 12.9-12.20 1 Samuel 27.10 Josué 10.40
2 Naye Abramu alikuwa ni tajiri sana kwa mifugo, kwa fedha, na kwa dhahabu.
Genèse 24.35 Psaumes 112.1-112.3 Proverbes 10.22 Job 1.3 Job 1.10
3 Akaendelea kusafiri kutoka kusini mpaka Betheli, mahali pale palipokuwapo hema yake kwanza kati ya Betheli na Ai;
Genèse 12.6 Genèse 12.8-12.9
4 napo ndipo palipokuwa na madhabahu aliyofanya hapo kwanza; naye Abramu akaliitia jina la Bwana hapo.
Genèse 12.7-12.8 Ephésiens 6.18-6.19 Jérémie 29.12 1 Corinthiens 1.2 Psaumes 84.10
5 Na Lutu aliyesafiri pamoja na Abramu, yeye naye alikuwa na makundi ya ng’ombe na kondoo, na hema.
Jérémie 49.29 Genèse 25.27 Genèse 4.20
6 Na ile nchi haikuwatosha, ili wakae pamoja; maana mali zao zilikuwa nyingi, hata wasiweze kukaa pamoja.
Genèse 36.6-36.7 1 Timothée 6.9 Ecclésiaste 5.10-5.11 Luc 12.17-12.18
7 Kukawako ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abramu, na wachunga wanyama wa Lutu; na siku zile Wakanaani na Waperizi walikuwa wakikaa katika nchi.
Genèse 12.6 Genèse 26.20 Genèse 21.25 1 Thessaloniciens 4.12 Exode 2.17
8 Abramu akamwambia Lutu, Basi, usiwepo ugomvi, nakusihi, kati ya mimi na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wachungaji wako; maana sisi tu ndugu.
Psaumes 133.1 Actes 7.26 1 Corinthiens 6.6-6.7 Ephésiens 4.2-4.3 Genèse 11.27-11.31
9 Je! Nchi hii yote haiko mbele yako? Basi ujitenge nami, nakusihi; ukienda upande wa kushoto, nitakwenda upande wa kuume; ukienda upande wa kuume, nitakwenda upande wa kushoto.
Genèse 20.15 Genèse 34.10 1 Pierre 3.8-3.12 1 Corinthiens 6.7 Hébreux 12.14
10 Lutu akainua macho yake, akaliona Bonde lote la Yordani, ya kwamba lote pia lina maji, kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora, lilikuwa kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri hapo unapokwenda Soari.
Deutéronome 34.3 Esaïe 51.3 Genèse 14.8 Joël 2.3 Genèse 14.2
11 Basi Lutu akajichagulia Bonde lote la Yordani; Lutu akasafiri kwenda upande wa mashariki; wakatengana wao kwa wao.
Genèse 13.9 Genèse 13.14 Genèse 19.17 1 Pierre 2.17 Psaumes 119.63
12 Abramu akakaa katika nchi ya Kanaani, na Lutu akakaa katika miji ya lile Bonde; akajongeza hema yake mpaka Sodoma.
Genèse 19.29 Genèse 14.12 Genèse 19.25 1 Corinthiens 15.33 2 Pierre 2.7-2.8
13 Lakini watu wa Sodoma walikuwa wabaya, wenye kufanya dhambi nyingi sana juu ya Bwana.
Genèse 18.20 Jude 1.7 Matthieu 9.13 Hébreux 4.13 2 Pierre 2.10

Nouvelles promesses à Abram

14 Bwana akamwambia Abramu, alipokwisha kutengana na Lutu, Inua sasa macho yako, ukatazame kutoka hapo ulipo, upande wa kaskazini, na wa kusini na wa mashariki na wa magharibi;
Deutéronome 3.27 Genèse 28.14 Esaïe 49.18 Genèse 13.10 Esaïe 60.4
15 maana nchi hii yote uionayo, nitakupa wewe na uzao wako hata milele.
Genèse 12.7 Actes 7.5 2 Chroniques 20.7 Genèse 24.7 Deutéronome 34.4
16 Na uzao wako nitaufanya uwe kama mavumbi ya nchi; hata mtu akiweza kuyahesabu mavumbi ya nchi, uzao wako nao utahesabika.
Nombres 23.10 Genèse 28.14 Genèse 32.12 Genèse 22.17 Genèse 15.5
17 Ondoka, ukatembee katika nchi hii katika mapana yake, na marefu yake, maana nitakupa wewe nchi hiyo.
Nombres 13.17-13.24 Genèse 13.15
18 Basi Abramu akajongeza hema yake, akaja akakaa kwenye mialoni ya Mamre, nayo ni miti iliyoko Hebroni, akamjengea Bwana madhabahu huko.
Genèse 14.13 Genèse 8.20 Genèse 35.27 Genèse 18.1 Genèse 12.7-12.8

Cette Bible est dans le domaine public.